DOWANS (BEHIND THE SHADOWS): What you were not supposed to know...!

Why JMK has to do that? Go to BRELA: BRELA-Home

Aisee, kuweni wajanja kama nyoka, watu wapo kazini na wanajua wanachokifanya hapa. Msikubali kuhamishwa kirahisi, Thread iendelee, jikaze kisabuni, kubali changamoto, lakini thread iendelee. Happy new year all
 
Mkuu, Waswahili wanasema "mwenye macho haambiwi kodoa"..

Welcome back sir, tuko pamoja... Nimejaribu kusoma hiyo document iliyowekwa na Invisible (ruling of the ICC), labda sijaona vizuri, lakini naona hiyo document ni ile iliyochakachuliwa. Original ruling ya ICC inasema kuwa Dowans wamempa Rostam Aziz power of attorney kupokea malipo kwa niaba ya Dowans. Sasa mbona sijaona jina la Rostam kwenye document yako, au nimeangalia haraka haraka. Ukweli ni kuwa the full ICC ruling inamtaja Rostam moja kwa moja, ndiyo maana wanasita kuipeleka High Court hiyo complete ICC ruling iwe registered kwani itakuwa ni public document na Rostam ataanikwa.

Kinachotolewa sasa hivi ni ruling ya ICC ambayo imechakachuliwa ili kuficha jina la Rostam.

Hiyo ya Dowans shadow uliyoweka wewe naona ni kesi kati ya Gire wa RDEVCO ya Houston Marekani na Dowans (Rostam) wakidaiana turbines zilizonunuliwa kwa $7.5m. RDEVCO wanasema wao walizilipia na wamewaandikia barua TANESCO kuwatahadharisha kuwa turbines hizo si mali ya Dowans ni za RDEVCO. On the other hand, Dowans wanasema walipochukua mkataba kutoka kwa Richmond, hizo turbines zilikuwa bado hazijanunuliwa na walilipa wao kwa pesa zao. Ni matapeli wawili wanafanya usanii tu hapa.
 
daresalaam, apuuzwe anatumia hiyo mbinu kutuhamisha kifikra. Asante invisible na mm.

Hakuna cha kuwahamisha fikra, nawaambia ukweli na ukweli mtupu. Haya ya Dowans tulibishana sana humu, rejea post za nyuma, tulisema hawa jamaa, watashinda kesi, na sasa tumeona. Yaani ilikuwa haina haja hata ya kufikiria ni kitu kilikuwa wazi. Mitambo imefika, mitambo mingine ni brand new, imeletwa haraka haraka na midege mikubwa ambayo ndio mara ya kwanza ituwe kiwanjani kwetu, mi Antonov.

thumbnail.aspx


Sasa nyie kwa fikira zenu, mlitaka hawa wafanya biashara waachie tu, wasidai kusitishwa mkataba? siwaelewi!

Kama ni madudu kuhusu umeme yalifanywa toka awamu ya kwanza, ya pili, ya tatu! Huyu JMK aliyeliona tatizo akaona afanye kila njia kulitatuwa ndio kawa mbaya? na Jee, hamkuona jinsi alivyolishughulikia hilo suala? For the First Time in The History of Tanzania, Waziri Mkuu na Mawaziri wengine nje. Nani alieweza kufanya hayo kabla ya JMK?
 
taratibu mkuu usije ukasahau katiba inaruhusu watu kuwa na mawazo tofauti ili mradi hawavunji sheria

Hapo umenena, hiyo ni haki ya msingi ya kila mtu, nami nikiwemo! Ingawa awamu ya kwanza ilitubana na katiba yetu! Unafikiri wakati wa Nyerere tungekuwepo hapa JF? duhhh, hata TV tulikuwa hatuna, magazeti ndio hivyo tena, Uhuru, Mzalendo na Ngurumo!

Halafu leo JMK mbaya!
 
.....ok ok ''pumba'' imemwagwa......wewe mipovu inakutoka hovyo hovyo kwa nini?

Hahahahahaaaaaaaa, mipovu? ni mimi au wamwaga pumba na watetea pumba ndio wanahaha mpaka wanapindisha ukweli!
 
"wajinga ndio waliwao" hiyo kujibu swali lako la kwanza.

Picha ipi wewe? watu wanadai haki zao humo, wee unafikiri utavunja tuu mikataba ya watu? Dowans lazima walipwe na wale waliowakopesha Dowans hiyo mitambo lazima walipwe. Usifikiri watu wanafanya biashara za kizamani za kuficha chini ya uvungu!

Si humu JF ndio mlikuwa mnashabikia Dowans wafutiwe mikata na mitambo isinunuliwe, tukasema, na hata mbunge wenu Zitto akasema "inunuliwe"! Great Tinkers waka-kataa! sasa mnalia nini? mlishindwa great thinkers na kujuwa consequences zake?

Ushauri wa bure: Kaeni chini na Dowans, wataelewa tatizo, lakini msijidai ubabe, enzi za ubabe zimekwisha! Hamsomi makosa ya zamani?

Nyerere alijidai ubabe kwa makaburu waliokuwa wanaunganisha materekta akawafungia akasema "sirudi" nyuma ntageuka "jiwe"! alivyoona mambo yamemkalia vibaya, kwani wale jamaa walikuwepo kihalali kabisa, akaona bora ageuke jiwe, akawawacha waendelee na shughuli zao.

Na haya ya Dowans tungejifunza kwa Nyerere! mbona hajageuka jiwe?


Inaonyesha hujasoma hizo document hapo juu, serikali ya Tanzania isingeweza kununua hizo jenereta kutoka kwa DOWANS kwani kampuni ya
REDVCO iliclaim ya kuwa hiyo mitambo ni ya kwake! Na kama serikali ingenunua hiyo mitambo kitu kingechofuata kingekuwa ni lawsuit tuu.
 
Wakuu nimejaribu kui down load hiyo document lakini nimeshindwa kuipata, kila nikifungua file linakuja kwenye window media then mashine yangu inaniambia, file lipo corrupt, please kama kuna mtu anaweza nisaidia anipe maelekezo. otherwise, asante sana mzee mwanakiji na invisible kwa kazi ya kizalendo mlioifanya. Mungu awazidishie.
 
Ahsante Mzee wa kijiji kwa kututanabaisha na taarifa hizi. Mwaka huu naona umeanza vibaya sana kwa mkulu..
 
Yaani mijitu mingine kwa kumwaga pumba! sasa hizo documents ndio zinasaidia nini na ni siri ipi? mbona zipo wazi tu hizo!

Mijitu mingine basi humu inashangilia hata haijuwi inacho-kishangilia na mkjj anawapata kweli. "ama kweli wajinga ndio waliwao".

Mambo yanaendelea, TZS 5,000 unapata 8kwhr. DAR ES SALAAM mkuu mbona unapenda kutuua!!!
Ada January, Umeme juu, Gesi juu, maji hakuna, kwetu hulali bila feni!! Tulikuwa tumezoea kunua umeme kwa ajili ya feni usiku, sasa mnataka tulaleje...!!!
 
Halafu eti akina Werema wanasema Mjadara umefungwa? labda haya hawajui ...Richmond na Dowans wote Uduwanzi tu wa ku-take advantage ya ujinga wetu Watanzania...Jameni wapeni basi akina werema, Tanesco na interested parties ili mambo hayo wayaone..

Wasiwasi wangu ni Kwamba : HAYA mambo ya Kesi ya DOWANS na Richmond yayaweza kumwangusha Kikwete... leo (LEO TU) nimekuwa Shiekh Yahya wa JF..
 
Ukitaka kujua kina cha ufisadi nchi ni pale unaposoma Enclosures one and two .........ambazo kwa makusudi mazima zinatamka ya kuwa uamuzi wa Msuluhishi ni wa mwisho........hivi vifungu vinakinzana na katiba yetu kabisa.........................haiwezekani masilahi ya taifa yakamalizwa na msuluhishi na Tanesco inapokubali hivyo ni dhahiri mlungula mkubwa ulilambishwa kwao........................This is criminal negligence............................Hawa watu wote ni wa kuwasekwa mahakamani tu......................
 
Yaani mijitu mingine kwa kumwaga pumba! sasa hizo documents ndio zinasaidia nini na ni siri ipi? mbona zipo wazi tu hizo!

Mijitu mingine basi humu inashangilia hata haijuwi inacho-kishangilia na mkjj anawapata kweli. "ama kweli wajinga ndio waliwao".

For once may you stop thinking using your a#@$!!
 
Katika Enclosures one and two vile vile Tanesco wamekubali kutohoji maamuzi ya msuluhishi yaani walijuaje kama Msuluhishi huyo angetoa uamuzi wa haki......................How did they agree to lock tanesco into speculative manipulations........................

Hakuna mtu yeyote mwenye akili timamu ambaye atakwenda kwa msuluhishi na kusema ya kuwa anakubali uamuzi wa msuluhishi na ya kuwa hataupinga hata kabla ya kujua msuluhishi ataamuaje?

Mahakama Kuu siku nyingi ilikwisha kukataa kuzuiwa na mkataba wowote ule kuuchunguza kwa sababu uhalali wa kusimamia haki unatokana na katiba...............................sijui hivi vipengele waliviweka kumtishia nani?

These clauses are simply redundant...............................and quite useless....ila zinasaidia kutuonyesha kina cha ufisadi ndani ya nchi hii..................
 
Ujinga mtupu,
natumia cm ya mchna,nijuzeni, ati kikwete katajwa kuwa mmiliki wa Dowans au?

Shule inakusumbua Rostam katajwa? Kikwete is the brain behind the rubbish. If not he is nuts he does not know what is going on around him. THE TRUTH NI UJINGA WA CCM KUTAKA FEDHA ZA AIBU NA CHAFU KUTOKA HATA KWA WEZI KWA AJILI YAKUGH'AGH'ANIA KUBAKI MADARAKANI.

Kifupi ukitaka kujua umasikini ndiyo huo KUKOSA UWEZO WA KUFANYA MAAMUZI SAHIHI
 
Dar es salaam siyo MJINGA. Mjinga ni yule anayetaka kubishana naye.

Mwanakijiji, ndiyo maana tulikumiss sana. Umeanza mwaka mpya powa sana.

Kidogo kidogo hadi kitaelewa. Ngoja niifungue na nisome.
 
Enclosure No 5 inatisha kabisa...........ni kwa misingi ipi Waziri Mkuu wa wakati huo Edward Lowassa by 12th June 2008 aliandika barua ya kuwa fedha za madai ya DOWANS ziwekwe kwenye Escrow Account........was he contemplating DOWANS will utlimately be paid the said colossal sums?

Hivi Lowassa hapa anaweza kujieleza vipi? ikumbukwe mgogoro wa tanesco na DOWANS umetokana na Tanesco kuzuia mitambo yao......Wakati huo Lowassa was no longer PM ......................However, it seems........... Lowassa had already plotted to breach the contract as far as 12th June 2008?

Mbona hii inatisha sana? Tutapona kweli na huu utawala wa kizandiki?
 
Clause 14. 1 (b).....ndiyo msalaba wa DOWANS.............................walikubaliana ya kuwa sheria za Tanzania ndizo zitaongoza usuluhishi na sheria zetu zipo wazi.........no contractual agreement ousting the jurisdiction of Tanzanian Courts will ever be entertained...............

Kwa hiyo vifungu vyote vinavyozuia Mahakama zetu kuchunguza haya makubaliano vinakinzana na katiba yetu.....i.e they are unconstitutional.....................and ought to be stricken out with costs...................
 
Hapo umenena, hiyo ni haki ya msingi ya kila mtu, nami nikiwemo! Ingawa awamu ya kwanza ilitubana na katiba yetu! Unafikiri wakati wa Nyerere tungekuwepo hapa JF? duhhh, hata TV tulikuwa hatuna, magazeti ndio hivyo tena, Uhuru, Mzalendo na Ngurumo!

Halafu leo JMK mbaya!

TV haikuletwa na JMK


Uhuru, Mzalendo na Ngurumo! Magazeti ya JMK na wewe usijisahau na ANNUR
 
mh hayaa tuone kama wanasheria wetu wanauelewa na sheria zetu maana naona kama hizo facts za humo hawatazielewa ila ni maoni yangu tutasikia tu.
 
Back
Top Bottom