nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
JUMATATU, OCTOBA 01, 2012 04:59 NA KHAMIS MKOTYA
Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa
MWENYEKITI wa Chama cha UPDP, Fahmi Dovutwa, amemshangaa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa, kutokana na uamuzi wake wa kutoa angalizo kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Dovutwa alisema Dk. Slaa hakupaswa kutoa angalizo hilo, kwani kufanya hivyo kunaonyesha wazi kuwa kiongozi huyo si mpinzani wa kweli na pia lengo lake ni kutaka CCM iendelee kubaki madarakani.
Dovutwa, ambaye aligombea urais mwaka 2010, amekosoa kauli ya Dk Slaa ambayo aliitoa hivi karibuni akiwa jijini Mwanza, akisema kuwa CCM inakufa kutokana na kushindwa kujisafisha na tuhuma za ufisadi kupitia uchaguzi wake wa ndani.
Dk. Slaa alisema kuwa chama hicho kikongwe sasa kimeonyesha dalili za wazi za kifo, kwa kushindwa kuwaengua katika uchaguzi wa NEC, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Mbunge wa Bariadi Mgharibi, Andrew Chenge, ambao ni watuhumiwa wakubwa wa ufisadi.
"Dk. Slaa hana dhamira ya dhati ya kutaka CCM iondoke madarakani, kama yeye anaona kurudishwa NEC kwa akina Lowassa na Chenge ndiyo kifo cha CCM hakupaswa kusema hayo.
"Alipaswa kunyamaza ili waweze kuishughulikia CCM na mwisho wa siku Chadema ishinde uchaguzi iingie Ikulu, lakini kwa maneno hayo ni sawa na kuifungua macho CCM, hivi wakisimamisha mtu strong (anayekubalika) Chadema itapitia mlango gani kuingia Ikulu?
"Kauli ya Dk. Slaa inashangaza na imevitia doa vyama vya upinzani, hii inaonyesha kumbe Dk Slaa anaogopa na hataki CCM ianguke mwaka 2015, swali la kujiuliza huyu bwana anamfanyia kazi nani? Nilitarajia Dk Slaa angefurahia CCM kuanguka ili Chadema iingie Ikulu, lakini yeye anasikitika CCM inakufa.
"Hivi CCM ikifa Dk. Slaa anaathirika na nini hadi atoe angalizo? CCM inatakiwa kufa kama UNIP (chama) ya Kaunda ilivyokufa Zambia au MMD ya Banda ilivyokufa Malawi au UPC ya Obote ilivyokufa kule Uganda," alisema Dovutwa.
Dovutwa alisema kuwa kauli hiyo inaonyesha kuwa Dk. Slaa bado ana mapenzi na CCM, licha ya kujitoa katika chama hicho mwaka 1995, vinginevyo atoe ufafanuzi kuhusu mantiki ya kutoa hoja ya angalizo na kuishauri CCM.
Kwa mujibu wa Dovutwa, akiwa Mwanza Dk. Slaa pia alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wakati akiwa bungeni aliwahi kumtaka Lowassa amtaje mtu aliyesababisha yeye awajibike kisiasa kwa kujiuzulu, ili kwa kufanya hivyo chama chake kiweze kumsafisha na tuhuma za ufisadi.
"Kwa maneno haya, Dk. Slaa alikuwa amejipanga kucheza mchezo mchafu baada ya Lowassa kumkatalia kumtaja huyo mtu, hii inaonyesha kuwa Dk. Slaa anafanya siasa za chuki za kulazimisha," alisema.
Mwenyekiti wa UPDP, Fahmi Dovutwa
MWENYEKITI wa Chama cha UPDP, Fahmi Dovutwa, amemshangaa Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Dk. Willbrod Slaa, kutokana na uamuzi wake wa kutoa angalizo kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari jana, Dovutwa alisema Dk. Slaa hakupaswa kutoa angalizo hilo, kwani kufanya hivyo kunaonyesha wazi kuwa kiongozi huyo si mpinzani wa kweli na pia lengo lake ni kutaka CCM iendelee kubaki madarakani.
Dovutwa, ambaye aligombea urais mwaka 2010, amekosoa kauli ya Dk Slaa ambayo aliitoa hivi karibuni akiwa jijini Mwanza, akisema kuwa CCM inakufa kutokana na kushindwa kujisafisha na tuhuma za ufisadi kupitia uchaguzi wake wa ndani.
Dk. Slaa alisema kuwa chama hicho kikongwe sasa kimeonyesha dalili za wazi za kifo, kwa kushindwa kuwaengua katika uchaguzi wa NEC, Mbunge wa Monduli, Edward Lowassa na Mbunge wa Bariadi Mgharibi, Andrew Chenge, ambao ni watuhumiwa wakubwa wa ufisadi.
"Dk. Slaa hana dhamira ya dhati ya kutaka CCM iondoke madarakani, kama yeye anaona kurudishwa NEC kwa akina Lowassa na Chenge ndiyo kifo cha CCM hakupaswa kusema hayo.
"Alipaswa kunyamaza ili waweze kuishughulikia CCM na mwisho wa siku Chadema ishinde uchaguzi iingie Ikulu, lakini kwa maneno hayo ni sawa na kuifungua macho CCM, hivi wakisimamisha mtu strong (anayekubalika) Chadema itapitia mlango gani kuingia Ikulu?
"Kauli ya Dk. Slaa inashangaza na imevitia doa vyama vya upinzani, hii inaonyesha kumbe Dk Slaa anaogopa na hataki CCM ianguke mwaka 2015, swali la kujiuliza huyu bwana anamfanyia kazi nani? Nilitarajia Dk Slaa angefurahia CCM kuanguka ili Chadema iingie Ikulu, lakini yeye anasikitika CCM inakufa.
"Hivi CCM ikifa Dk. Slaa anaathirika na nini hadi atoe angalizo? CCM inatakiwa kufa kama UNIP (chama) ya Kaunda ilivyokufa Zambia au MMD ya Banda ilivyokufa Malawi au UPC ya Obote ilivyokufa kule Uganda," alisema Dovutwa.
Dovutwa alisema kuwa kauli hiyo inaonyesha kuwa Dk. Slaa bado ana mapenzi na CCM, licha ya kujitoa katika chama hicho mwaka 1995, vinginevyo atoe ufafanuzi kuhusu mantiki ya kutoa hoja ya angalizo na kuishauri CCM.
Kwa mujibu wa Dovutwa, akiwa Mwanza Dk. Slaa pia alinukuliwa na vyombo vya habari akisema wakati akiwa bungeni aliwahi kumtaka Lowassa amtaje mtu aliyesababisha yeye awajibike kisiasa kwa kujiuzulu, ili kwa kufanya hivyo chama chake kiweze kumsafisha na tuhuma za ufisadi.
"Kwa maneno haya, Dk. Slaa alikuwa amejipanga kucheza mchezo mchafu baada ya Lowassa kumkatalia kumtaja huyo mtu, hii inaonyesha kuwa Dk. Slaa anafanya siasa za chuki za kulazimisha," alisema.