Doufu Ndani ya Majani ya Yungiyungi

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Feb 3, 2009
42,299
33,080
Mapishi ya kuchemsha doufu kwa mvuke ndani ya majani ya yungiyungi


Mahitaji
0808.jpg


Doufu gramu 300, nyama ya kuku gramu 30, uyoga gramu 10, uyoga mweusi gramu 10, yai moja, vipande vya paja la ash la nguruwe gramu 10, majani ya yungiyungi, chumvi kijiko kimoja, sukari kijiko kimoja, vipande vya vitunguu maji na tangawizi kila kimoja gramu 5, mafuta ya ufuta kijiko kimoja, wanga wa pilipili manga kijiko kimojra, siki kijiko kimoja, mchuzi wa sosi vijiko viwili, mharadali kijiko kimoja

Njia:

1. kata kata doufu iwe kama iliyosagwa, saga nyama ya kuku. Kata uyoga na uyoga mweusi viwe vipande vipande. Koraga yai halafu washa moto mimina mafuta kwenye sufuria, mimina yai lililokorogwa kwenye sufuria likaange. Halafu lipakue na vikata liwe vipande vipande.
2. koroga doufu, nyama ya kuku, vipande vya paja la ash la nguruwe, uyoga, chumvi, sukari, vipande vya vitunguu maji na tangawizi, mafuta ya ufuta, wanga wa pilipili manga, siki, mchuzi wa sosi na mharadal, halafu weka kwenye majani ya yungiyungi, weka vipande vya yai na uyoga mweusi. Washa moto tena mimina maji kwenye sufuria weka majani ya yungiyungi kwenye sufuria chemsha kwa mvuke kwa dakika 10, ipakua. Mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.


Mapishi ya kukaanga uyoga

mashrooms.jpg


Mahitaji

Uyoga gramu 150, unga gramu 80, chembechembe za kukoleza ladha gramu 2, chumvi iliyokorogwa pamoja na pilipili manga gramu 2, ute wa mayai mawili

Njia

1. kata uyoga uwe vipande vipande, koroga pamoja na chembechembe za kukoleza ladha, chumvi na unga. Koroga ute wa mayai na unga.
2. washa moto mimina mafuta kwenye sufuria, mpaka yawe nyuzi ya joto la 50, weka vipande vya uyoga kwenye ute wa mayai na unga halafu weka kwenye sufuria vikaange mpaka viwe rangi ya hudhurungi, vipakue. Mimina chumvi iliyokorogwa pamoja na pilipili manga kwenye uyoga, mpaka hapo kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.

Mapishi ya samaki na bilinganya


Mahitaji
20060609121731919_3.jpg

Samaki mmoja, bilinganya moja, chumvi vijiko viwili, chembechembe za kukoleza ladha kijiko kimoja, mchuzi wa sosi vijiko viwili, pilipili manga kijiko kimoja, vipande vya vitunguu maji, pilipili hoho, tangawizi , sosi ya pilipili hoho vijiko viwili.

Njia

1. ondoa vitu vilivyo ndani ya tumbo la samaki, halafu osha samaki na kumkata awe vipande.
2. kata bilinganya liwe vipande. Washa moto weak sufuria motoni, tia vipande vya bilinganya vikaange halafu vipakue.
3. tia vipande vya tangawizi na sosi ya pilipili hoho korogakoroga, halafu tia vipande vya samaki korogakoroga, mimina maji baada ya kuchemka, tia chumvi, chembechembe za kukoleza ladha, korogakoroga, tia vipande vya bilingaya, na pilipili hoho korogakoroga halafu punguza moto kidogo, baada ya dakika 15, tia mchuzi wa sosi na maji ya wanga korogakoroga, ipakue. Tia vipande vya vitunguu maji na pilipili hoho. Mpaka hapa kitoweo hiki kiko tayari kuliwa.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom