Don't trust even your shadow!

Jaguar

JF-Expert Member
Mar 6, 2011
3,438
1,026
Siku moja bwana Mungo park alifika kando ya mto niger akiwa na farasi wake.Alimfunga yule farasi kwenye mti wa karibu kisha akaenda kuoga mtoni.Alipokuwa akirudi,alielekea kule alikomwacha farasi wake lakini huku macho yake yakitazama mandhari maridadi ya ule mto.Alipofika pale chini ya mti,bila kumtazama 'farasi', alimshika mgongoni.Kwa kushangazwa na mabadiliko ya mguso wa mgongo,alishusha macho na kukutana uso kwa uso na sura ya nyamaume(simba dume).Ule mgongo alioushika ulikuwa ni wa simba ambaye aliyekwisha mrarua farasi dakika chache zilizopita.Mungo aliwahi bunduki yake na alifanikiwa kumuua yule simba.duh!yatupasa kuwa makini kila sekunde ya maisha yetu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom