Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,890
- 6,896
Kitendo cha shule zinazomilikiwa na Mchungaji Rwekatare kuhusishwa na kashfa ya kuiba unit za Luku Tanesko ni jambo la kushtusha, na pengine kuna mengi zaidi kwa wakubwa uchunguzi ukifanyika, huyu ni dagaa tu.
Mmiliki wa shule hizo akiwa Mbunge na mchungaji ingawa haimhusinshi moja kwa moja au hajatajwa wazi wazi, lakini ananaswa na kitanzi cha umiliki wa shule hizo, jambo ambalo alitakiwa kuwa na uangalifu wa hali ya juu kufuatili matumizi na mapato ya shule zake kwamba hayawezi kuleta utata wo wote, na hata bodi za shule hizo zimeshindwa kufuatilia kinachoendelea kuliibia shirika la umeme mapato.
Mbunge ambaye ana tenda ya kuuzia TANESCO matairi ya magari si kazi kumpata, tuvute subira kwani ataanikwa na wajuaji soon hapa jamvini. Huyo ana kashfa nzito zaidi kuliko Rwakatare.
Kwa vyo vyote wabunge ambao wametoka kifua mbele kutetea hatua za Waziri wa Nishati na Madini kusafisha shirika kuna kila dalili za kuhusika na ufisadi ndani ya shirika hili, wengi wao ni wajanja wajanja ambao hutumia njia za panya ili wasishikwe kirahisi, lakini zipo njia nyingi tu za kuwanasa, moja wapo kauli zao zimeshawatilia doa tayari kabla utafiti haukajamilika, ingwa wamejenga utetezi wa kwamba walitetea taratibu zifanyike.