nonino
Member
- Apr 11, 2012
- 32
- 12
Kuna mtoto wa ndugu yangu msichana yuko chuoni tayari,kuna mvulana wanasoma naye wako very close,mara nyingi nawakutaga au nawaona katika mikao yenye utata,sasa kwa vile nilishawahi kumuuliza kama ana rafiki wa kiume akanijibu hana na siku akipata boyfriend ataniambia,sasa nilivyomuona na huyo kijana,ikabidi nimuulize mwenzangu vipi ndio tayari umepata,jibu alilonipa limeniacha hoi;akasema yule sio mpenzi wangu lakini ni zaidi ya rafiki,nikashindwa hata kuendelea kuuliza,maana nina uhakika yeye na huyo kijana wameshakutana kimwili mara nyingi tu,kuna siku nilimsikia akimsimulia shosti wake hapa home,wakijua mi nimelala. Hebu nielezeni jamani ,mtu wa opposite sex kuwa zaidi ya rafiki kwako ndio inakuwaje kuwaje?