kilimo ni uti wa mgongo wa nchi yetu hilo liko wazi. Ila wimbo huu unaonekana kutokuwa na maana hasa kwangu kwa viongozi wetu kugawa ardhi nzuri yenye rutuba kwa wageni( eti wawekezaji) kuja kupanda mazao ya mafuta kama Jatropha.Maeneo mengi ya rutuba kama kisarawe na bagamoyo wamepewa 'eti wawekezaji' waje kuvuna mafuta huku mlala hoi akiwa amefukuzwa kwenye maeneo hayo.
Nani ambaye hataniambia huu ni ukoloni wa 'pili' tena wa aina yake. Kwani walivyokuja mwanzo si walitaka ardhi na tukawapandia mazao 'malighafi' na wakapeleka kwao.
Inasikitisha kuona viongozi wetu hawalioni hili, wakati huku kwao ulaya walishajitosheleza kwa chakula, na kwa sababu wengi wa vinchi vyao sio vikubwa 'kwa eneo ' kama ya kwangu TZ' basi wanafanya kila hila, wanawalaghai tunaowahita viongozi.
Nani ambaye hajui kwamba watanzania wanakufa kwa njaa? Mimea kama Jatropha inahitaji rutuba nyingi na mpaka ivunwe inachukua miaka na mbaya zaidi ikishavuwa udongo unabaki bila rutuba yeyote.Matokeo yake tutawalimia na kuwategemea kwa chakula.Labda utajiuliza ndani ya nyumba yako ulikosa chakula inakuwaje?
Nani ambaye hataniambia huu ni ukoloni wa 'pili' tena wa aina yake. Kwani walivyokuja mwanzo si walitaka ardhi na tukawapandia mazao 'malighafi' na wakapeleka kwao.
Inasikitisha kuona viongozi wetu hawalioni hili, wakati huku kwao ulaya walishajitosheleza kwa chakula, na kwa sababu wengi wa vinchi vyao sio vikubwa 'kwa eneo ' kama ya kwangu TZ' basi wanafanya kila hila, wanawalaghai tunaowahita viongozi.
Nani ambaye hajui kwamba watanzania wanakufa kwa njaa? Mimea kama Jatropha inahitaji rutuba nyingi na mpaka ivunwe inachukua miaka na mbaya zaidi ikishavuwa udongo unabaki bila rutuba yeyote.Matokeo yake tutawalimia na kuwategemea kwa chakula.Labda utajiuliza ndani ya nyumba yako ulikosa chakula inakuwaje?