Candid Scope
JF-Expert Member
- Nov 8, 2010
- 11,883
- 6,884
Wabunge wangaka
Wabunge jana waligeuka mbogo wakiitaka Ofisi ya Spika, kuchukua hatua kukomesha kile walichokiita unyanyasaji unaofanywa dhidi yao na polisi katika matukio ya kuwakamata wanapohusishwa na uvunjaji wa sheria.
Habari kutoka ndani ya kikao cha kutoa mwongozo kwa wabunge kuhusu Mkutano wa Tano wa Bunge kilichofanyika jana katika ukumbi wa Pius Msekwa, Dodoma zinasema kuwa wabunge waliochangia hoja hiyo walisema ukamataji unaofanywa na polisi kwa wabunge unaonekana kudhamiria kuwadhalilisha badala ya kusimamia sheria.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Pauline Gekul ndiye aliyeibua hoja hiyo huku akiitaka Ofisi ya Spika kuchukua hatua za kuwaondolea wabunge adha hiyo na kadri mjadala ulivyoendelea, suala hilo liliungwa mkono na wabunge wa kambi zote.
Aliposimama Gekul kuzungumza baadhi ya wabunge walidhani kwamba pengine ni hoja ya wapinzani kuwatetea wabunge wa Chadema waliokamatwa Arusha, kwa hiyo baadhi yetu walikuwa kama wanaguna vile, lakini baadaye ilibainika kwamba kamatakatama hiyo imewakumba wabunge wote wa upinzani na wa CCM, alisema mbunge mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe.
Wabunge wengine waliotajwa kuzungumzia hoja hiyo ni Livingstone Lusinde wa Mtera (CCM), Murtaza Mangungu- Kilwa Kaskazini (CCM), Israel Natse- Karatu (Chadema) na Christopher Akunaay- Mbulu (Chadema).Kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao walisema kwa nyakati tofauti kwamba mbunge anapotenda kosa anaweza kuarifiwa kwamba anahitajika kituo cha polisi na yeye kwenda bila kushurutishwa.
Mbunge hawezi kutoroka au kuwakimbia polisi, dhamana aliyonayo ni kubwa kwanza wapigakura waliomchagua, Bunge kama taasisi na hata chama chake cha siasa, sasa huwezi kusema unamtafuta mbunge kama anavyoweza kumsaka mhalifu mwingine ambaye hatambuliki. Huu ni udhalilishaji, alisema mbunge mwingine ambaye pia aliomba jina lake lihifadhiwe.Spika Anne Makinda aliahidi kuwasiliana na vyombo vya usalama ili vifuate utaratibu wakati wanapotaka kuwakamata wabunge kutokana na makosa mbalimbali wanayofanywa.
Miongoni mwa taratibu ambazo wabunge wamekuwa wakitaka zifuatwe ni Ofisi ya Spika kuarifiwa kabla ya kukamatwa na kuitwa kwenda polisi wenyewe badala yakufuatwa na idadi kubwa ya askari.
Hata hivyo, Spika aliwataka wabunge kwa upande wao kuwa makini kwa kuzingatia sheria na uhusiano mwema na vyombo vya dola ili kuepusha misuguano baina ya mihimili ya Bunge na Serikali.
Habari hii imeandikwa na Peter Saramba, Arusha, Hussein Issa, Dar na Neville Meena, Dodoma.
Mwananchi
Wabunge jana waligeuka mbogo wakiitaka Ofisi ya Spika, kuchukua hatua kukomesha kile walichokiita unyanyasaji unaofanywa dhidi yao na polisi katika matukio ya kuwakamata wanapohusishwa na uvunjaji wa sheria.
Habari kutoka ndani ya kikao cha kutoa mwongozo kwa wabunge kuhusu Mkutano wa Tano wa Bunge kilichofanyika jana katika ukumbi wa Pius Msekwa, Dodoma zinasema kuwa wabunge waliochangia hoja hiyo walisema ukamataji unaofanywa na polisi kwa wabunge unaonekana kudhamiria kuwadhalilisha badala ya kusimamia sheria.
Kwa mujibu wa habari hizo, Mbunge wa Viti Maalumu (Chadema), Pauline Gekul ndiye aliyeibua hoja hiyo huku akiitaka Ofisi ya Spika kuchukua hatua za kuwaondolea wabunge adha hiyo na kadri mjadala ulivyoendelea, suala hilo liliungwa mkono na wabunge wa kambi zote.
Aliposimama Gekul kuzungumza baadhi ya wabunge walidhani kwamba pengine ni hoja ya wapinzani kuwatetea wabunge wa Chadema waliokamatwa Arusha, kwa hiyo baadhi yetu walikuwa kama wanaguna vile, lakini baadaye ilibainika kwamba kamatakatama hiyo imewakumba wabunge wote wa upinzani na wa CCM, alisema mbunge mmoja ambaye hakutaka jina lake liandikwe.
Wabunge wengine waliotajwa kuzungumzia hoja hiyo ni Livingstone Lusinde wa Mtera (CCM), Murtaza Mangungu- Kilwa Kaskazini (CCM), Israel Natse- Karatu (Chadema) na Christopher Akunaay- Mbulu (Chadema).Kwa mujibu wa taarifa hizo, wabunge hao walisema kwa nyakati tofauti kwamba mbunge anapotenda kosa anaweza kuarifiwa kwamba anahitajika kituo cha polisi na yeye kwenda bila kushurutishwa.
Mbunge hawezi kutoroka au kuwakimbia polisi, dhamana aliyonayo ni kubwa kwanza wapigakura waliomchagua, Bunge kama taasisi na hata chama chake cha siasa, sasa huwezi kusema unamtafuta mbunge kama anavyoweza kumsaka mhalifu mwingine ambaye hatambuliki. Huu ni udhalilishaji, alisema mbunge mwingine ambaye pia aliomba jina lake lihifadhiwe.Spika Anne Makinda aliahidi kuwasiliana na vyombo vya usalama ili vifuate utaratibu wakati wanapotaka kuwakamata wabunge kutokana na makosa mbalimbali wanayofanywa.
Miongoni mwa taratibu ambazo wabunge wamekuwa wakitaka zifuatwe ni Ofisi ya Spika kuarifiwa kabla ya kukamatwa na kuitwa kwenda polisi wenyewe badala yakufuatwa na idadi kubwa ya askari.
Hata hivyo, Spika aliwataka wabunge kwa upande wao kuwa makini kwa kuzingatia sheria na uhusiano mwema na vyombo vya dola ili kuepusha misuguano baina ya mihimili ya Bunge na Serikali.
Habari hii imeandikwa na Peter Saramba, Arusha, Hussein Issa, Dar na Neville Meena, Dodoma.
Mwananchi