The Worshiper
JF-Expert Member
- Oct 5, 2012
- 302
- 89
Dodoma ni moja ya mikoa iliyo nyuma kimaendeleo hapa nchini na haufanani kabisa na jina kubwa ililobebeshwa na serikali ya CCM kwamba ni mji mkuu na makao makuu ya serikali.Mambo mengi bado hayako vile inavyotakiwa kuwa kama Mji mkuu,KWAKIFUPI mambo bado sana bila kusahau ndio mkoa unasifika na unaotoa omba omba wengi hapa nchini.
Nimekuwa nikifuatilia sana siasa za nchi hii na zaidi hasa hapa Dodoma.Kwa ujumla mambo yote haya yanachangiwa na serikali ya CCM,kwanza kwakutambua udhaifu wa watu wa mji huu (zaidi wenyeji-wagogo na warangi) katika eneo la ukabila.Siasa za ukabila ziko kwa kiwango chakutisha mno, hapa nazungumzia kwa makabila haya mawili,ni ngumu mno tena mno kwa mtu yeyote kutoka nje ya makabila haya kupenya na kushika nafasi kisiasa kuongoza, hapa haupimwi kwa uwezo ama nia thabiti uliyonayo bali kabila ulilonalo.CCM imetumia udhaifu huu kujenga ngome imara vijijini ambako ndiko walipo watu wengi.Na lugha zinazotumika katika kampeni kushawishi ni za makabila hayo.
CCM pia inatumia ujinga mwingi wa wenyeji wa mkoa huu katika kushinda.Mfano wakati wa kampeni utashuhudia ombaomba wengi (wanajulikana)na vikundi kibao vya ngoma vya akina mama wakiwa wametinga furana na kofia za CCM wakijimwaya kwa nyimbo,ngoma na mapambio wakifurahia shilingi elfu mbili mbili wanazopewa wakiitukuza CCM na kusahau kwa muda shida zao na kuipigia kura ya ushindi.Lakini baada ya kampeni huwa ni kilio na kusaga meno,Ndio kampeni zimeshaisha nguo na elfu mbili mbili watatoa wapi tena ni mpaka baada ya miaka mitano ambapo cha kushangaza huwa wanarudia makosa yaleyale miaka nenda rudi?,ombaomba nao kama kawaida hurejea fani yao nakujaza mitaa tena.Ukweli wengi wa wanaotaka maendeleo na mabadiliko ya kweli ya mkoa huu ni wageni kutoka mikoa mingine na wenyeji walioshika nafasi hakuna chochote wanachofanya.
Hofu ya kufanya mabadiliko na hali ya mazoea ni tatizo pia miongoni mwa wenyeji wa mkoa huu.Wengi ni waoga wa mabadiliko huku hali mbaya ya umasikini ikiwa imeshamiri miongoni mwao,vijiji vingi vipo katika hali mbaya,huku kila mwaka ahadi zikimiminika.Wengi wao wameshaizoea hali mbaya waliyonayo na wanaona hivyo ndivyo wanavyopaswa kuwa.Wao suala la Dodoma kuwa Makao makuu au kutokuwa kwao sio kitu cha msingi sana,hali na gharama ya maisha kupanda kwa kiwango cha juu kwao si jambo la maana,mji kuwa mchafu,umasikini uliotopea wao ni kawaida,kupungua kwa huduma ya maji huku vijijini ikiwa ndiyo taabu kabisa kwao ni sawa na hakuna haja ya kufanya mabadiliko.
Nimekuwa nikifuatilia sana siasa za nchi hii na zaidi hasa hapa Dodoma.Kwa ujumla mambo yote haya yanachangiwa na serikali ya CCM,kwanza kwakutambua udhaifu wa watu wa mji huu (zaidi wenyeji-wagogo na warangi) katika eneo la ukabila.Siasa za ukabila ziko kwa kiwango chakutisha mno, hapa nazungumzia kwa makabila haya mawili,ni ngumu mno tena mno kwa mtu yeyote kutoka nje ya makabila haya kupenya na kushika nafasi kisiasa kuongoza, hapa haupimwi kwa uwezo ama nia thabiti uliyonayo bali kabila ulilonalo.CCM imetumia udhaifu huu kujenga ngome imara vijijini ambako ndiko walipo watu wengi.Na lugha zinazotumika katika kampeni kushawishi ni za makabila hayo.
CCM pia inatumia ujinga mwingi wa wenyeji wa mkoa huu katika kushinda.Mfano wakati wa kampeni utashuhudia ombaomba wengi (wanajulikana)na vikundi kibao vya ngoma vya akina mama wakiwa wametinga furana na kofia za CCM wakijimwaya kwa nyimbo,ngoma na mapambio wakifurahia shilingi elfu mbili mbili wanazopewa wakiitukuza CCM na kusahau kwa muda shida zao na kuipigia kura ya ushindi.Lakini baada ya kampeni huwa ni kilio na kusaga meno,Ndio kampeni zimeshaisha nguo na elfu mbili mbili watatoa wapi tena ni mpaka baada ya miaka mitano ambapo cha kushangaza huwa wanarudia makosa yaleyale miaka nenda rudi?,ombaomba nao kama kawaida hurejea fani yao nakujaza mitaa tena.Ukweli wengi wa wanaotaka maendeleo na mabadiliko ya kweli ya mkoa huu ni wageni kutoka mikoa mingine na wenyeji walioshika nafasi hakuna chochote wanachofanya.
Hofu ya kufanya mabadiliko na hali ya mazoea ni tatizo pia miongoni mwa wenyeji wa mkoa huu.Wengi ni waoga wa mabadiliko huku hali mbaya ya umasikini ikiwa imeshamiri miongoni mwao,vijiji vingi vipo katika hali mbaya,huku kila mwaka ahadi zikimiminika.Wengi wao wameshaizoea hali mbaya waliyonayo na wanaona hivyo ndivyo wanavyopaswa kuwa.Wao suala la Dodoma kuwa Makao makuu au kutokuwa kwao sio kitu cha msingi sana,hali na gharama ya maisha kupanda kwa kiwango cha juu kwao si jambo la maana,mji kuwa mchafu,umasikini uliotopea wao ni kawaida,kupungua kwa huduma ya maji huku vijijini ikiwa ndiyo taabu kabisa kwao ni sawa na hakuna haja ya kufanya mabadiliko.