Do you know who is JOSEPH KABILA?.....read the attached document

Sio siri kuwa kuna watu wa asili ya Kitusi ambao baba zao walikuja siku nyingi kama wakimbizi na kuishi sehemu za mikoa wa Tabora na Kagera na sasa wana nyadhifa kubwa kwenye serikali yetu. Wengine ndio hao uraia wao ulileta utata enzi ya Mkapa na wengine walipewa ubalozi na Kagame mara alipoingia madarakani na wengine ndio wakina Kamanzi na Rutayisire waliokuwa waalimu IFM na UDSM respectively; baada ya Kagame kuingia madarakani wakatoroka na kurudi kwao!! Sasa kama watu wa usalama wa Taifa wangekuwa wanafanya kazi yao vizuri wangeweza kuwatambua hao watu walioinfiltrate serikali kwani inasemekana wapo mpaka kwenye baraza la mawaziri not to mention mashirika nyeti kama EWURA!! Hiyo ndiyo strategy ya kufanikisha BAHIMA empire!!

Katika hivi vi nationstate vya Afrika mashariki vilivyoanza miaka 50-60 iliyopita, ukjianza kuwa trace watu historia zao hakuna atakayebaki Mtanzania.

Utaambiwa Nyerere Mrundi, Mwinyi na Kinana Wasomali, Mkapa anatoka Msumbiji na Kikwete actually ni Mngazijana na Karume ni Mnyasa wa Malawi.

Na Wakurya wanataka kuchukua jeshi while wachagga wanataka kuchukua biashara huku Wasukuma na Wanyakyusa wakigombea nafasi nono kwenye mashirika ya umma.

Na Wanyakyusa si Watanzania hasa kwa sababu asili yao ni Malawi na Zambia, wakati Wasukuma wametokea Zaire.

Ukiangalia sana Wabantu wote si Watanzania kwa sababu walitokea Nyanda za Kaskazini ya Nigeria na Magharibi ya Cameroon.

Sasa tutaishi vipi hapo?
 
Hii stori, iko karibu kama wakongo fulani rafiki zangu walivyonisimulia, Lakini wao walikuwa wanasema Tz ndo imemsimika kabila na wanasema kabila ni mtanzania. Hapo ndo kuna kazi.

Kuhusu abanyarwanda. Pia inabidi kutoisahau historia yani ya kwamba hadi mwaka 1920 tanganyika, rwanda na burundi ilikua nchi moja, na ndio maana ukiangalia kwa makini hawa jamaa kwa namna moja ama nyingine tuko nao karibu nao sana hatuna mawaaaaa nao kama nchi zingine.
 
Hii stori, iko karibu kama wakongo fulani rafiki zangu walivyonisimulia, Lakini wao walikuwa wanasema Tz ndo imemsimika kabila na wanasema kabila ni mtanzania. Hapo ndo kuna kazi.

Kuhusu abanyarwanda. Pia inabidi kutoisahau historia yani ya kwamba hadi mwaka 1920 tanganyika, rwanda na burundi ilikua nchi moja, na ndio maana ukiangalia kwa makini hawa jamaa kwa namna moja ama nyingine tuko nao karibu nao sana hatuna mawaaaaa nao kama nchi zingine.

Mkuu nakubaliana na point kwamba hawa Rwanda na Burundi tuko karibu sana nao na ni wenzetu kwa sababu miaka hiyo ya 1920 sote ilikuwa ni nchi moja. Kilichokuja kuharibu ni wafaransa ambao walipandikiza ukabila kwa wenzetu na hivyo wakaanza kuchukiana.

Lakini kuhusu Joseph Kabila, kuna ukweli kwamba yeye siyo mkongo na ni kweli kwa sababu baba yake siyo LD kabila. Mgogoro wa DRC kwa sasa hauta kwisha kwa sababu unakuwa engineered na Rwanda kupitia UN ili kuwazuia waasi wa kihutu walioko kongo wasirudi kuipindua serikali ya Kigali. UN na US wanajua hilo na baadaye ni kwamba mashariki ya DRC kutakuwepo na eneo huru ambalo litakuwa chini ya uangalizi wa UN lakini litakaliwa na wanyarwanda.
 

Baada ya kuisoma doc hiyo naomba nami nichangie mjadala huu.

Binafsi naona Joseph Kabila siyo kiongozi muafaka wa kuiongoza DRC baada ya miongo minne ya vita na maendeleo duni, pamoja na utajiri mkubwa nchi hiyo iliyobarikiwa.

Ninavyoona, suala kubwa si asili ya kiongozi, achilia mbali iwapo ni mtoto halali (biological son) wa baba – bali uwezo wa kuongoza na kuendeleza watu wake zaidi kwa ku-utilize rasilimali za nchi.

Kuna viongozi foreigners wameongoza nchi nyingine na kuleta maendeleo makubwa – mfano naoupata mara moja hapa ni Mahathir Mohammad aliyeiongoza Malaysia kwa kipindi cha zaidi ya miongo miwili. Yeye alikuwa mhamianji tu kutoka India.

Swali: Jee Kabila katimiza ndoto za watu wa DRC? Sidhani, na hakuna hata dalili ya hilo kwamba makubwa yanatarajiwa -- hata tukisema muda ni mdogo (miaka 7 tangu ashike). Tatizo ni kwamba anachukuwa muda mwingi kujijenga madarakani kuliko kufanya maendeleo.

Kitu alichokosea ni tamaa ya madaraka na kuna kila dalili kwamba hili linasukumwa na mataifa makubwa yenye masilahi nchini humo. Pengine tunashuhudia Mobutu No 2 hapa.

Maandalizi yaliofanywa ya uchaguzi ‘huru' (2006) baada ya miaka mingi ya udikteta, wengi walishauri Kabila asingegombea urais – angebakia tu kama kiongozi wa mpito aliyetayarisha nchi kwa kuiweka katika njia ya demokrasia halisi. Yaani kama vile ilivyotokea kwa Burundi pale Domitien Ndayezeye alipokuwa kiongozi wa mpito.

Kabila hakulitaka hilo, alitaka yeye mwenywe kugombea – na kama tujuavyo jinsi inavyokuwa kwa marais katika Bara la Afrika waliye madarakani kugombea – hushinda tu – kwa kutumia hila zoooote.

Matatizo mapya yakaanza hapo – baada ya 'kushinda' kukawa ugomvi na hasimu wake mkubwa wa kisiasa – Jean Pierre Bemba.

Hapa ndipo nchi za Magharibi wakaingilia na kufanya kamchezo kao ka siku zote – kuhakikisha kwamba mahasimu wao hawaingii madarakani (au hawatawali) katika nchi ambazo kuna masilahi yao.

Wakatumia mbinu kwa kupitia Baraza la Usalama la UN – na ambalo wana ushawishi mkubwa nalo – kuishawishi International Criminal Court kumfungulia mashitaka ya ‘uhalifu wa kivita na mauaji' na hatimaye kupelekwa The Haig.

Ilionekana dhahiri kuwa ilikuwa ni kibarua kikubwa kwa Kabila kuendelea kumshikilia au kumfungulia mashitaka hasimu yake na kumtupa jela nchini DRC kwani bado angekuwa kivuli kikubwa juu yake.

Mtindo huu ndiyo uliyotumiwa kuhusu Bashir wa Sudan – ambaye anatakiwa akamatwe kwa uhalifu wa kivita na mauaji -- na kupelekwa The Hague. Nchi za magharibi zinakosa masilahi nchini Sudan (mafuta yaliyogunduliwa) na hivyo wakalikuza suala la uasi wa Darfur kwa kiasi kikubwa sana.

Ajabu uasi wa aina hiyo uko katika nchi nyingi tu kama vile Ethiopia, Chad, Somalia, Ivory Coast etc. Lakini katika nchi hizi majeshi ya serikali yanapopambana na waasi hao na kuwaua linakuwa si suala kubwa – kwamba marais wa chi hizo wamefanya ‘uhalifu wa kivita na mauaji' katika nchi zao – na kutakiwa kukamatwa -- isipokuwa hili ni sawa kwa Bashir wa Sudan.

Inatia moyo kuona AU iliona upuuzi huo na kupinga kukamatwa kwa Bashir.

Mwaka 2003 Bush na Blair walilizunguuka baraza lao hilo hilo la Usalama la UN walipoona linagoma kuruhusu wao kuvamia Iraq.

Kwa ujeuri tu waliamuru majeshi ya nchi hizo mbili kuingia Iraq na kuua, lakini hadi sasa International Court haijaona umuhimu wa kuwakamata Bush na Blair kwa uhalifu wa kivita na mauaji.

Kwa kumalizia tu, inasikitisha kuona bado nchi za magharibi zina uwezo na mbinu nyingi za kuzitawala nchi zetu kwa kutumia ‘local government' – siyo lazima wao wawepo physically kama wakati ule wa ukoloni.

Mimi naamini kabisa kama kuna uwezekano, nchi za Magharibi zingemshawishi muungwana wetu aendelee tu kutawala – kwani anakidhi kabisa masilahi yao.
 
Mnaodhani tatizo haswa ni ''origins'' za Kabila you are just mistaken..Kuna uzi mwingine ulitotkea hapa JF miezi michache ilopita kuhusu Kaguta M7 nadhani ukiunganisha na hii utaanza kupata picha kamili. Anyways the bottomest of the lines kwene hii bloody pursuit of power struggle in the DRC ni rasilimali zinazokutikana nchini DRC ambazo zinakadiriwa kufikia dola za kimerekani bilioni 200.

Sasa kinachotokea ni kuanzisha struggle ambayo mwisho wa siku ni kuweka mechanism kwa wanene wa dunia kuzichota hizo rasilimali kwa urahisi. We all know RPF started from UG, and after few months in office these strategists waged another vicious war from Kigali to Kinshasa. Mind u uccessfully! Unaeza ukashangaa kanchi kadogo kaa Rwanda kana-engage vita from border with Uganda up to DRC. Kwa wale wataalamu wa jeshi watakuwa wanaelewa gharama za vita, sie vita ya UG ilikuwa unatucost kama 2 mil USD per day na mpaka leo tupo hoi bin taaban.. GO AND FIGURE.
 
Mkuu nakubaliana na point kwamba hawa Rwanda na Burundi tuko karibu sana nao na ni wenzetu kwa sababu miaka hiyo ya 1920 sote ilikuwa ni nchi moja. Kilichokuja kuharibu ni wafaransa ambao walipandikiza ukabila kwa wenzetu na hivyo wakaanza kuchukiana.

Lakini kuhusu Joseph Kabila, kuna ukweli kwamba yeye siyo mkongo na ni kweli kwa sababu baba yake siyo LD kabila. Mgogoro wa DRC kwa sasa hauta kwisha kwa sababu unakuwa engineered na Rwanda kupitia UN ili kuwazuia waasi wa kihutu walioko kongo wasirudi kuipindua serikali ya Kigali. UN na US wanajua hilo na baadaye ni kwamba mashariki ya DRC kutakuwepo na eneo huru ambalo litakuwa chini ya uangalizi wa UN lakini litakaliwa na wanyarwanda.

Mkuu nawakirisha hoja!
Pamoja na yote wanayozungumza ktk pdf hiyo, yawezekana ukweli na wakatia vichorombwezo ambavyo vinaifanya documents isiwe sahihi mbele ya wachambuzi. (Nirekebishe kama nitakua nimekosea) Josee hata alipokua ujanani TZ pia alikuwa anajulikana kwa jina la Josee , tofauti na pdf ilivyoainisha. Pili Josee amechukua mafunzo ya jeshi nchini TZ ktk jeshi letu la jwtz kama sikosei ni kule mbeya. Sasa ukiunganisha hizo doti na jinsi mwandishi alivyoandika historia yake inaonekana ni uongo hata kama alikua anaelezea ukweli.
 
Mkuu nawakirisha hoja!
Pamoja na yote wanayozungumza ktk pdf hiyo, yawezekana ukweli na wakatia vichorombwezo ambavyo vinaifanya documents isiwe sahihi mbele ya wachambuzi. (Nirekebishe kama nitakua nimekosea) Josee hata alipokua ujanani TZ pia alikuwa anajulikana kwa jina la Josee , tofauti na pdf ilivyoainisha. Pili Josee amechukua mafunzo ya jeshi nchini TZ ktk jeshi letu la jwtz kama sikosei ni kule mbeya. Sasa ukiunganisha hizo doti na jinsi mwandishi alivyoandika historia yake inaonekana ni uongo hata kama alikua anaelezea ukweli.

KWELI KABISA KAMA UNAVYOSEMA MKUU, KAMA UNAAMUA KUANDIKA KITU BASI NI BORA UWEKE HISTORIA KAMILI, kuhusu shule ni kweli huyu bWana alisoma Zanaki (A level), nadhani kwenye late 80s na early 90s, nakumbuka kipindi hicho ndio alikuwa Mwanafunzi mvulana pekee katiaka shule ya Wanawake (ZANAKI), lakini hapa nashindwa kujua ilikuwaje serikali (maana alikuwa sponsored na GOV) isimpeleke kwanye shule ambazo zilikuwa na combination anayoitaka, maana by that time shule za wavulana A level Dar zilikuwa ni TAMBAZA (PCB na PCM) na AZANIA (PCM), LAKINI HUYU BWANA KUNA KOZI ALIYOKUWA ANASOMA PALE ZANAKI YA KUUNGAUNGA (NAMAANISHA KOZI ALIYOKUWA ANASOMA HAIKUWEPO ZANAKI, LAKINI ALIKUWA ANAUNGA UNGA MASOMO YA KOZI KAMA MBILI TATU KUTENGENEZA HIYO KOZI YAKE), NA ALIKUWA NI MCHEZAJI MZURI WA KARATE PALE ZANAKI NA KAMA SIJAKOSEA ALIKUWA NA ORANGE AU BROWN BELT, hayo mengine ya huyo bwana mwenye hiyo PDF sina uhakika nayo sana lakini ukiangalia huyo jamaa alipotokea hata hapa TZ na jinsi alivyokuwa basi unaweza kwa kiasi fulqani kuwa 50-50
 
Mkuu nawakirisha hoja!
Pamoja na yote wanayozungumza ktk pdf hiyo, yawezekana ukweli na wakatia vichorombwezo ambavyo vinaifanya documents isiwe sahihi mbele ya wachambuzi. (Nirekebishe kama nitakua nimekosea) Josee hata alipokua ujanani TZ pia alikuwa anajulikana kwa jina la Josee , tofauti na pdf ilivyoainisha. Pili Josee amechukua mafunzo ya jeshi nchini TZ ktk jeshi letu la jwtz kama sikosei ni kule mbeya. Sasa ukiunganisha hizo doti na jinsi mwandishi alivyoandika historia yake inaonekana ni uongo hata kama alikua anaelezea ukweli.

Mkama sema wewe bwana, yaani kuna mengi sana ya kuungaunga katika hiyo document yanayoraise more questions than answering.
 
Baada ya A level, alikwenda JKT Makutupola (Operation vyama vingi) 1992/93
Hili pia si jambo kubwa kuwa mentioned kwenye history yake? am also doubtful with the ka PDF
 
PDF kama hizo zipo nyingi sana mtandaoni. Hiyo ni kazi wanayoifanya wapinzani wa Kabila junior, na ni yaleyale ya kifo cha mfa maji. Hakuna zaidi.:yuck:
 
PDF kama hizo zipo nyingi sana mtandaoni. Hiyo ni kazi wanayoifanya wapinzani wa Kabila junior, na ni yaleyale ya kifo cha mfa maji. Hakuna zaidi.:yuck:

Mkuu uko shallow mambo haya ni zaidi ujuavyo.....subiri baada ya uchaguzi wa rwanda utaona nini kitafuata.
 
OK, vizuri. Your humility is charming and shows a backhanded intelligence that was much veiled in your original post. If indeed it is humility and eminence I am seeing.

Let me break it down for you.

Nilichosema ni kwamba, kuna uvumi usio msingi kwamba kuna Watutsi wanataka kutawala Afrika mashariki na kati, uvumi huu ndiyo msingi wa "Hima Empire theory" ambayo inasema Kagame na Museveni ndio viongozi walio implement hii plan, na hata katika serikali ya Tanzania kuna Watutsi wanaotaka kutekeleza hii plan.Nimesema huu ni uvumi usio msingi, kama uvumi uliopelekea kuuawa kwa wayahudi kwa kutumia kijitabu cha uongo cha "The Protocols of The Elders of Zion" ambacho Hitler alikitumia kama propaganda ya chuki dhidi ya Wayahudi kabla ya kuwaua.

Nilichosema ni kwamba, tuyachambue mambo kiundani ili tusirudie makosa waliyoyafanya Wajerumani ya kukubali propaganda za kisiasa bila kuzichambua.

In fact, nilichosema ni quite the opposite ya wanachoelewa watu wengine.Wengine - kama wewe- wanaelewa kwamba nimesema kuna Watutsi katika serikali ya Tanzania wanaotaka kuichukua serikali. mimi nimesema kuna uvumi usio msingi, unaoendana na Hima Emipre theory na "The Protocols of The Elders of Zion" ili kuwafanya Watutsi waonekana wana empire ambitions.

Sasa mtu ukiwa huelkewi Hima Empire ni nini, kwa nini nimeita Hima Empire theory kama uvumi, kwa nini nimetoa hiyo link ya Allafrica.com inayomquote Museveni aki dismiss Hima Empire rumors, ukiwa hujui "The Protocols of The Elders of Zion" ni nini na ilichangiaje kuuawa kwa Wayahudi, ukiwa huelewi role ya propaganda katika mauaji ya halaiki ya Rwanda, unaweza kusoma kisentensi kimoja, kuki misinterpret, na kuona tofauti na kilichosemwa.

Sikatai kwamba hiki kijibooklet kinaweza kuwa na ukweli, lakini aliyekiandika inabidi atuletee a more concrete case than this hodgepodge of incredible propaganda.

Nilivyokuwa sekondari, years ago, nilikuwa mpenzi wa vitabu vya James Hadley Chase. Kuna kimoja kinaitwa "Believe this, you will believe anything"

It is inevitable that part of this document carries some truth.Mtu hawezi kuandika out and out falsehoods like that. Lakini pia hii ni document ya kisiasa, wapinzani wa Kabila wa kisiasa wameiandika, kwa hiyo inabidi tujue ukweli uko wapi na propaganda zilizo subject to interpretation ziko wapi na uongo uko wapi.

Kwa wale wanaotaka kulimeza pdf lote kama gospel truth, nawaambia kama alivyosema Chase.

Believe this, you will believe anything.
You couldn't have put it better.
Tafadhari waelimishe maana ni wengi sana wenye imani za conspiracy theories za hima tutsi empire. Unakuta mtu amesoma lakini anaishi kama mshirikina, mpiga ramli kwa kuamini kitu cha kufikirika..kwa kweli wajinga ni wengi hii nchi. Wana makaratasi kwamba ni degree lakini upstairs hakuna kitu..msomi yeyoye lazima ufanye jitihada za kujua mazingira yanayokuzunguka.
 
You couldn't have put it better.
Tafadhari waelimishe maana ni wengi sana wenye imani za conspiracy theories za hima tutsi empire. Unakuta mtu amesoma lakini anaishi kama mshirikina, mpiga ramli kwa kuamini kitu cha kufikirika..kwa kweli wajinga ni wengi hii nchi. Wana makaratasi kwamba ni degree lakini upstairs hakuna kitu..msomi yeyoye lazima ufanye jitihada za kujua mazingira yanayokuzunguka.

Mkuu secret societies DO EXIST..usikatae, na habari zake si rahisi kuzipata ktk public domain ndio maana zinaitwa secret societies, ni exclusive kwa watu au makundi fulani tu. Ni vema kuwa open-minded badala ya kuwa media junky wa Corporate Media.
 
Mkuu secret societies DO EXIST..usikatae, na habari zake si rahisi kuzipata ktk public domain ndio maana zinaitwa secret societies, ni exclusive kwa watu au makundi fulani tu. Ni vema kuwa open-minded badala ya kuwa media junky wa Corporate Media.

Tatizo si kwamba tunakataa secret societies hazipo, tatizo kiPDF hakijatoa a coherent and informed case.
 
Tatizo si kwamba tunakataa secret societies hazipo, tatizo kiPDF hakijatoa a coherent and informed case.
Mi nadhani sio lazima sana hiyo doc iwe inakava 'kila kitu'..Kitu muhimu ni kuangalia ishu yenyewe inayoongelewa kama ni kweli tunaweza kufix mambo fulanifulani kuwa ni facts na zipi sio facts, hata kwa kutumia sources nyingine.
 
huyu bWana alisoma Zanaki (A level), nadhani kwenye late 80s na early 90s, nakumbuka kipindi hicho ndio alikuwa Mwanafunzi mvulana pekee katiaka shule ya Wanawake (ZANAKI), (maana alikuwa sponsored na GOV)


salalee,khaaa
 
Kati ya anayekubali kila kitu anachoona kwenye pdf kama ukweli, na anayeuliza maswali yanayojibu maswali yatakayoulizwa kuhusu hayo maswali nani ana papara?

Umeona humility yangu hapo juu? Umeona doubt yangu hapo juu? Umeona uncertainty yangu hapo juu? Umeona probing yangu hapo juu?

Mbona wewe unakuwa arrogant sana? Mbona wewe unakuwa sure sana? Mbona wewe unakuwa certain sana? Mbona wewe unakuwa trusting sana?

Hebu Juxtapose the two, halafu fikiri tena.

Sijasema kwamba Kabila malaika. Ninasema muandishi wa hiki ki booklet inabidi afanye kazi ya ziada kunifanya nimuamini, ama sivyo nitaona na yeye anatumia Machiavellian propaganda tu.

I agree with Kiranga, this is a pure conspirancy theory. There can be truth in it OR no truth in it since hakuna kinachoshindikana under this sun
 
Siasa ni kitu cha ajabu kabisa ninachoona katika hiyo ripoti ni namna jinsi watu walivyulitumia suala la uzawa kama ajenda ya kupakana matope. Ikumbukwe hata Salim alikwishakumbana na kadhia hiyo mwaka 2005 alipotaka kugombea urais Tanzania. Leo tuna nini? Kama sio Mabua.
 
Back
Top Bottom