Do we really need TAKUKURU?

Wanajamvi tujadili kama Great Thinkers hapa: issue sio kuwepo au kutokuwepo kwa TAKUKURU, issue ni kwamba TAASISI iliyopo haina Uhuru na haina Meno kupambana na Rushwa. na hata tukisema tuivunje, huyo atakayepewa jukumu hilo naye hatuna Guarantee kuwa atakuwa na Uhuru na Meno(Nguvu) kiasi gani cha kupambana na Rushwa. Mfano, nilisikia ktk Sera ya CHADEMA katika hili ni kwamba wao watakiingia madarakani watakachofanya ni kuipa uhuru na meno TAKUKURU wafanye kazi yao bila kuingiliwa na mtu yeyote, hii ni nzuri kwa maoni yangu mm. Lakini kwa jinsi mfumo/sheria iliyoiunda TAKUKURU hivi sasa, ambapo Mkurugenzi wake Mkuu anateuliwa na Rais, tunategemea nini???, hakuna Uhuru wa Meno hapo!!!!. NASHAURI: Watanzania sasa tudai Katiba mpya ili vyombo vya kisheria/vya Dola kama TAKUKURU, TISS, POLICE,JWTZ etc viwe huru visiingiliwe na wanasiasa kama ilivyo sasa, majirani zetu Kenya wameweza na sasa wanafurahia mabaliko ya Katiba yao. TUACHE KULALAMIKA
 
A CCM CRAP! haina tija kwa taifa letu ifutweeee. Kiundwe chombo huru na si hiki cha uteuzi wa RAIS
 
Kama Polisi na Mahakama zitatekeleza majukumu yake ipasavyo htatutakuwa na haja ya TAKUKURU
 
Kuvunjwa tu kwa takukuru haitoshi, wapewe haki yao, wanastahili adhabu nzuri tu. Maada mwanzoni uingereza waliiamini takukuru na walipokuwa wakimpatia bw hosea taarifa na mipango ya kuwanasa akina chenge, hosea anamtonya chenge. Hawa takukuru tunaihitaji lakini sio hii ya sasa.
 
Kwani taasisi kuwepo muda mrefu ndio kuwa na ufanisi?

i'm a believer of experience.....ila kwenye topic hii nilikuwa namaanisha kuwa kama haikuhitajika muda wote huu, basi labda sio muhimu kiivyo...na inaweza kufuta na kutengenezwa nyingine nzuri zaidi...yenye "ufanisi" zaidi.....dah, mpaka naanza kusound kama CCM, kasi zaidi, ari zaidi....anyways!
 
Back
Top Bottom