Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Nimepata taarifa kwamba huko Kyela baada ya ndg Mwanjala kutangaza kugombea ubunge akipambana na Dkt Mwakyembe, hali si shwari kwa upande wa Kambi ya Dkt Mwakyembe hasa kwa upande wa vijana mbalimbali wanapotoa kauli mbalimbali kumponda! Wengi wao wanadai kwamba kinachotakiwa kudumu ni CCM na sio mtu! Pia baadhi yao wanadai kuwa walimpenda Dkt Mwakyembe, lakini wanampenda Mwanjala zaidi, kwa kuwa hawajaona matunda yoyote ya ubunge wake Kyela! Baadhi wanadai eti kwenye nafasi ya ukatibu wa Mbunge kwenye Ofisi yake amemweka mtu aliyepata Division ZERO kidato cha IV ambaye ni ndugu Emanuel ambaye hana msaada mkubwa wa kutekeleza majukumu yake! Dkt Mwakyembe inasemekana alipata pigo jingine hivi karibuni baada ya mtu wake wa karibu, aliyekuwa M/kiti wa Halmashauri ndg Kisugujila kuvuliwa madaraka na kwa bahati mbaya timu hiyo hiyo ya madiwani iliyovua madaraka M/kiti wa Halmashauri ikiongozwa na Chris, Diwani wa Ipinda na Majuni, Diwani wa Kajunjumele, iko kinyume kabisa na Dkt Mwakyembe! Pia wenyeviti wengi wa kata wako kinyume na mheshimiwa huyu! Badala ya kupanga mikakati Dkt Mwakyembe amesikika akilalamika kwamba "Mafisadi wamemwaga fedha" jimboni kwake ili kutaka kumng'oa, tuhuma ambazo hajazithibitisha! Mh Dkt Mwakyembe, hali si shwari Jimboni kwako na kama ulidai endapo "Mafisadi" wakitaka kukung'oa Kyela basi wakaweke kambi na wake zao miaka 5 ndipo watakapokung'oa sidhani kama hiyo kauli unaweza kuitoa kwa sasa hali ilivyo! Wenye updates zaidi toka Kyela watupatie, pls!