kinepi_nepi
JF-Expert Member
- Aug 16, 2007
- 869
- 235
Dk Slaa: Wana CCM niungeni mkono nimng'oe Kikwete Send to a friend Tuesday, 27 July 2010 22:50 0diggsdigg
Dk Slaa
Mussa Juma, Karatu
MGOMBEA urais wa Chadema Dk Wilbroad Slaa, amezidi kupandisha joto la kisiasa nchini, baada ya jana kuomba nguvu za wana CCM wazalendo ili amng'oe Rais Jakaya Kikwete, hapo Oktoba.Ombi hilo la kuomba nguvu kutoka miongoni mwa wana CCM, limekuja kipindi ambacho chama hicho kikongwe barani Afrika, kikiwa kimepigwa na mawimbi mazito ya kisiasa, baada ya kuibuka makundi miongoni mwa vigogo wake.
Akihutubia mamia ya wapigakura wake katika jimbo la Karatu ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru, Dk Slaa aliomba nguvu hizo akirejea mafanikio yake bungeni akisema, :"Yalikuwa ni mafanikio kwa maslahi ya taifa zima si Chadema."
Kumbukumbu za bunge zitamuonyesha Dk Slaa kama mbunge aliyeibua kashfa nzito, ikiwemo wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), ufisadi wa Meremeta na Tangold na Deep Green Finance.
Kashfa nyingine kubwa ambazo aliziibua na kushikia bango ni pamoja na Kampuni ya Tanpower Resources, iliyowahi kuuziwa mgodi nyeti wa makaa ya mawe Kiwira.
Tanpower Resources imekuwa ikitajwa kuihusisha familia mbili za Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa na waziri wake wa Nishati Daniel Yona.
Hata hivyo, katika kashfa hizo kubwa za kitaifa zinazohusu upotevu wa takriban sh 1trilioni, ni EPA tu ndiyo iliyochunguzwa na watuhumiwa akiwemo mfanyabiashara maarufu Jeetu Patel, kufikishwa mahakamani.
Dk Slaa mgombea ambaye ameweza kufanyakazi hizo na nyingine kuibua ufisadi wa kitaifa, alirejea mafanikio hayo akisema ni faida kwa taifa zima hadi kwa wana CCM si upinzani pekee.
Alifafanua kwamba, kwa taifa lilipofikia hivi sasa linahitaji mtu atakayeweza kufanya maamuzi magumu ili kuondoa hali ya kulindana.
Mbunge huyo wa Karatu anayemaliza muda wake, alisema anaamini yeye anaweza kushughulikia matatizo makubwa ya taifa hili.
Kwa mujibu wa Dk Slaa, tatizo la kulinda watuhumiwa wa ufisadi linatokana na kuwepo uongozi usio makini.
Aliongeza kwamba, mafanikio ya uongozi wake yatakuwa ni kwa taifa zima hivyo akasisitiza, wana CCM wazalendo wanapaswa kumuunga mkono.
Mwanasiasa huyo ambaye pia ameweza kuteka hisia za watu wa kada tofauti wakiwemo wasomi, alisema huu ni wakati wa kufanya mabadiliko.
Katika siku ya pili ya mikutano yake ya kuaga wapigakura wake wa Karatu, Dk Slaa amekuwa akipaa kwa helikopta tarafa kwa tarafa.
Ndani ya helikopta hiyo wamo pia mwenyekiti Freeman Mbowe na Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) Profesa Mwesiga Paregu.
Kwa upande wake Profesa Baregu, alisema Dk Slaa hajapotea kugombea urais na kusisitiza, ni mtu mwenye uwezo mkubwa.
Wakati huo huo, Mkurugenzi wa masuala ya bunge wa chadema, John Mrema, alieleza chama hicho kimejipanga kuhakikisha kinavunja rekodi ya watanzaniua ambao watamdhamini Dk Slaa kuwania urai
Mussa Juma, Karatu
MGOMBEA urais wa Chadema Dk Wilbroad Slaa, amezidi kupandisha joto la kisiasa nchini, baada ya jana kuomba nguvu za wana CCM wazalendo ili amng'oe Rais Jakaya Kikwete, hapo Oktoba.Ombi hilo la kuomba nguvu kutoka miongoni mwa wana CCM, limekuja kipindi ambacho chama hicho kikongwe barani Afrika, kikiwa kimepigwa na mawimbi mazito ya kisiasa, baada ya kuibuka makundi miongoni mwa vigogo wake.
Akihutubia mamia ya wapigakura wake katika jimbo la Karatu ikiwa ni sehemu ya kuwashukuru, Dk Slaa aliomba nguvu hizo akirejea mafanikio yake bungeni akisema, :"Yalikuwa ni mafanikio kwa maslahi ya taifa zima si Chadema."
Kumbukumbu za bunge zitamuonyesha Dk Slaa kama mbunge aliyeibua kashfa nzito, ikiwemo wizi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya Benki Kuu (BoT), ufisadi wa Meremeta na Tangold na Deep Green Finance.
Kashfa nyingine kubwa ambazo aliziibua na kushikia bango ni pamoja na Kampuni ya Tanpower Resources, iliyowahi kuuziwa mgodi nyeti wa makaa ya mawe Kiwira.
Tanpower Resources imekuwa ikitajwa kuihusisha familia mbili za Rais mstaafu wa awamu ya tatu Benjamin Mkapa na waziri wake wa Nishati Daniel Yona.
Hata hivyo, katika kashfa hizo kubwa za kitaifa zinazohusu upotevu wa takriban sh 1trilioni, ni EPA tu ndiyo iliyochunguzwa na watuhumiwa akiwemo mfanyabiashara maarufu Jeetu Patel, kufikishwa mahakamani.
Dk Slaa mgombea ambaye ameweza kufanyakazi hizo na nyingine kuibua ufisadi wa kitaifa, alirejea mafanikio hayo akisema ni faida kwa taifa zima hadi kwa wana CCM si upinzani pekee.
Alifafanua kwamba, kwa taifa lilipofikia hivi sasa linahitaji mtu atakayeweza kufanya maamuzi magumu ili kuondoa hali ya kulindana.
Mbunge huyo wa Karatu anayemaliza muda wake, alisema anaamini yeye anaweza kushughulikia matatizo makubwa ya taifa hili.
Kwa mujibu wa Dk Slaa, tatizo la kulinda watuhumiwa wa ufisadi linatokana na kuwepo uongozi usio makini.
Aliongeza kwamba, mafanikio ya uongozi wake yatakuwa ni kwa taifa zima hivyo akasisitiza, wana CCM wazalendo wanapaswa kumuunga mkono.
Mwanasiasa huyo ambaye pia ameweza kuteka hisia za watu wa kada tofauti wakiwemo wasomi, alisema huu ni wakati wa kufanya mabadiliko.
Katika siku ya pili ya mikutano yake ya kuaga wapigakura wake wa Karatu, Dk Slaa amekuwa akipaa kwa helikopta tarafa kwa tarafa.
Ndani ya helikopta hiyo wamo pia mwenyekiti Freeman Mbowe na Mjumbe wa Kamati Kuu (CC) Profesa Mwesiga Paregu.
Kwa upande wake Profesa Baregu, alisema Dk Slaa hajapotea kugombea urais na kusisitiza, ni mtu mwenye uwezo mkubwa.
Wakati huo huo, Mkurugenzi wa masuala ya bunge wa chadema, John Mrema, alieleza chama hicho kimejipanga kuhakikisha kinavunja rekodi ya watanzaniua ambao watamdhamini Dk Slaa kuwania urai