Gobret
JF-Expert Member
- Jun 11, 2010
- 320
- 88
Nimeamua kutumia maneno hayo kwa sababu nina shindwa kupata neno la kutumia badala yake. Si kawaida kuona watu wa namna hii. Mtu huyu si mbinafsi na amejitoa kwa maslahi ya watu wake. Watu wa Karatu ninawaheshimu sana kwa kumleta na kumruhusu agombee urais wa Tz kwa ridhaa yenu. Watu wa Karatu walikuwa na hofu kuwa kugombea kwake urais wao watapoteza mtu makini lkn kwa sasa wameelewa kuwa si kupoteza bali kupata. Wengi hatumwelewi vizuri Dk Slaa kwa sababu tu tuna desturi ya kuongozwa na CCM. Mwl Nyerere kama mtakumbuka alishasema CCM si mama yake na muda wowote atatoka akitaka. Wengine wana nena kuwa ni mkristu tena mkatoliki. Huu ni upuuzi mtupu. Wengine wamefika mbali kwa kusema ni padri aliyeasi hivyo hafai kuwa kiongozi. Kweli hafai kuwa kiongozi? Kuwa kiongozi tunapima nini? Uaminifu, uzalendo wake na uwezo wake. Hatuongozwi na chama, ukabila, udini wetu bali watu walio na maadili ya uongozi. Watu wenye maadili ya uongozi sasa hawapo CCM, wapo nje ya CCM. Ona wanavyofanya kwenye kura za maoni, hizo ni kufuru. Ni kweli kwamba tunawashabikia watu wa namna hii. Ndio maana wanatukana wanavyopenda hadharani.............sitaki kura zenu........acheni kazi...........Mungu akupe nini sisi binadamu na hali hatuna umaskini wa mawazo. Inatosha sasa. Vijana, wazee, wababa na wamama wakati ni wetu kuionyesha CCM kuwa imetosha, na enzi na nyakati zao zimepita. Tuanza na tumalize na Dk Slaa. God bless DK SLAA.