Dk slaa kwa hili tusidangnyane (nyani haoni kundule)

DK SLAA ASEMA "Pinda, kwa siku moja akiwa kule bungeni hupata posho ya Sh200,000 ambayo inazidi mshahara wa mwezi mmoja wa mwalimu, hata polisi anayelinda usalama wenu,
Dk Slaa aliyekuwa mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka jana alisema, inasikitisha kuona Mbunge wa Katavi anakuwa mbinafsi kwa kujiwekea umeme wa jua kwenye nyumba yake pekee katika Kijiji cha Usevya badala ya kuupeleka kwa wananchi wote.
source mwananchi.

lakini huyuhuyu dk slaa anayesema pinda hupata posho ya sh 200,000 kwa siku mbona yeye hajapinga chama chake kumlipa marupurupu na mshahara anaolipwa mbunge ambao yy mwenyewe alisema ni milioni 7. kwa ufupi dk ni muongeaji mzuri na mhamasishaji mzuri wa wananchi lkn katika vitendo ni ZIRO kabisa, yy kila siku hulia kuwa posho wanazolipwa wabunge ni kubwa leo posho anayolipwa waziri mkuu ni kubwa sasa mbona yy haonyeshi mfano kwa kukataa marupurupu ambayo chadema wameamua kumlipa, aseme tu msinilipe hizi hela ni bora tuwasomeshee yatima ktk majibo yetu, tena kwa hivyo itakuwa kakisaidia sana chadema.

Tofautisha basi,mshahara na marupurupu.M7 za Dr slaa ni mshahara,200,000 ya pinda ni marupurupu,kwa siku.Piga hesabu zako pinda anapata Marupurupu sh ngapi kwa mwezi? + mshahara.Marupurupu tu ya pinda yanazidi mshahara wa DR Slaa.Sasa kwanini point ya DR isiwe na mashiko.
 
Tayari we ni mbwa ndo maana unashika unapoambiwa kamata ...kaanze na pindua aliyetoa mfano wa kutotaka ku2mia VX ili hali amelipaki pembeni linamsubiri ....Dont u think ua a big DOG! halafu kuthibitisha wewe ndo hushirikishi akili yako ni kwamba kama ugonjwa nilionao hauna tiba niende kwa Babu Loliondo ...huoni kama ni TIBA? bado kweli huoni kundule wewe...

siwezi kushindana na mtu ambaye alizaliwa nyumba ya wageni. na siku zote ni kujisumbua kushindana na mtu asiyemjua mama ake. lakini hongera nasikia dk SLAA mekuruhusu kuwa mwanawe wa kufikia.
 
Hawa CDM ni wazushi, Mwenyewe Mbowe kama kiongozi wa upinzani mbona hajalikataa shangingi analolitumia la serikali?? Wakati huo huo hatujasikia pesa za ruzuku zimepelekwa matawini ili kuimarisha chama badala yake wanatumbua kupitia "MRADI WA MAANDAMANO ENDELEVU" tena maandamano yanafanyika kipindi cha kilimo. ACHENI KUDHOOFISHA KILIMO KWANZA!!!!!

Kipindi cha kilimo? Ulisikia wakulima wakilamikia kupotezewa mda wao au unawasemea?
 
Hii hoja haina mshiko wowote. Kwamba dr Slaa anakubali mshahara kutoka chama chake, nadhani hiyo ni haki yake kama mtendaji wa chama. Wewe ulitaka atumikie CHADEMA kwa kujitolea?

Swala hapa ni kwamba Pinda na mafisadi katika serikali wanatafuna fedha ya uuma ambayo inatokana na kodi ya wananchi whereas CHADEMA kama chama kinamlipa katiba mkuu wake kutokana na kasma wanayopata toka kwa wanachama, wahisani na pia ruzuku ya serikali. Fedha ya CHADEMA haipo kwa ajili ya kutatulia matatizo ya wananchi kwa sababu CHADEMA haina serikali.

Hawa akina Pinda wanafanya matumizi mabaya ya fedha ya umma ambayo inatakiwa kutumika kuwahudumia wananchi katika kugharimia shughuli za maendeleo. Hiyo gari ya milioni 500 ni anasa zisizo za msingi wowote ule.Huo ni ulimbukeni ambao ndio sera mojawapo ya Chacha Cha Magamba.
 
Kaka usiongee usichokijua , maandamano ya CDM hayana posho either kwa Dr slaa, mbowe pamoja na wabunge na wafuasi wa chadema.
Kila mmoja huwa tunatumia pesa zetu mfukoni kwa chakula , malazi, na pia watu wenye kipato kikubwa kwenye chama kama wabunge huwa wanachangia shilling laki tatu na nusu kwa mwezi ili chama kiweze kujiendesha kwa kulipia vyumba vya ofisi Tanzania nzima.

Maandamano ya CDM siyo semina elekezi za magamba ambazo kila mtu analipwa , for your information ni katibu mkuu tu kwa sasa anayelipwa mshahara katika top management ya CDM wengine ambao ni wabunge hawana wanafanya kazi za kujitolea za chama.

Kumbuka ruzuku ya chadema bado ni ndogo haiwezi kukidhi mahitaji ya chama tanzania nzima.

Chiefmasanja, Asante kwa majibu mazuri.
Naomba uiandike tena hii taarifa ieleweke vizuri. Inatutia simanzi wale tunaopenda mabadiliko na ukiweza kuiweka vizuri zaidi kwa mifano ya wazi wazi inaweza kutuhamasisha wengine japo si wanachama wa CDM mkaona tukajitolea kutoa michango yetu kwa kazi nzuri mnayoifanya mpaka sasa. Kwa mfano wapeni wananchi matumizi mnayotumia jumla kwa kila mwezi au kwenye maandamano muhimu kama ya juzi Mbeya, mkionyesha ni ngapi zimechangiwa na viongozi wenyewe. Ruzuku ionekane imepelea kiasi gani. Sisi tunaoipenda nchi yetu, bila kujali tunatoka chama gani tutawaongezea nguvu. Msidhani hatupo wananchi tunaoweza kujitolea kama mfanyavyo ninyi. Mtakuwa mnakosea kujipunguzia nguvu. Kuna wengine nyadhifa zao haziruhusu sana kujikita kwenye siasa lakini wajibu wao kama raia wanaujua.

Elimu ya Uraia mnayotoa haswa kwa vijana wa Tanzania na watu wa miji midogo na vijijini ni muhimu kuliko hata kushinda uchaguzi na kuingia Ikulu kwa kipindi kimoja katika taifa letu.

Moja wapo ya mapungufu muhimu sana ambayo watu hufanya wanapokuwa katika harakati ya kufanya mambo mema ni pale wanaposahau au shindwa kuandika ripoti "to document" kuelezea kilichofanyika, jinsi au mbinu zilizotumika, waliohusika na jumla ya matumizi ikiwezekana na mchanganuo wake uwepo). Na mwisho tulichojifunza "lessons learned".

Sina maana kuwa nina wasiwasi ya kwamba hilo halifanyiki Chadema, lakini unapotoa majibu mazuri haya hapo juu ukiongezea takwimu kidogo utafanya watu wa aina yangu kufikiria la kufanya ili kuwawezesha zaidi.

Yule ambaye hajawahi kufanya la kujitolea hata mara moja katika maisha yake hawezi kukuelewa. Lakini msichoke kuendelea kuelimisha.

Nawatakieni kazi njema, Mungu ibariki Tanzania na watu wake wote Wapagani, Waislamu na Wakristo kwa ujumla wao.
 
Huyo kanyasu ndio Kanichefua kabisa? anaposema Chadema wana mambo ya Kike anamaanisha nini? kama ni mwanaume basi hajui maana ya watu wanaitwa wanawake. Hamna ushujaa wa mwanamke alioufanya kama kukubali kulala na mwanaume na kukuzaa wewe, tena kwa kubeba mimba miezi tisa na kuzaa kwa uchungu, iwe hospitali kubwa kama Agha Khan ama kule kijijini nyamilama wanakozaliwa kwa kumulika kwa kiberiti ama kiberiti. Tuache maneno ya kibaguzi ambayo hayasaidii kuijenga nchi.
Hoja ilikuwa nyepesi kwamba Slaa aakisi kile anachosema. Wenye busara wameeleza tofauti ya sera ya kitaifa na mambo madogo madogo. Na hoja ya msingi kwa Slaa ni kuwa kama kiongozi unaanza na watu wako, yeya ameanza kujiwekea miradi yake ya binafsi ya ufugaji nyuki na samaki. Manake nini kama kiongozi anayechukizwa angeanzisha miradi kwa wajili ya kukombo jamii inayomzunguka,manake ndio kupambana na umaskini wa watu. Kwa hiyo hoja ya Slaa haikuwa a petty issue ni mfano mdogo uliobeba ujumbe mzito
 
YouTube - why sell shares and not this?

Mbona hata mbunge mmoja hajaongelea swala hili la posho?....hata CDM arusha walichukua posho halafu wakaondoka,wabunge hapa tuliwauliza juu ya posho zao wakasema ni siri kubwa! Vipi kuhusu ilani yenu ya uchaguzi?
Badala yake mnataka kuuza shares za NBC na Airtel kwa mafisadi!
 
mpendatz
ulichoongea ndicho wengi watz tunakosa. Tunabishana kuhusu watu badala ya issue zitakatotuota kuwa taifa maskini sana duniani, kama Dr. Bilal na Prof. Tibaijuka walivyothibitisha kwa kushiriki mkutano huko intambul, na kama mwenyewe mzee kikwete alivyotuambia juzi kuwa hawako mkutanoni, ila watawabakizia makabrasha. tutakufa lakini Tz itabaki miaka mingi ijayo. Tafakari
 
huyu si alijifanya kukataa gari jipya? then waandishi wa habari wakaiandika hii taarrifa? au ni kujin'garisha kwa wanatanganyika

Jibuni hoja kwanza. Huyu Dr. Slaa amekuwa akipiga kelele nje wakati jua likizama wanajilipa posho kama vile yeye ni mbunge na wakati hahudhurii kikao hata kimoja. Kwa nini asingesema kwamba anacholipwa ambacho ni mishahara ya walimu zaidi ya 30 kitumike katika kusaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu na hatarishi? Unafiki mtupu
 
Hafikii hata chembe ya ufisadi wa bilionea Riz One! hatudanganyiki. Dr Slaa PhD tunaomba maandamano nchi nzima....nchi inakoelekea ni kubaya.

Madness at its best. Tuambiwe gharama za maandamano na athari zake kwa hazina yetu!
 
Yani wabongo mnachekesha kweli, mtu unajadili maandamano lakini hapohapo huoni semina elekezi zinavyotafuna pesa za nchi yetu. Kazi ya siasa ni pamoja na maandamano na mikutano sasa inapofanyika mnasema ufisadi, nyie mtafunguka akili lini? Hata vijana walio vijiweni ambao hawana hata access ya mtandao wameerevuka kuliko nyie wapambe wa ccm.
 
Haya ! endeleeni na fikira zenu mgando, niwaulize ninyi mlio kinyume na Cdm, hivi mnafikiri serikali ikishindwa kutimiza majukumu kwa wanainch wake nani atakaye nyoshewa kidole ? jibu liko wazi ni ccm ndo itakayo nyoshewa vidole

Kuna sababu gani kujiwekea posho kubwa kwa wabunge kiasi kikubwa hicho, huku unaendelea kuwa ombaomaba au kukopa, mimi nilitegemea chama kilichoko madarakani ndo kingekuwa ngangari kusimamia mabo kama hayo.

kwa mwendo huo 2015 out !
 
Walewale..............uwa bado mnaendelea kupambana na watanzania? Maana kutaka hawa jamaa waendelee kutuibia ni kuwa unakubaliana na uwizi wao...Nimekuwa nikisema hapa JF mara kwa mara..Pinda ni mtoto wa mkulima aliyetusaliti watoto wa wakulima.........Mimi uwa namuita mtoto wa mkulima asiye mkulima.that is to say..kazaliwa na mkulima lakini ameukana ukulima wake kwa vitendo vyake visivyoshabiliana na falsafa yake...
 
Hivi umekosa hoja, masaa matatu yanaweza kudhofisha Kilimo Kwanza, please contact me ni kuelimishe wimbo huo unaoitwa kilimo kwanza , ndipo utakapotambua kuwa ccm inacheza tu, hakuna maendeleo ya kilimo kupitia kilimo kwanza huo ni wimbo kama nyimbo zingine
 
Sichangii thread za ...cdm/dr/zitto/mbowe...kwa ili tusichanganyane au ...mfano: Utasikia ..zito kwa ili umetudanyanya... Thread za muundo huu ni umbeya mtupu!
 
Hivi ni kweli wabunge wetu kupewa fedha ya gari milion 90m/= badala ya 45m/= kutokana na budget iliyoidhinshwa?

Nikweli dr slaa kuwa unachukua 12m/= kwa mwezi?

Dr slaa hebu sasa weka mpira chini watu wafanye kazi yaani madiwani wetu wa cdm na wabunge , kwani ukiendelea kupiga kelele itageuka mazoea.

Hebu sasa toeni japo hesabu ya matumizi ya cdm kupitia ruzuku watu tuone tofauti yako dr slaa na makamba (mjeshi) ndani ya vyama.
 
DK SLAA ASEMA "Pinda, kwa siku moja akiwa kule bungeni hupata posho ya Sh200,000 ambayo inazidi mshahara wa mwezi mmoja wa mwalimu, hata polisi anayelinda usalama wenu,
Dk Slaa aliyekuwa mgombea urais katika Uchaguzi Mkuu Oktoba mwaka jana alisema, inasikitisha kuona Mbunge wa Katavi anakuwa mbinafsi kwa kujiwekea umeme wa jua kwenye nyumba yake pekee katika Kijiji cha Usevya badala ya kuupeleka kwa wananchi wote.
source mwananchi.

lakini huyuhuyu dk slaa anayesema pinda hupata posho ya sh 200,000 kwa siku mbona yeye hajapinga chama chake kumlipa marupurupu na mshahara anaolipwa mbunge ambao yy mwenyewe alisema ni milioni 7. kwa ufupi dk ni muongeaji mzuri na mhamasishaji mzuri wa wananchi lkn katika vitendo ni ZIRO kabisa, yy kila siku hulia kuwa posho wanazolipwa wabunge ni kubwa leo posho anayolipwa waziri mkuu ni kubwa sasa mbona yy haonyeshi mfano kwa kukataa marupurupu ambayo chadema wameamua kumlipa, aseme tu msinilipe hizi hela ni bora tuwasomeshee yatima ktk majibo yetu, tena kwa hivyo itakuwa kakisaidia sana chadema.

HAPO KACHEMKA MBONA HASEMEI KIASI GANI WAZIRI MKUU KIVULI WA UPINZANI ANAPATA KAMA POSHO BUNGENI? NA MASLAHI YAKE KAMA GARI, OFISI NA KURUGENZI, DEREVA NA FEDHA ANAZOPATA KWA UENDESHAJI WA OFISI YAKE KWA MWEZI?

AMA ASEME YEYE ALIPOKUWA MWENYEKITI WA KAMATI YA LAC ALIKUWA ANAPEWA NGAPI? NA KWA SASA WAKINA ZITO-POC MREMA -LAC, CHEYO-PAC nk.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom