BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,005
| ||
|
| ||
|
DR. Slaa tunataka maandamano ya kuwashinikiza hawa magamba bila maandamno hawatawajibika, na safari hii yawe ya nchi nzima...
EEE,..MUNGU TUNAKUOMBA 2015 IWE KESHO ILI TUWEZE KUISAMBARATISHA HII SERIKALI YA MAJAMBAZI sote tuseme aaaamen.
Aaaamen !
Maandamano pliiiiizDR. Slaa tunataka maandamano ya kuwashinikiza hawa magamba bila maandamno hawatawajibika, na safari hii yawe ya nchi nzima...
Dk. Slaa: Baraza la Mawaziri livunjwe
Amshangaa Rais Kikwete kuendelea na ziara nje
na Waandishi wetu, Dodoma na Dar
Tanzania Daima
CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimelitaka Baraza lote la Mawaziri la Rais Jakaya Kikwete, kujiuzulu kwa madai kuwa limeshindwa kuona dharura ya tatizo la umeme nchini na kulitafutia ufumbuzi.
Pia chama hicho kimemtaka Rais Kikwete kujiuzulu nafasi yake kwa kudharau na kuendelea na ziara yake nchini Afrika ya Kusini wakati akijua fika kwamba Bunge limekwamisha bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo, anakabiliwa na tuhuma za ufisadi.
Pasco said:...Rais Jakaya Kikwete, ameuzungumzia mgao wa umeme unaendelea sasa nchini kote, amesisitiza "tatizo ni ukame".
Rais Kikwete alikuwa akizungumza kwenye mahojiano maalum na BBC akiwa nchini Afrika Kusini yaliyorushwa jioni hii na BBC Swahili.
Rais amesisitiza, kwa vile mitambo yetu mingi inategemea nguvu za maji, hivyo tatizo la umeme limesababishwa na ukame.
Mwandishi akahoji kuwa tangu 2006 mgawo ulipoanza, bado tuu mlikuwa mkitegemea mvua?.
Rais alijibu kuwa baada ya 2006 hatua mbalimbali zimechukuliwa kuzalisha umeme kwa njia za gesi, makaa ya mawe hata umeme wa nguvu za upepo, lakini miradi hii yote inahitaji muda muafaka wa kuagiza mashine, akasisitiza ununuzi ewa mitambo unachukua muda, "huwezi kununua mitambo ya umeme hivi hivi tuu kama unavyoingia dukani kununua koti lako, mitambo huagizwa kwa kupeleka order kiwandani utengenezewe. hata hii mitambo inayoingizwa nchini hivi sasa, iliaagizwa toka mwaka jana.
Rias Kikwete amewataka wanasiasa wasibeze juhudi za serikali kuwaletea umeme wa uhakika Watanzania.
Pia Rais Kikwete, ameuhakikishia tena ulimwengu kupitia BBC kuwa serikali yake ni sikivu, kama kuna watyu wenye hoja za msingi kuhusu utatuzi wa tatizo la umeme, wasiishie tuu kulalamika, bali waje na hoja za jinsi ya kutatua tatizo hili na serikali yake itazipokea hoja hizo na kuzifanyia kazi.