Dk. Slaa amlipua Lukuvi; Awarushia pia kombora Chami, Simbachawene

Sasa naamini kuwa chadema wanatumiwa na mapacha watatu kwani hii staili yao ya kutwanga kotekote imelenga kuwaokoa mapacha watatu.Kwanini wameanza kipindi hiki wakati walikuwa wanayajua yote hayo? Halafu wanakazana kuwashambulia kina Sitta na wengine wanaopambana na mafisadi ndo kabisa wanaonyesha kuwa wanatumiwa.Kwa staili hii vita dhidi ya ufisadi itakuwa ngumu sana na nchi itaendelea kuliwa na wenye pesa.

Kama hata chadema imenunuliwa basi watz mjue kuwa ukombozi wetu uko mbali sana! Nyie hamjiulizi kwanini hata gazeti la Mbowe la


Tanzania daima nalo linatumiwa na Rostamu? Amkeni jamani na msifikiri chadema kuwa ni chama makini bali ni wanafiki tu!

Ingawa inaonekana unataka kupindisha point ya muhimu inayojadiliwa katika uzi huu, binafsi ningependa CCM waamini kuwa Chadema wanawatetea mapacha watatu na kwa kuwa huwa wanafanya vitu kuwapinga chadema hapa watalazimika kuwawajibisha hao mapacha watatu ili mradi tu waonekane kuwa wanapambana na chadema na sie waDanganyika kufaidika kwa kuwajibishwa kwa hao mafisadi. Ila pia ninachoshangaa ni kuwa CCM ndo wana mamlaka ya kuwawajibisha hao, kwa nini hawafanyi hivyo?
 
Surely we don't have officials but predators who just use their influence kujigawia na sio vipaji vya ujasiriamali!

Hili ndo suala kubwa zaidi, una miliki bilion za fedha, halafu unazungumzia biashara kiurahisi rahisi
eti hata jamaa zangu wanafanya hivyo? mambo ya kimjini mjini hayo!
 
Chami, Lukuvi wamshukia Dkt. Slaa


Na Mwandishi Wetu

Gazeti la majira; Mei 20, 2011

WAZIRI wa Viwanda na Biashara, Dkt. Chyril Chami na mwenzake wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Uratibu na Bunge) Bw. William Lukuvi wamemshukia Katibu
Mkuu wa CHADEMA, Dkt. Willibrod Slaa na kusema kuwa anachanganya maana ya neno 'ufisadi', badala ya kulipua wenzake, anajilipua mwenyewe.

Mawaziri hao walitoa kauli hizo jana kwa nyakati tofauti walipozungumza na gazeti hili kufuatia madai ya Dkt. Slaa kwamba viongozi hao na wanasiasa wengine wanafanya ufisadi kujigawia vitalu vya kuvuna magogo katika msitu wa Sao Hill, Mafinga mkoani Iringa.

Akizungumzia madai hayo, Dkt. Chami alisema tatizo la Dkt. Slaa ni kushindwa kuelewa ukweli katika suala la vibali vya uvunaji magogo hayo na kuchanganya maana ya neno 'ufisadi'.

"Vibali vya kuvuna magogo kwenye msitu huo sio kitu cha siri, ni jambo la wazi, kila mwananchi anaruhusiwa kuomba, wanaokubaliwa majina yao yanabandikwa ubaoni ni mamia ya watu. Hapa Dkt. Slaa anakosea, anashindwa kuelewa maana ya neno ufisadi na kupotosha umma," alisema Dkt. Chami.

Alifafanua kuwa vitalu vya msitu wa Sao Hill ni mali ya serikali na havimilikiwi na mtu yeyote bali umekuwepo utaratibu wa kuvuna mbao kila mwaka ambao hauna tenda na wananchi kwa maelfu wamekuwa wakiomba na kupata vibali hivyo.

" Maelfu ya wavunaji huomba na kupata vibali vya kuvuna magogo kwa utaratibu wa kuandika barua, ni lazima uandike barua kila mwaka kuomba na kulipia kibali hicho. "

"Dkt. Slaa hawezi kuthibitisha kuwa nimejimilikisha kitalu kwasababu hakuna mtu mwenye uwezo wa kujimilikisha msitu wa serikali,"alisema Dkt. Chami na kuongeza kuwa aliomba kibali hiyo kwa nia njema ya kupata mbao za kusaidia ujenzi wa shule mbalimbali jimboni kwake.

Kwa upande wake Bw. Lukuvi alisema mbali ya mawazo yake kuwalipua mawaziri hao, Dkt. Slaa amejilipua mwenyewe kwani ameropoka jambo asilo na ushahidi wake.

Alisisitiza kuwa msitu huo ni mali ya serikali na hakuna yeyote mwenye uwezo wa kumiliki eneo ndani ya msitu huo.

"Dkt. Slaa asome hata vitabu vya sheria, msitu huu ni mali ya serikali, hakuna aliyemilikishwa. Uvunaji wake umewekwa kwenye utaratibu wa wazi kwa kila mtu, hapa ufisadi haupo!" alisema Bw. Lukuvi.

Akaongeza "Niliomba kibali ili nipate mbao za kwenda kuezeka shule ya Idodi iliyoungua kwenye jimbo langu, nilifanya hivyo kupunguza gharama za bidhaa hiyo, nikapata kibali nikavuna mbao za kutosha kama 1,000 nilipomaliza kazi hiyo sikuomba tena kibali kiliisha siku ilele. Anachozungumza Dkt. Slaa ni mambo ya mwaka juzi na hayana ufisadi wowote.

" Fedha nilizolipa kwa Idara ya Misitu kama ushuru na kodi ya kupasua mbao hizo ni 2, 835,330/- Mimi natoa ushauri wa bure kwa Dkt. Slaa asiwe mzee wa mipasho na milipuko. Katika hili, amejilipua mwenyewe baada ya kukubali kupokea maneno na kuropoka bila utafiti, aige mfano wa mbayuwayu" alisema Bw. Lukuvi na kuleza kwamba anamfahamu na kumheshimu Dkt. Slaa kutokana na huduma mbalimbali za shirika la CCBRT mkoani Iringa lakini kwa hili ameteleza
 
Ninawapongeza waheshimiwa kwa kukiri ukweli, ni wachache sana wanaoweza kuwa na ujasiri kama wenu, watu kama kina RZ1, Mh.Hussein Mwinyi na JK wao wamekwanusha wakati DR.SLAA anatabia ya kupata kwanza nondo husika then ndo anatoa statement. Mawaziri wetu wamekiri kuwa walipewa vibali hiyo tu imenifurahisha na wamedhihirisha jinsi walivyosomA KWA UHAKIKA NA KUELEWA SHULE. DR.Chami nimekukubali kwa ujasiri huo.

Kifuatacho baada ya kukiri:
Ni vema sheria ikaangaliwa kama upatikanaji wa vibali kwa waheshimiwa haukuwa na mgongano wa kimaslahi, je walifanya ku-declare interest kabla ya kupewa vibali?????. Kama walifanya hicho basi tutawasamehe, lakini kinyume na hapo itabidi watuombe RUNGU LIWASHUKIE kwa kutumia madaraka yao vibaya.
 
Ninawapongeza waheshimiwa kwa kukiri ukweli, ni wachache sana wanaoweza kuwa na ujasiri kama wenu, watu kama kina RZ1, Mh.Hussein Mwinyi na JK wao wamekwanusha wakati DR.SLAA anatabia ya kupata kwanza nondo husika then ndo anatoa statement. Mawaziri wetu wamekiri kuwa walipewa vibali hiyo tu imenifurahisha na wamedhihirisha jinsi walivyosomA KWA UHAKIKA NA KUELEWA SHULE. DR.Chami nimekukubali kwa ujasiri huo.

Kifuatacho baada ya kukiri:
Ni vema sheria ikaangaliwa kama upatikanaji wa vibali kwa waheshimiwa haukuwa na mgongano wa kimaslahi, je walifanya ku-declare interest kabla ya kupewa vibali?????. Kama walifanya hicho basi tutawasamehe, lakini kinyume na hapo itabidi watuombe RUNGU LIWASHUKIE kwa kutumia madaraka yao vibaya.

Wewe unaugua ugonjwa wa kupenda! Hao jamaa wanamlaumu Slaa kwa kurupuka wewe unampongeza kwa kuwa anapata "nondo!" Nilidhani ungesema labla kwa hili Slaa hakupata hizo nondo kabla ya kuropoka ningekuelewa!
 
Huyu Dr Chami si Mchagga?Sasa mbona anamshambulia Dr Slaa wakati NAPE anasema CHADEMA ni mali ya Wachagga? Mimi siwaelewi hawa CCM kabisa
 
Lukuvi ni fisadi na wenzio ,serikali nzima imeoza kabisa.........................................
 
Wewe unaugua ugonjwa wa kupenda! Hao jamaa wanamlaumu Slaa kwa kurupuka wewe unampongeza kwa kuwa anapata "nondo!" Nilidhani ungesema labla kwa hili Slaa hakupata hizo nondo kabla ya kuropoka ningekuelewa!

Tunachoongelea hapa ni Je, WALIPEWA MAENEO???? NA KAMA WALIPEWA WALIPEWA PASIPO MAZINGIRA YA MGONGANO WA KIMASLAHI KUTOKEA?? THEN HATUA.PERIOD
 
Doctor Slaa hajakosea hata kidogo, kumbuka hawa mawaziri ni wakubwa wa serikali na wanamamlaka ya kupata chochote kwa nguvu zao, sasa huwezi kuwashindanisha na wananchi wa kawaida hata kidogo, unadhani huyo mtoa vibali hajipendi ikiwa atawanyima hawa mawaziri na kuwapa wananchi wa kawaida? Mantiki hapa siyo haki ya kila mwananchi bali ni jinsi hawa wakubwa wa chama na serikali wanavyoweza kutumia madaraka waliyonayo kujinufaisha wenyewe na maslahi yao, huo nao ni ufisadi pai.
 
Watu tujadili Hoja kwa hoja tusiwe Mavuvuzela, Lukuvi ni mwanasiasa, kitendo cha kuhusisha shule iliyopata maafa na Ufisadi wake hii si sawa kabisa. Je yeye Lukuvi ni Mkandarasi?

Je baada ya kupata kitalu cha Mbao aliuzia mbao zote kwa shule hiyo? Au nyingine aliuza mwenyewe? Je hiyo shule kwa kupata hicho kitalu cha miti ilifaidika vipi na Mbao hizo?

Wizara ya elimu ilijua Lukuvi alitoa mchango wake kwa kuwa alikuwa na kitalu cha uvunaji?
LUKUVI IS ANOTHER CROOK, KUFA KUFAANA.

Naona yote haya kuna harufu ya kujitajirisha kwa mgongo wa maafa na siasa. Jamani wanasiasa kweli mnavuna na kula bila kunawa!! Lukuvi utetezi wako ni just bla bla
 
Hao Mawaziri hawaruhusiwi kuwa na kazi kama hizi na tena kwenye Mashamba ya SERIKALI wakati wao ndiyo Maboss wa SERIKALI.

Hapo hakuna ushindani ila kutumia MABAVU.

Wajiondowe haraka sana.
 
CHAMI NA LUKUVI wasiwafanye wananchi wajinga. Ni mzee Juma akiomba kibali na hao kina CHAMI nao wakiomba kibali cha msitu huo huo ni nani atapewa? Hao watoa vibali wakiona barau za akina CHAMI na LUKUVI hata barua ya Mzee Juma hatasomwa tena. Hivyo mzee Juma ataambulia patupu tu.

Nyerere alisema viongozi wa kisiasa wasimiliki mali lakini viongozi wa CCM kwa uroho wao wakabatilisha kule Zanzibar. Matokeo yake ndio hayo ya vibali vya misitu.
 
Watu tujadili Hoja kwa hoja tusiwe Mavuvuzela!! Lukuvi ni mwanasiasa, Kitendo cha kuhusisha shule iliyopata maafa na Ufisadi wake hii si sawa kabisa!! Je yeye Lukuvi ni Mkandarasi? Je baada ya kupata kitalu cha Mbao aliuzia mbao zote kwa shule hiyo? au nyingine aliuza mwenyewe? Je hiyo shule kwa kupata hicho kitatu cha miti ilifaidika vipi na Mbao hizo? Wizara ya elimu ilijua Lukuvi alitoa mchango wake kwa kuwa alikuwa na kitalu cha uvunaji?
LUKUVI IS ANOTHER CROOK!! KUFA KUFAANA!! Naona yote haya kuna harufu ya kujitajirisha kwa mgongo wa maafa na siasa. Jamani wanasiasa kweli mnavuna na kula bila kunawa!! Lukuvi utetezi wako ni just bla bla

Kwanza Lukuvi katoa data ambazo hazina mahusiano na madai yake mwenyewe .Katoa tarehe za shule kuungua za uongo na jinsi alivyo omba kibali cha mbao . Now angalia hili . Slaa yeye kafumua kuwaamsha watanzania wala hahitaji ushahidi mwingi kihivyo alichosema kina ukweli now endeleeni kufuatilia utajua mengi zaidi .
 
Jamani,

Issue iko wazi na clear, waheshimiwa wamekiri waliomba vibali kwa ajili ya Idodi sec school iliyoungua, huyo ni Lukuvi.

Chami yeye anasema aliomba kibali sijui akezeke nini sijui, mnataka ushahidi gani tena. Alichokisema Dr Slaa ndo hicho walichokiri hawa waheshimiwa.

Mnataka waseme mpaka tani walizovuna, na mabillioni waliyopata? Hapa ni kama alivyosema yeye mwenyewe Lukuvi, kwamba ametuambia na tumechanganya na za kwetu" jibu ndo hilo.

Safi mawaziri wetu mmeonyesha matunda ya semina elekezi. Mmejibu mapigo kwa kukiri tuhuma zenu.

Haya kamati ya maadili mnasubiri ushahidi gani tena.
 
ina maana awajaelewa tu kwamba wao ni mawarizi na wao kuomba hivyo vibali maombi yao kukataliwa ni ngumu kutokana mfumo wetu maana hao watoa vibali ni watumishi wa chini sana kwao,
bila shaka hata hizo barua za maombi wanaandika hao hao wanaotoa vibali mimi nimewai kushuhudi ya namna hiyo, kumuomba mkubwa akutumie barua kila mwaka ni kama kuchoka kazi. wauzi mafratic watakueleza simamisha daladala ya mkubwa hata kwa bahati mbaya wewe wanakutupa mtwara tena polisi wa kawaida
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom