Dk. Slaa Ajibu Mapigo ya CCM

mwissho wa ubaya aibu, imefika wakati lazima ccm wajue kuwa mwisho wao umefika, kwani hakuna mwanzo uso na mwisho, kazeni kamba cdm bado kidogo tu watangoka, tayari washaregea wanaanza kupayuka na kuongea mambo ambayo hayapo. big up sanaaaaa.
 
narudia tenna kusema, slaa dr slaaaaaaaaaa hawez kukamatwaaaaa na siroakali hiiiii ya kifisadi.

laslaa faya kazi yako ya kuamsha watznznania kwwnye usingizi wa pono.

nasema tena akunan qwa kumkataw slaa dr wilbroads pita

s*e*z type
 
Mh. Raisi,

Salaam.

Nasikitika sana ukikosea na wengine wote wanakosea. Siamini wanakosea kwa bahati mbaya ila ni kwa sababu umewasabisha wakosee.

Umeongelea maandamano ya Chadema kwenye hotuba yako. Wengine wamekurupuka wanazungumza pia. Wanalaani.

Kama umeshasema nilitegemea kitu cha kufuata ni utekelezaji wa amri yako (najua hukutoa) au maagizo yako. Sasa wote mnatoa kauli, mnatuchosha kutuambia ambayo sisi tunayajua.

Ni nani amekwambia kuna mtu anapenda kutembea juani kilomita 10? Je Mh. Raisi unafikiri watu wanapenda kutumia mafuta yao ya pikipiki na kuacha vibarua vyao watembee tu barabarani?

Mnawaita wazururaji, je umesikia Bank au mwajiri yeyote amelalamika mfanyakazi ameacha desk akaenda kwenye maandamano? Hujiulizi kwanini wanazurura?

Mheshimiwa Raisi, na hao waliofeli kidato cha nne kwa maelfu wataacha kuzurura? Au unafikiri wameenda wapi baada ya kufeli? Yakitokea maandamano wakae nyumbani kisa amani na utulivu?

Mnatoa kauli za kejeli badala ya kujibu hoja na kuongoza nchi. Waziri Mkuu anapotoa kauli 'hao chadema wenyewe waoga wakipigwa mabomu wanakimbia' anaitakia hii nchi amani? Kuanzia sasa polisi wakipiga mabomu hatutakimbia, tutajibu kwa mabomu ya petroli si ndicho anachotaka?

Anayechochea hapa ni nani? Anayekejeli wananchi wakikimbia au anayekimbia? Kwa sababu anataka watu wasikimbie basi asubiri aone. Wapige tena mabomu.

Mh. Raisi, umezungukwa na watu wasiofikiri wala hawana msaada kwako. Mbona hawakuongea kabla hujaongea wewe? Wassira, Vuai nk walikuwa wapi? Tendwa alikuwa hajui kuhusu hili mpaka sasa? Acheni kutuona wajinga. Mkituheshimu tutawaheshimu.

Mnataka kusujudiwa na kuogopwa. Hapana. Nchi ina matatizo na matatizo ni yaliyopo sasa hivi sio historia ya 'oooh tumeitoa nchi mbali'. Mbali wapi?

Mheshimiwa Raisi, hao wakina Wassira, Tendwa na Jumuiya ya Wazazi nk ni wanafiki na hawana maana. Hawakwambii ukweli na ukikosea wanazidi kukupoteza.

Mh. Raisi, waandamanaji ni wananchi. Ni watanzania. Wanaipenda amani yao. Wao ndio sababu ya amani na utulivu. Sio ccm wala chadema.

Wananchi ndio wanailinda amani hiyo. Sio ccm wala chadema.

Wanapokimbia ili amani na utulivu viendelee Waziri Mkuu anawaita waoga. Take it from me, hawatakimbia tena halafu tuone.

Mh. Raisi, tafadhali waongoze viongozi wako. Wafundishe adabu na heshima kwa wananchi wa taifa hili. Dharau na kejeli zao zitaleta majuto.

Mh. Raisi, jitahidi kutatua kero za wananchi. Yote yanayozungumzwa yapo. Ndio maana wananchi wanaandamana. Hawalazimishwi kushiriki. Ni shida zao ndio zinawafanya waamue kueleza kilicho moyoni mwao.

Mh. Raisi, nashindwa kukuelewa. Wananchi wanakwambia hatuna kazi, maisha magumu, tunafeli mitihani, nchi yetu inaibiwa nk wewe unasema wanatishia amani!! Kweli umeshindwa kuona kwamba kinachotishia amani ni hizo sababu na sio wananchi wala chadema?

Mh. Raisi, narudia kusema, wanaoandamana ni wananchi. Sio chadema. Wengi wa waandamanaji hao walikupigia kura 2005 na 2010. Tafadhali wewe na viongozi wako msiwadharau.

Kama waliwachagua wakiwa wanazurura basi msiwatupe baada ya kuwachagua kisa eti ni wazururaji.

Chadema ni waandaaji. Washiriki ni wananchi, watanzania.

Huna wa kukwambia, ukikosea wewe wamekosea wote. Hilo ni tatizo.
 
Nyie bwana kwa mikwara, Slaa akikamatwa mtabaki mnaongea kwenye keyboard tu siku tatu nne na baada ya hapo mtasahau wala hamtaifanya kitu chochote serikali.

Wakoloni wa ccm hawaogopi kumtia slaa kolokoloni kwa sababu za wananchi waoga kama sie, wao wanachoogopa ni kupoteza reputation yao na madili yao kimataifa.
Slaa akiingia kwenye 18 zao ambayo ktk darubaini ya kimataifa itaonekana OK , na watamtia na uhakika hamtafanya lolotee wapiga mluzi.
 
Mafisadi wa EPA, Rada, Kagoda, Ndege ya Rais, helicopters za jeshi, Meremeta, Richmond/Dowans, mikataba feki ya madini, Wezi wa Kiwira Coal Mining wote hawa wameshindwa kuwakamata! ila sasa hivi wanataka kuwakamata watetezi wa maslahi ya Tanzania na Watanzania!
 
Mbona Pro. Lipumba walishawahi kumuweka Ukonga kinachowashinda nini kwa Dr. Slaa na Mbowe! Tena basi sheria inamruhusu rais kumuweka mtu yoyote kizuizini kwa muda anaoutaka, mbona hatumii fursa hii kwa makosa ya wazi ambayo ni uchochezi, uhaini n.k
CCM wanajua kabisa wanachokifanya akina Dr. Slaa na wenzake ni haki yao lakini indirect ni kama kuwaambia wapunguze. Serikali ikishindwa nguvu ya dola itatumika, huu ni uoga wa maamuzi.
 
Akamatwe kwa kosa lipi? labda la kupoka mke wa mtu? na hilo kisha lipanguwa kwa kulipa ugoni!
 
moto wa mageuzi umeshawaka hakuna anayeweza kuuzima olewake atakaejaribu kuuzima atajuta kwanini alizaliwa dk kaza buti vijana tuko pamoja Mungu ibariki Tanzania Mungu ibariki Chadema
 
Naunga mkono mkuu, CCM walishazoa vyama dhaifu vinaonekana vinauhai wakati wa uchaguzi tu ,sasa CDM na stratagy ya hakunakulala ni kuchapa kazi katika kuonyesha madudu ya serikali na uwajibikaji sasa ccm wanaogopa kwani huu moto wa chadema ni mkali sana, na kwakuwa ccm wameishiwa hoja ya kuuzima wanasingizia amani na wanajenga mazingira ya kibabe kutaka kukidhibiti na jinsi tunavyokwenda huko mbele dola itangilia kati na kudhofisha CDM.

Ushauri.
Chadema lazima wajipange kubadilisha mbinu za upambanaji kadri mazingira yatakavyoruhusu mfano kumobulize watu wafungue matawi kakatika kila wilaya na na kuwalika vionguzi wa juu kuja kuyafungua, pia kuwatumiwa vingoozi wa wilaya katika kuanzisha matawi na kuwa karibu na wanachama wa eneo lao.
Pia kufanya uchunguzi na kuwachukulia hatua mara ikibainika kuwapo kwa mamluki na wasaliti ndani ya chama , jua hali hii imejitokeza sana kipindi cha uchaguzi na ikiachiwa itastawi na kuwa tatizo

Nadhani watakuwa wameupata ushauri huu... na waufanyie kazi>>>Kwani, wanawindwa sana!!!
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Wilbroad Slaa amejibu mapigo ya Chama cha Mapinduzi(CCM) na kusema kuwa Chama chake hakitasitisha maandamano yanayoendelea katika mikoa mbalimbali nchini na kwamba yupo tayari kwa lolote.

........

Kwa msisitizo akasema kuwa yeye na Mwenyekiti wake Freeman Mbowe wako tayari kwa lolote hata kama ni kukamatwa kwa ajili ya kutetea maslahi ya Watanzania.

.......

Hata hivyo, Dk. Slaa alisema CCM ndio inasababisha vitendo vya uvunjifu wa amani nchini kutokana na Serikali yake kutowajali wananchi maskini, hivyo lawama hizo hazipaswi kwenda kwa viongozi wa Chadema waliojitolea kufa kwa ajili kupiga kelele kwa kukataa ukandamizwaji huo.

"Mimi sina hofu na kauli wanazozitoa CCM, waache wapige kelele kwani inaonyesha ni jinsi gani serikali ilivyoshindwa kuongoza na sasa wanahitaji huruma za wananchi ambao kwa miaka mingi wamenyimwa haki zao," alisema Dk. Slaa.

Aliendelea kusema "Nchi ni sawa na tunda la amani, lilokuwa juu ya mti unaoitwa haki, nashangaa sana CCM inavyopaza sauti juu ya amani pekee ikiwa inakakataa kutoa haki, tunachohitaji ni haki ifanyike."

Hata hivyo, alisema kabla ya kwenda kushtaki kwa wananchi kwa njia ya maandamano katika mikoa mbalimbali, walitumia wabunge kuilalamikia Serikali ndani ya Bunge juu ya malipo ya Dowans, Kagoda na Meremeta, lakini serikali ilikataa kutoa majibu. Alisema, kama Serikali inaona maandamano wanayoyafanya yanavunja sheria ya nchi hakuna haja ya kukiadhibu Chadema, bali yeye na Mwenyekiti wake Mbowe wakamatwe.

Alimtaka Kapteni Chiligati kujifunza sheria na kusoma Katiba ya nchi kwanza kabla ya kuanza kutoa vitisho ambavyo vinaweza kuipeleka nchi katika sehemu mbaya.

"Naomba waache kukiadhibu chama, naomba wanitafute mimi na Mbowe watukamate tupo tayari kukamatwa kwa ajili ya kutetea wananchi, kinyume cha hapo moto huu hautazimika hadi kieleweke," aliongeza kusema.


Full Story: Home

SOURCE: NIPASHE, Jumapili, 06th March 2011.

Ndiyo maneno tunayopaswa kuyasikia kutoka kwa makamanda. Aluta continuuuuuuaaaaaa!!
 
Nyie bwana kwa mikwara, Slaa akikamatwa mtabaki mnaongea kwenye keyboard tu siku tatu nne na baada ya hapo mtasahau wala hamtaifanya kitu chochote serikali.

Wakoloni wa ccm hawaogopi kumtia slaa kolokoloni kwa sababu za wananchi waoga kama sie, wao wanachoogopa ni kupoteza reputation yao na madili yao kimataifa.
Slaa akiingia kwenye 18 zao ambayo ktk darubaini ya kimataifa itaonekana OK , na watamtia na uhakika hamtafanya lolotee wapiga mluzi.

Endelea kuwaza kama mlevi wa mataputapu! Unadhani dunia ya jana ndiyo ya leo. Wamkamate Dr. Sla waone cha moto. Unadhani kwa nini hawamkamati pamoja na kuwalipua mara kwa mara?? Miaka mitano yote ya uongozi wa serikali yako ya kifisadi mmekuwa mkishughulikia kashfa nzito anazolipua Dr. Slaa. Mtake msitake Dr. Slaa hawezi kukamatwa kipuuzipuuzi tu. Sahauni kabisa!!
 
Sasa mimi nashindwa kuelewa, Azimio la Arusha tuliandamana sana tu. Halafu CCM ni chama chama cha kudumu, inakuwaje sasa tuaogopa CDM. Maadui wa CCM wamo ndani, wafukuzeni muone kama watu hawakuandamana nchi nzima kuwaunga mkono. Ngoja niwape kidogo List.
RS
EL
AK
MK
AC
SS

sasa kuangaika na chadema, mnapoteza muda, hatutaki watu watakaotokea nsituni, heri hawa wanaosema tu. Chonde chonde safisheni nyumba ndani. Wakafanye biashara hawa.:hand:

mbona unaandika kwa woga...si uweke majina kamili. RS ndo nani?
 
Chadema wa Jf mtachoga saaaaana. Lakini nchi itaongozwa na wengine. Si slaa wala Mbowe. Kelele zote hizi ni kwa vile walikosa kura. Kaza buti wana Jf kwa kupiga debe humu ukichanganya na kelele za slaa mtakuwa matajiri wote. Bravo kwa matusi wanachadema humu jf na Slaa kwenye maandamano. Keep it up mwisho wa siku wananchi watawaelewa na kufanya maamuzi. Kwa sisi ambao tayari tunaona majibu yenu humu jf hayana tofauti na mikutano ya Chadema(kwa matusi) ni dalili tosha kabisa kuwa Milembe inawasubiri.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom