Buchanan
JF-Expert Member
- May 19, 2009
- 13,199
- 1,969
Joseph Lyimo, Simanjiro
MGOMBEA wa urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa kuwa gumzo kwa wakazi wa Mkoa wa Manyara imezidi kuwapa maumivu makali viongozi wa CCM mkoani humo na kusababisha kufanya vikao vya ndani hadi saa 7:00 usiku.
Viongozi hao wa CCM Mkoa wa Manyara wakiongozwa na katibu wake, Avelin Mushi, Katibu wa Wazazi Mkoa, George Kijaji, Katibu wa UWT Mkoa,Grace Maholelo na wabunge wateule wa viti maalumu mkoa huo, Dorah Mushi na Martha Umbulla na mgombea ubunge katika Jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wanakutana muda huo, kujadili hilo ni jinsi gani watakabiliana na Chadema.
Wengine wanaokutana katika mkutano huo ni kamati ya siasa ya Wilaya ya Simanjiro,wagombea udiwani wa CCM na wajumbe wa Halmashauri ya CCM katika Kata ya Mererani.
Katika vikao hivyo vilivyofanyika juzi kuanzia saa 11:00 jioni hadi saa 7:00 usiku kwenye ukumbi wa Manyara Inn uliopo mji mdogo wa Mererani wilayani Simanjiro, pia ulihudhuriwa na mkuu wa wilaya hiyo Khalid Mandia ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM wilayani humo.
Mmoja kati ya wajumbe wa vikao hivyo ambaye hakupenda kutaja jina lake kwa vile siyo msemaji wa chama hicho, alisema kuwa upepo wa kisiasa siyo mzuri mkoani Manyara kwa CCM, hivyo uongozi wa mkoa huo umejadili hilo ili kunusuru hali hiyo.
Alisema nyota ya kisiasa mkoani Manyara kwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Slaa ipo juu, hivyo wanapanga mikakati mbalimbali ya kukinusuru chama hicho.
Alidai kuwa kuna baadhi ya wanachama wa CCM mkoani humo walipandikizwa mbegu chafu kwamba wawachague diwani na mbunge wa CCM, lakini kura ya urais wampe Dk Slaa, hivyo kutokana na hilo uongozi wa mkoa unafanya vikao hivyo, ili kunusuru hali hiyo.
Katibu wa CCM mkoani Manyara, Avelin Mushi alisema kura za wakazi wa mkoa huo, hazitatosha kumfanya Dk Slaa kuwa rais wa Tanzania kwani wananchi wengi wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete.
"Nimekutana na kamati ya siasa ya wilaya,wagombea udiwani na wajumbe wa Halmashauri ya CCM Kata ya Mererani ili kujadili na kupanga mikakati ya ushindi kwenye uchaguzi mkuu," alisema Mushi.
Katibu huyo aliwaasa wakazi wa mkoa huo kutopoteza kura zao kwa kutambua mazuri yaliyofanywa na chama hicho kwa kumpa kura nyingi za ndiyo mgombea urais wa CCM.
Japokuwa CCM mkoani Manyara imefanikiwa kumpitisha Ole Sendeka bila kupingwa kwenye ubunge Simanjiro na madiwani 24, wamepita bila kupingwa,bado inawakati mgumu kwenye majimbo mengine matano, kwa kuwa mapokezi ya mgombea urais wa chama hicho, hayakuwa mazuri na kwamba alizomewa alipokuwa akijinadi wilayani Mbulu.
Source: MWANANCHI.
MGOMBEA wa urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk Willibrod Slaa kuwa gumzo kwa wakazi wa Mkoa wa Manyara imezidi kuwapa maumivu makali viongozi wa CCM mkoani humo na kusababisha kufanya vikao vya ndani hadi saa 7:00 usiku.
Viongozi hao wa CCM Mkoa wa Manyara wakiongozwa na katibu wake, Avelin Mushi, Katibu wa Wazazi Mkoa, George Kijaji, Katibu wa UWT Mkoa,Grace Maholelo na wabunge wateule wa viti maalumu mkoa huo, Dorah Mushi na Martha Umbulla na mgombea ubunge katika Jimbo la Simanjiro, Christopher Ole Sendeka wanakutana muda huo, kujadili hilo ni jinsi gani watakabiliana na Chadema.
Wengine wanaokutana katika mkutano huo ni kamati ya siasa ya Wilaya ya Simanjiro,wagombea udiwani wa CCM na wajumbe wa Halmashauri ya CCM katika Kata ya Mererani.
Katika vikao hivyo vilivyofanyika juzi kuanzia saa 11:00 jioni hadi saa 7:00 usiku kwenye ukumbi wa Manyara Inn uliopo mji mdogo wa Mererani wilayani Simanjiro, pia ulihudhuriwa na mkuu wa wilaya hiyo Khalid Mandia ambaye ni Mjumbe wa Kamati ya Siasa ya CCM wilayani humo.
Mmoja kati ya wajumbe wa vikao hivyo ambaye hakupenda kutaja jina lake kwa vile siyo msemaji wa chama hicho, alisema kuwa upepo wa kisiasa siyo mzuri mkoani Manyara kwa CCM, hivyo uongozi wa mkoa huo umejadili hilo ili kunusuru hali hiyo.
Alisema nyota ya kisiasa mkoani Manyara kwa mgombea urais kwa tiketi ya Chadema, Dk Slaa ipo juu, hivyo wanapanga mikakati mbalimbali ya kukinusuru chama hicho.
Alidai kuwa kuna baadhi ya wanachama wa CCM mkoani humo walipandikizwa mbegu chafu kwamba wawachague diwani na mbunge wa CCM, lakini kura ya urais wampe Dk Slaa, hivyo kutokana na hilo uongozi wa mkoa unafanya vikao hivyo, ili kunusuru hali hiyo.
Katibu wa CCM mkoani Manyara, Avelin Mushi alisema kura za wakazi wa mkoa huo, hazitatosha kumfanya Dk Slaa kuwa rais wa Tanzania kwani wananchi wengi wana imani kubwa na Rais Jakaya Kikwete.
"Nimekutana na kamati ya siasa ya wilaya,wagombea udiwani na wajumbe wa Halmashauri ya CCM Kata ya Mererani ili kujadili na kupanga mikakati ya ushindi kwenye uchaguzi mkuu," alisema Mushi.
Katibu huyo aliwaasa wakazi wa mkoa huo kutopoteza kura zao kwa kutambua mazuri yaliyofanywa na chama hicho kwa kumpa kura nyingi za ndiyo mgombea urais wa CCM.
Japokuwa CCM mkoani Manyara imefanikiwa kumpitisha Ole Sendeka bila kupingwa kwenye ubunge Simanjiro na madiwani 24, wamepita bila kupingwa,bado inawakati mgumu kwenye majimbo mengine matano, kwa kuwa mapokezi ya mgombea urais wa chama hicho, hayakuwa mazuri na kwamba alizomewa alipokuwa akijinadi wilayani Mbulu.
Source: MWANANCHI.