Dk. Nchimbi tulia! Mwosha huoshwa

Kwenye kundi la Nchimbi kuna Asha Kigoda ambaye kila Spika bila aibu anakazana kwa sauti kumwita Dr.Asha Kigoda .

Dr Aisha Kigoda hawezi kuwa kwenye kundi la Nchimbi kamwe. Aisha amesomea udaktari katika ngazi inayoitwa Assistant Medical Officer, ambao nchini Tanzania wanatambulika na pia wana leseni kutoka Baraza la Madaktari, na katika leseni zao hizo hutambuliwa na kuandikwa Dr (kabla ya jina la mhusika). Kwa hiyo Dr Aisha Kigoda "hajajiita" daktari, bali kapewa cheo hicho na Baraza la Madaktari baada ya kufikia kiwango ambacho Baraza hilo linakubali aitwe hivyo. Na wala hajafoji vyeti, maelezo yake anayotoa kwenye wasifu wake ndiyo elimu halisi aliyo nayo, na vyuo alivyosoma ni vya Tanzania na vinatambulika. Msimwonee dada wa watu.
 
Nikirudi kwa Nchimbi na UVCCM yake, je ana nafasi gani ya kuendelea kushinikiza mambo humo baada ya kuondoka kwenye uenyekiti? Labda bado anaogopa kuachia ngazi, kama alivyosema Tony Blair kuwa japo kuachia ngazi ni kuzuri kwa manufaa ya chama, ni uamuzi mgumu sana kwa anayeachia ngazi (hii aliisema alipokuwa anautema u-PM). Huyu Nchimbi asijidanganye kuwa akiweka mtu anayemtaka ati ataendelea kuongoza hiyo UVCCM kwa remote control. Kwani huyo mwenyekiti mpya akikataa kumsikiliza Nchimbi atamfanyaje (na wakati huo nadhani Nchimbi atapaswa awe ameondoka kwenye umoja huo maana si kijana tena!)

Ukisikia kutapatapa ndio huku, au labda ni kuchanganyikiwa kama teenagers wanavyopata ugumu kujua identity zao: Binti kashavunja ungo, lakini bado anataka kucheza "mdako" na vitoto, akiulizwa anasema yeye mtoto ni haki yake kucheza, lakini akikutwa anazoza "chemba" na "linjemba" akigombezwa analalamika kuwa ati yeye ni mtu mzima anaingiliwa uhuru wake! Nchimbi uwanja si wako tena huo, wapishe vijana wachukue nafasi yao. Kama unaishi kwa kutegemea mbinu chafu, au unatafuta watu wa kuunda nao ushirika wa kufanya nao mbiu chafu baadae, basi mie nakutahadharisha kuwa "USHIRIKA WA WANGA HAUDUMU!"
 
Mwandishi wa makala anatakiwa aandike makala nyingine tuone atakachoweza kuandika ! there is nothing new but anti-ccm with no concerns !

kila siku mmewakalia viongozi wa chama kimoja utadhani mbowe hayupo, mnyika hayupo ! sijawahi kuona hata siku moja skendo zao, au hao ni malaika ?

i'll be starting to raise concerns juu ya viongozi wa upinzani, iweje wao washindwe kuchunguzwa, regardless of their private life, or that of the government !
 
Mwandishi wa makala anatakiwa aandike makala nyingine tuone atakachoweza kuandika ! there is nothing new but anti-ccm with no concerns !

kila siku mmewakalia viongozi wa chama kimoja utadhani mbowe hayupo, mnyika hayupo ! sijawahi kuona hata siku moja skendo zao, au hao ni malaika ?

i'll be starting to raise concerns juu ya viongozi wa upinzani, iweje wao washindwe kuchunguzwa, regardless of their private life, or that of the government !


Wee kada,
Kila mtu anatetea kitumbua chake. Uliona wapi makala za gazeti la Uhuru zikiwalenga viongozi wa CCM kwa mabaya yao?
 
nishawahi kuona kwenye front page ya uhuru !

guess what ! am not shocked kuona hiyo habari kwenye gazeti la mbowe na nafikiri tushazoea ! wengine tusipoona habari zisizo na vichwa wala miguu ktk gazeti la mbowe, tunajiuliza leo vipi wameshiba nini ?
 
nishawahi kuona kwenye front page ya uhuru !

guess what ! am not shocked kuona hiyo habari kwenye gazeti la mbowe na nafikiri tushazoea ! wengine tusipoona habari zisizo na vichwa wala miguu ktk gazeti la mbowe, tunajiuliza leo vipi wameshiba nini ?

Kada,kidumu chama cha mapinduzi...ccm hoyeee...unaonaje badala ya kuwa-criticize hao wanaong'ang'ania kuandika habari ambazo ni anti-CCM,wewe kama kada ukachua jukumu la kuandika habari zilizo pro-CCM (kama zipo)....
 
^ there i guess you are trying to be sacarstic ! mm kuandika habari za pro ccm wont solve anything ! the message i was trying to put out here was and is so simple and clear, LETS STOP THAT BEHAVIOR ! period, and not otherwise !
 
^ there i guess you are trying to be sacarstic ! mm kuandika habari za pro ccm wont solve anything ! the message i was trying to put out here was and is so simple and clear, LETS STOP THAT BEHAVIOR ! period, and not otherwise !

wakale wapi?
 
gotcha ! kumbe wanafanya hivyo kwa ajili ya njaa zao, lakini na hiyo ruzuku inayowapendezesha inayotolewa na chama tawala hawashibi tu ?
Ruzuku inatolewa na chama tawala?Kada fikiri kabla ya kuandika.Kwanza nani kakwambia watu wanapendeza kwa ruzuku?Hayo mambo ya ulaji yako CCM na ndio maana hata ufisadi imekuwa kama Ibada kwao.
 
nilifikiria sana kabla ya kuandika ! off course na chama tawala = SERIKALI ILIYO CHINI YA CHAMA TAWALA ! au na serikali iliyo chini chini ya wapinzani ??
 
Nchimbi anataka kumpaya kiongozi ambaye atakuwa anawajibika kwake. Kwa maana nyingine anataka kuifanya Kin Maker wa vijana na baadaye kutumia remote kuwageuza anavyo taka kwa masalhi yake siku zijazo .Hili liko wazi na Nchimbi hawezi kutoa tamko kama hili labda yeye akiandikiwa akawa anasoma kwa mara ya kwanza bila ya kutafakari .

wafuatao ndo wanotarajiwa kugombea mpaka sasa taendelea kuwataarifu wanapokuja new comers.
1;VAILET MZINDAKAYA
2;BENO MALISA
3;HUSEN MOHAMED
4;JERRY SLAA
5;NAPE NAWIYE
6;ZAINAB KAWAWA
7;EDWIN SANDA
8;EDWIN MTAKA
Wana JF wenzangu hao ndio wanosemwa semwa kua wanataka kumrithi Dk Nchimbi
 
[QUOTE=KadaMpinzani;154369]nilifikiria sana kabla ya kuandika ! off course na chama tawala = SERIKALI ILIYO CHINI YA CHAMA TAWALA ! au na serikali iliyo chini chini ya wapinzani ??[/QUOTE]

ruzuku kamwe haikuwekwa kwa ajili ya wapinzani ...ipo kuwanufaisha ccm...ingalikuwa wapinzani mfano chadema wana wabunge say 120....yaani na wao wangekuwa wanapata bilioni kwa mwezi...ungeona ccm wangepeleka mswada bungeni kufuta ruzuku....jumla ya pesa wanayopata wapinzani kwa mwezi haifiki milioni 80...ccm wanapata zaidi ya bilioni moja kwa mwezi...sasa hapo nani ananenepa kwa ajili ya ruzuku...tuwe wakweli.....
 
Hii forum ina marafiki wa Nchimbi, ambao huenda mpaka jimboni kwake kumsaidia mbona wako kimyaa? Sasa urafiki gani huo, sisi wa kwetu huwa tunawasimamia nyinyi vipi? Au mlifikiri hatujui kuwa huwa mnaenda huko Songea na Nchimbi kinyemelea, halafu mnakuja kuwa Chadema hapa JF na kuulizia vyeti vyake?

Mpashe Mpashe vipi kaka? vipi ukijipasha sasa kwenye hii topic?, kweli mjanja hajinyoi, mlifikiri wote hapa forum tumelala ?
 
Hii forum ina marafiki wa Nchimbi, ambao huenda mpaka jimboni kwake kumsaidia mbona wako kimyaa? Sasa urafiki gani huo, sisi wa kwetu huwa tunawasimamia nyinyi vipi? Au mlifikiri hatujui kuwa huwa mnaenda huko Songea na Nchimbi kinyemelea, halafu mnakuja kuwa Chadema hapa JF na kuulizia vyeti vyake?

Mpashe Mpashe vipi kaka? vipi ukijipasha sasa kwenye hii topic?, kweli mjanja hajinyoi, mlifikiri wote hapa forum tumelala ?

Mkuu naona umewadhamiria hasa!
 
Kama mna uhakika wamefoji vyeti basi nendeni Mahakamani...JF si mahakama. Mtikila kwa muda amekuwa anasimama Mahakamani kupinga mambo mengi tu...mengine ameshinda na mengine kushindwa. Kama mmeshindwa basi Basi tumuombe Mtikila asimamie hilo!!! kinyume chake itakuwa kuwalaumu watu pasi na Hoja nzito.

Bado zipo Online degree nyingi tu na wengi wamekuwa wanafanikiwa. Leo TZ kipo Open University sijui wao graduate wao wanafanyaje. Nakumbuka Mzee Malecela nae alipewa Dr. wa Heshima na Open University hapa DSM..(kama nimekosea naomba mniweke sawa)

You missed even the glimpse of the Train.

We are not talking about Online universities, we are talking about fake Universities.
Ziko nyingi sana hizo, na mazuzu kama Nagu Nchimbi nk wanaona ni kivuno.

Check and differenciate between the two.

PhD za heshima anaweza pewa mtu ambaye hata kusoma hajui, sifa za kupewa PhD za heshima zipo na kila chuo kinautaratibu wake.
Pia wakati inatolewa Dunia nzima huambiwa ni PhD ya heshima.

PhD yeyoteile Duniani hutolewa kwa kupiga shule isiyo pungua 3 years kama wewe ni kipanga. Wapo wazee kibao hapo Tanzania wamepiga PhD zao miaka 7 mfululizo kwa sababu pengine Presentation zao zilikuwa hazikukubaliki au ugumu wa kuweka Thesis zao katika vitendo.

Hata mimi ningependa kupata PhD.
Hiyo Masters tu inanitoa kamasi kama mtoto wa tumbiri alo lowa maji ya mvua za masika kule Morogoro. PhD Je?

PHD Fake ni dalili moja kubwa ya kukosa uaminifu katika mambo yote unayo yafanya.


Watu hawa wanao foji PhD ukiwachunguza utagunduwa kwamba hata walipokuwa mashuleni walikuwa na vyeti Feki vya Ugonjwa ili shule iwapikie Light Diet na kusamehewa kufanya kazi za mikono.

MH mmoja tulikuwa naye shule kule Mazengo Dodoma, alikuwa na cheti cha daktari kwamba anaumwa Vidonda vya tumbo na Uti wa mgongo.

Sasa Kituko.

Nikiwa muajiriwa pale Dar siku moja tuligongana Joyce kwa Joyce(ana kwa ana) wote tukila Chipsi Dume zenye Pili Pili na chachandu la nguvu kwa mzee wa kuchoma mihogo pale karibu na Azania Sec School.

Jicho alilo nikata lilitosha kabisa kufunga nusu ya mdomo wangu.

Hata hivyo niliweza kumwuliza. " Vipi tatizo la tumbo liliisha?"

akanijibu yale yalikuwa mambo ya shule siku hizi kila kitu kinapita, siunajua mwenyewe dar hii na usawa ndo huu?
Nikamwuliza kazi anafanya wapi akaniambia Quality Garage kama Body Builder. Sikuwa na haja tena ya kumwuliza vipi tatizo la mgongo kwani jibu nilikuwa nalo tayari.

Ugonjwa na Vyeti vyote vilikuwa Fake

Wana JF na watanzania wote walio soma na kuelimika, jitokezeni mgombee Ubunge ifikapo 2010 ili Bunge letu tukufu liwe na Wabunge walio na elimu isiyo na maswali wala dalili za ubabaishaji.
Kusitasita kwenu ndiyo kunawafanya hawa wagonjwa hawa wenye uzoefu wa kufoji tangu secondary kutuongoza kama mikondoo mijinga wakati sisi ni watu na akili zetu.

Nchimbi subiri zamu yako ya kunawishwa.
 
Vihiyo ni wengi sana katika Tanzania. Kuanzia serikalini, mashirikani nk.

Kampuni ya sigara inaongoza kwa kuwa na vihiyo wengi ikifuatiwa na TRA. Sijui kwanini uchunguzi wa kina haufanywi kuhusu cheti cha mtu kabla ya kumpa kazi.
 
Mtambo,

TRA kuna vihiyo?! Kaka/dada upo serious?. Kumbuka hapa ni JF kuna watu wana data.

Naomba uthibitishe uliyoandika.
 
Back
Top Bottom