Dk. Kitine: CCM imechafuka; Apongeza maandamano ya CHADEMA

nngu007

JF-Expert Member
Aug 2, 2010
15,862
5,797
• Apongeza maandamano ya CHADEMA

Na Helena Denis

MKURUGENZI mstaafu wa Usalama wa Taifa, Dk. Hassy Kitine, amesema kuwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), kimechafuka na yeyote anayeingia madarakani anawaza kujitafutia fedha.

Amesema chama hicho kimechafuka zaidi hivi sasa kwa kuwa watendaji wake walivunja Azimio la Arusha na maadili ya uongozi.

Dk. Kitine, ambaye amepata kuwa Mbunge wa Makete, alitoa kauli hiyo jana wakati wa hafla ya kukabidhi zawadi kwa washindi wa Bahati Nasibu ya ‘Nina Ndoto', iliyoandaliwa na Kampuni ya Faidika inayojihusisha na utoaji wa mikopo.

Dk. Kitine alisema kuwa kutokana na uchafu huo, CCM imeamua kujivua gamba ili kujisafisha sehemu zote ilizokuwa imekosea.

"Walijiruhusu kwa muda mrefu kukaa na uchafu mpaka wameamua kujisafisha. Nani aliyewaweka uchafu kama si wao wenyewe?" alihoji Dk. Kitine.

Kitine alisema kuwa kuvunjwa kwa Azimio la Arusha, ambalo ndilo lililokuwa likiweka misingi mizuri ya viongozi wa umma, ndiko kumewafanya makada wa CCM kufanya mambo kwa utashi binafsi.

Alisema jambo kubwa lililopaswa kufanywa na makada wa CCM ambao ndio wenye kuiongoza serikali ni kujali zaidi masilahi ya wananchi pamoja na kuzingatia miiko ya kazi yao.

Hata hivyo aliisifia hatua hiyo kwamba ina lengo la kujisafisha na kusisitiza kwamba chama hicho kinapaswa sasa kuonyesha kwa vitendo kuwa kimejivua gamba.
Alisema yeye anapenda kusema ukweli kutokana na nafasi yake kwenye jamii, kwani alishalitumikia taifa katika ngazi tofauti kabla ya kustaafu.

"Mimi mara nyingi napenda kusema ukweli, lakini ninaposema ukweli viongozi wanachukia," alisema Dk. Kitine.

Akitolea mfano wa harakati za kuwania uongozi, Dk. Kitine alisema kwa hali ilivyo sasa watu wanataka uongozi ili wapate fedha badala ya kujali masilahi ya taifa.

Dk. Kitine alisema hali hiyo imetokana na kuvunjwa kwa Azimio la Arusha lililoweka maadili ya viongozi wa umma.

Kuhusu maandamano yanayofanywa sehemu mbalimbali na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), ambayo yamekuwa yakibezwa na CCM, Dk. Kitine alisema hauoni ubaya wake hasa kama yanalenga kuelimisha umma.

"Kama maandamano hayo ni ya maendeleo na yamelenga katika kuwasaidia Watanzania kuamka ili kujiletea maendeleo, sioni ubaya," alisema.

Akizungumzia hali ya uchumi nchini, Dk. Kitine alisema Watanzania chini ya asilimia moja ndio wanaomiliki asimilia 99 ya uchumi.

" Hali hii inatokana na kudharau miradi kama ya ‘Faidika' yenye lengo la kuwawezesha kumiliki uchumi nchini lakini kwa hali ilivyo sasa, wachache ndio wanaomiliki asilimia kubwa ya uchumi wa taifa hili, jambo ambalo ni hatari," alisema.

Akitangaza majina ya washindi wa shindano la ‘Nina Ndoto', Dk. Kitine alimtangaza mwalimu wa Manispaa ya Shinyanga, Sofia Simba, aliyeshinda sh milioni moja, Amir Othman (sh milioni tano), Makono Andrew (sh milioni tatu), Martin Lalika (sh milioni mbili) na Ferdinanda Lameck (sh milioni moja).

Dk. Kitine alisema lengo la ‘Faidika' ni kuwawezesha Watanzania kumiliki uchumi kwani hivi sasa taasisi hiyo ina matawi katika kila wilaya nchini.

 
Kikwete alisema serikali yake ni ya Kibepari Tatizo ni kuwa Viongozi wengi Serikalini bado wana Mrengo wa Kushoto Socialist ambao bado Wanazuia Wawekezaji Nchini anasema Wengi wao wako kwenye Kustaafishwa na Vijana Wanaingia kwenye hayo Madaraka

Kwahiyo Subirini another 4 yrs mtakumbuka kuwa Umasikini saa nyingine ni Uhuru; Ubepari na Ubeberu ndio Utumwa Mantinki

Everything will go to a selected class of people... Class society ni dhambi kuliko Udini na Ukabila
 
Kitime ilikuwa agombee urais wakala kichwa, na wakampaka matope kama ilivyokuwa kwa aliyeukosa urais kiduchu....Salim A.Salim;;;;Ama kweli tulikosa majembe ya kazi tukaishia kupiga picha za pamoja (Nyerere alituambia) na flying, handsome president ****** wa ukweli
 
Former Intelligence chief Hassy Kitine yesterday came out in support of the opposition Chadema’s stance on various issues.He told journalists in Dar es Salaam that demonstrations organised by Chadema across the country in protest at the spiralling cost of living and the party’s demand for the scrapping of sitting allowances were pertinent issues which the country’s leadership should take seriously.

Dr Kitine is the first prominent CCM cadre to have publicly supported Chadema’s cause, which has in recent months been roundly criticised by the ruling party and some opposition parties.He said it was a fact that the high cost of living was a heavy burden on Tanzanians, adding that something should urgently be done to address the situation.

Dr Kitine, a former Cabinet minister and MP, said whatever Chadema was doing to draw attention to such issues deserved support, and added that the opposition party should not be demonised for practising its democratic rights.
He made the remarks when journalists sought his comments on various national issues at the end of a meeting organised by Faidika, a microfinance institution in which he is a director.

Dr Kitine said he had also been closely following the debate on whether or not MPs and other holders of public office deserved sitting allowances.“What Chadema is doing is healthy for our democracy because everyone is entitled to their own opinion, but the views should be constructive…they should not be aimed at destroying the country.”

Dr Kitine warned that the widening gulf between the rich and poor was “very dangerous”, saying it posed a serious threat to peace and stability in Tanzania.He said the country could not expect to remain peaceful forever when a few individuals controlled 99 per cent of the economy.

Dr Kitine said he was only trying to speak the “truth”, although he was aware that his comments would not go down well in some quarters.“I, like other Tanzanians, am giving my views on various national issues, but I know that some people are not happy with my comments. But even if I don’t say what I am saying, other people will say it.”
On the Chadema demonstrations, Dr Kitine said what the opposition party was doing was a challenge to the government and other political parties.

“What we need to look at is what they (Chadema) are advocating in their demonstrations. If you talk of life having become unbearably tough, that’s reality because many people are feeling the pinch...I support the demonstrations although I’m a CCM member,” he said.

Comparing the reign of retired President Benjamin Mkapa and President Jakaya Kikwete’s Fourth Phase government, Dr Kitine said he had not noticed any major difference between the two phases.He said, however, that things had gone from bad to worse after principles enshrined in the Arusha Declaration were abandoned, adding that people were now freely buying their way into elective office.

“In the past, when I was appointed Director of Intelligence by Mwalimu Nyerere and later a minister before I became an MP, the sole motive for seeking leadership was to serve the people,” he said.

Dr Kitine said the political landscape had changed dramatically since the Arusha Declaration was shunted aside.
It was very difficult in the past for people who had amassed wealthy and failed to explain its source to be allowed to seek elective office, he said.

In a swift response, CCM Publicity Secretary Nape Nnauye told The Citizen that there was nothing wrong with convincing people to fight for their rights, adding that the issue was how this was done.

“Even CCM has been doing a lot to raise people’s awareness and sensitise them on their rights. Take for instance the decision to construct a secondary school in every ward across the country…this aims at increasing people’s awareness by giving them education,” he said when he toured Mwananchi Communications Limited head office in Dar es Salaam.

“The difference is that while we (CCM) are empowering the people by educating them, Chadema stops people from engaging in economic activities by holding demonstrations daily and deceiving them that this is a shortcut to State House,” he said.
 
We know why Kitine is saying all these today!!! its too late and he will never win it.
 
ni kutokana na kushindwa kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea asikitishwa na kauli ya rais kikwete ya kuwa wanaotaka ccm ife watakufa wao kwanza asema mwaenyekiti ccm taifa anakata tawi alilokalia yeye mwenyewe hivyo ategemee kuanguka pindi atakapo maliza kulikata
source chanel ten kipindi je tutafika?
 
siasa za ujamaa na kujitegemea ni za kitapeli kwani zinawapa wachache mwanya wa kula nchi kwa niaba ya wengi...they may sound good theoritically but they do not work practically.
 
Ujamaa na kujitegemea sio kwa manufaa ya wachache mkuu, rudi tena darasani ukajifunze!
darasa langu zuri ni hapa Tanzania nilipo kila siku nikiamka nikiingia mitaani nakuwa darasani na siyo kwenye makaratasi kama wewe...
nikienda mahospitalini najifunza, nikienda mashuleni naona na wanaopeleka watoto wao kusoma wanafahamika na wanaotumia kodi za wananchi kwenda kutibiwa nje india na usa wanafahamika na siyo wanaotibiwa mwananyamala au muhimbili hospital huo ndio ujamaa na kujitegemea ulichotuletea in practical.
 
Aongee tu maana ni haki yake kikatiba, lakini Ccm haitakufa kwa sababu ya kauli ya mtu yeyote.
 
Aongee tu maana ni haki yake kikatiba, lakini Ccm haitakufa kwa sababu ya kauli ya mtu yeyote.

Haujajibu hoja ya msingi ya Mzee Kitine, unless na wewe unawatabiria kifo wanaoitabiria CCM kifo iwapo haitabadilika kuepuka kifo kwani katika hali ya sasa, the future of CCM ni kifo;
 
ni kutokana na kushindwa kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea asikitishwa na kauli ya rais kikwete ya kuwa wanaotaka ccm ife watakufa wao kwanza asema mwaenyekiti ccm taifa anakata tawi alilokalia yeye mwenyewe hivyo ategemee kuanguka pindi atakapo maliza kulikata
source chanel ten kipindi je tutafika?

OH YEAH Baada ya KUCHOTA PESA za UONGO kutibu MKEWE NJE YA NCHI; alilipwa MARA DUFU zaidi ya MATIBABU walivyowachaji na HELA sa SERIKALI ndio ILIKUWA inalipa; UGONJWA wenyewe UNGEWEZA hata kutibiwa TANZANIA lakini wakagushi MAANDISHI ya MADAKTARI ili tu waende NJE na KUSHOP... Sasa alipotaka kugombea TENA akashindwa kwenye CHAGUZI za CCM; LEO HII ANAFANYA kusahau UFISADI wake???

NA CCM na SERIKALI yake hawakumshitaki waliacha yapite TANGANYIKA ni TAJIRI utaiba na bado UKO HURU hauendi JELA...

HUYO NI MWIZI HAFAI KABISAAAAA
 
ni kutokana na kushindwa kufuata siasa ya ujamaa na kujitegemea asikitishwa na kauli ya rais kikwete ya kuwa wanaotaka ccm ife watakufa wao kwanza asema mwaenyekiti ccm taifa anakata tawi alilokalia yeye mwenyewe hivyo ategemee kuanguka pindi atakapo maliza kulikata
source chanel ten kipindi je tutafika?

Nani kamkabidhi kazi ya marehemu sheikh Yahaya..?!
Haya na tusubirie hicho kifo cha ccm...,
Mie mchango wangu ni sanda ya HARIRI na jeneza la DHAHABU!!
Magamba msinitoe machooo.., natania tu!!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom