Diwani wa CHADEMA Gibson Meseyeki auza Kata kwa CCM........

Meitinyiku L. Robinson

JF-Expert Member
Aug 29, 2011
412
90
Ni Diwani ya kata ya Olturoto kwa tiketi ya CDM ambaye kwa asilimia 95 amesabisha kata kwenda kwingine. Pamoja na jitihada zake za kutoa pesa zake mpaka kufikia kiwango chake cha mwisho huyu jamaa kaonekana kuwa nincompoop;

Kimsingi huyu jamaa baada ya kutoa lile liRange lake likapigwa rangi za chama basi ameshaanza kujiona kuwa yeye ndiye kila kitu ndani ya Chama Mkoani Arusha na hakuna kinachoweza kufanyika bila yeye. Na amekuwa akijitunuku majina hasa lile la mfadhili mkuu wa CDM Mkoani Arusha.

Jeuri hii na kiburi hiki ndiyo ilimfanya adharau viongozi wadogo wa Kata ya Bagata na hata Wilaya ambao ndio waliokuwa chachu ya CDM katika Kata hiyo kwa kuwabebesha tuhumu nzito na kutokana na hizo nguvu zake za pesa hakutaka hata kuwapa nafasi ya kusikilizwa jambo ambalo liliwapa hasira wanachama wengi hasa wa Sasi na kuamua kukihama Chama hicho.

Jamaa amekuwa akijinadi kuwa ndiye Mbunge wa Jimbo la Arumeru na kama Chama hakitampitisha basi Chama nacho kisahau ufadhili wake na gari lakee arudishiwe. Kauli hizi ndizo zilizomgaribi na watu wameamua kumwonesha kuwa kwa tabia aliyonayo hata huo Ubunge ausahau. Hii inatokana na yeye kuonekana kutumia pesa nyingi kumbe anachotegemea ni kulipwa fadhila na Chama kwa kuteuliwa kuwania kiti cha Ubunge. Hivyo jamaa kunyukwa Bangata ni funzo tosha kwake na kaambiwa huo ni mwanzo tu.

Viongozi wa ngazi za juu kuanzia Mkoa na hata Taifa wameonesha kumwogopa sana huyu mtu manake walifikishiwa malalamiko ila mpaka Kata inaondoka hawakuchukua hatua zozote ikiwa ni kwa kumwonya hata kwa maneno. Hivyo ni dhahiri kuwa nguvu za pesa zinaendela kudhihirisha namna zinavyotesa vyama vya siasa Nchini.

Na nguvu hizi zimedhihirishwa na namna ambavyo Chama kiko tayari kupoteza ushindi na si kuwakwaza wale wenye kukisaidia. Yani Sabodo naye angeingia kwenye Siasa hali ingekuwa tete............ Gibson hongera sana
 
haya ulipaswa kuyasema kabla ya uchaguzi ili yasahihishwe na kuleta matokeo mazuri sasa tumepoteza kata wewe ndio unakuja na utumbo wako hapa? ni kuwa unashangilia kupoteza kata au vipi? au wewe ni gamba? Tumia wakati akili wakati mwingine,.usipende kujipatia umaarufu kwa kutumia matokeo haya mabaya!!
 
haya ulipaswa kuyasema kabla ya uchaguzi ili yasahihishwe na kuleta matokeo mazuri sasa tumepoteza kata wewe ndio unakuja na utumbo wako hapa? ni kuwa unashangilia kupoteza kata au vipi? au wewe ni gamba? Tumia wakati akili wakati mwingine,.usipende kujipatia umaarufu kwa kutumia matokeo haya mabaya!!

Soma thread na kuielewa acha ulimbukeni....... Yalishasemwa kwenye vikao husika ila anaogopwa. Uwoga huo ndo mavuno ya haya yote.....
 
Soma thread na kuielewa acha ulimbukeni....... Yalishasemwa kwenye vikao husika ila anaogopwa. Uwoga huo ndo mavuno ya haya yote.....

wewe sio limbukeni tu ni dunya hujui unachoongea wala hujui Arusha iko wapi wala hujui vikao vya chama vinaongozwaje, hebu nukuu kikao kimoja kilichozungumzia swala hilo na nani anamuogopa?? ukianza kunitolea maneno ya kijinga bila point utasababisha ban bure nina hasira kupoteza hiyo kata kijinga bado wewe unaleta upuuzi juu ya upuuzi just keep qiute!
 
Muacheni Kamanda Gibson, ni kweli alijitolea kwa hali na mali sema tuu huyu mgombea wenu naye alikuwa hauziki. Suala la kugombea Ubunge mbona badoo.:eek:hwell: si tusubiri hiyo 2015 ifike. matamanio sio mabaya ila yaende kwa utaratibu. Hata Laigwanani Lowassa bado hajatamka lakini anapambana.
Lakini kumbuka msemo usemao " IF WISHES WERE HORSES EVEN HORSES COULD RIDE"
 
Hizi siasa za CDM na Tanzania mbona Kichefuchefu? CDM isiposhinda ni NONGWA ikishinda NONGWA nyie mwataka nini? Mtaanza kulana wenyewe kumbukeni mmefikia pabaya ambapo wa kuwarudisha nyuma ni akili binafsi ama sivyo sioni kama mnajijua mnakoenda!!
 
Kwanza kabisa naomba nitumie nafasi hii kukanusha taarifa hizi, mimi nilikuwa mmoja wa kati ya waliompigia debe mgombea wa chadema ndug erick samson mollely, taarifa hizi si za kweli ni upotoshaji mkubwa mh. Gipson ole miseyeki ni diwani wa kata ya olturot na hakuwahi kutangaza nia ya kugombea jimbo ubunge kwenye jimbo lolote, tulishindwa udiwani bangata kwa sababu zifutazo;
1. Watu wengi hawajui kusoma wala kuandika, hivyo ccm walitumia fursa hiyo kuwahonga wazee wengi ambao ndio waliokuwa na shahada za kupiga kura kwa hela na waliwapa watu wa kwenda kuwa saidia kupiga kura
2. Chadema tuliungwa mkono na vijana lakini hawakuwa na shahada za kupiga kura.
Hivyo mh olemiseyeki hausiki kwa chochote
 
Frank nakubaliana na wewe, acha kilaza shondola. Hizo ndo point za kuleta kwa watu great thinkers kama cc hapa. Tena nakushukuru, tufanyie kazi mawazo haya.


Kwanza kabisa naomba nitumie nafasi hii kukanusha taarifa hizi, mimi nilikuwa mmoja wa kati ya waliompigia debe mgombea wa chadema ndug erick samson mollely, taarifa hizi si za kweli ni upotoshaji mkubwa mh. Gipson ole miseyeki ni diwani wa kata ya olturot na hakuwahi kutangaza nia ya kugombea jimbo ubunge kwenye jimbo lolote, tulishindwa udiwani bangata kwa sababu zifutazo;
1. Watu wengi hawajui kusoma wala kuandika, hivyo ccm walitumia fursa hiyo kuwahonga wazee wengi ambao ndio waliokuwa na shahada za kupiga kura kwa hela na waliwapa watu wa kwenda kuwa saidia kupiga kura
2. Chadema tuliungwa mkono na vijana lakini hawakuwa na shahada za kupiga kura.
Hivyo mh olemiseyeki hausiki kwa chochote
 
Frank nawe unaongea pumba, utasemaje cdm imeshindwa kwa kuwa watu hawajui kusoma wala kuandika. Hayo uliyajua baada ya kushindwa au ...Na wakati kata ilipkuwa cdm hao hao watu walijua kusoma na kuandika miaka miwili baadaye wapenzi wa cdm hawajui k&k. Acha ujinga utachekwa, sema watu wameanza kuchoka maandamano yasiyo na tija na kupotezewa muda bila sababu. Kubali cdm imeshindwa kihalali, watu washaamia AIRTEL
 
Soma thread na kuielewa acha ulimbukeni....... Yalishasemwa kwenye vikao husika ila anaogopwa. Uwoga huo ndo mavuno ya haya yote.....

Wivu tu, huna lolote. Peleka application yako na CV yako pale kwenye kampuni yake ya TANZANIA (2000) ADVENTURES LTD ufikiriwe kupata ajira. Acha kuchafua watu huku.

 
Kama kuna tatizo wahusika wafuatilie na c.o. tabia ya kusikia lalamiko na kuanza kutoleana maneno ya kashfa. Sawa inwzekna ni kweli au majungu lakini la msingi siyo jazba. Jifunzeni kwa watani zetu wanatoleana bastola mfano hai TABORA.Tujenge CHADEMA
 
Kwanza kabisa naomba nitumie nafasi hii kukanusha taarifa hizi, mimi nilikuwa mmoja wa kati ya waliompigia debe mgombea wa chadema ndug erick samson mollely, taarifa hizi si za kweli ni upotoshaji mkubwa mh. Gipson ole miseyeki ni diwani wa kata ya olturot na hakuwahi kutangaza nia ya kugombea jimbo ubunge kwenye jimbo lolote, tulishindwa udiwani bangata kwa sababu zifutazo;
1. Watu wengi hawajui kusoma wala kuandika, hivyo ccm walitumia fursa hiyo kuwahonga wazee wengi ambao ndio waliokuwa na shahada za kupiga kura kwa hela na waliwapa watu wa kwenda kuwa saidia kupiga kura
2. Chadema tuliungwa mkono na vijana lakini hawakuwa na shahada za kupiga kura.
Hivyo mh olemiseyeki hausiki kwa chochote

Waii! Comrade hapa ni kupigwa mumepigwa vizuri sana hivi visingizio visivyo
Na mantiki wekeni kando msije kuwa kama mbaazi pale ikosapo tunda.....
 
wewe sio limbukeni tu ni dunya hujui unachoongea wala hujui Arusha iko wapi wala hujui vikao vya chama vinaongozwaje, hebu nukuu kikao kimoja kilichozungumzia swala hilo na nani anamuogopa?? ukianza kunitolea maneno ya kijinga bila point utasababisha ban bure nina hasira kupoteza hiyo kata kijinga bado wewe unaleta upuuzi juu ya upuuzi just keep qiute!

Mtu kama wewe siwezi kukutofautisha na soksi na viatu......... Manake ukiabudicho hukiamini ila akiabudicho Gibson kwako burdaaaaani...... Pole
 
Back
Top Bottom