Diwani CHADEMA arejea CCM

Mwigulu mtu makini na mjanja sana,,, ana uwezo mkubwa wa kutokomeza kabisa upinzani Iramba. Dogo alikuwa mbishi sana lakini kavaa kisiki mwa Mchemba
 
Siasa uchwara hizi hata Rostam zimemshinda. alichaguliwa na wananchi kwenye kata yake ili alete maendeleo sasa sioni conection yoyote ya alichokiongea, lakini hii ni habari njema kwa Chadema kwamba iwe makini na mamluki na iwe ni marufuku kuchukuwa makapi ambayo yameshindwa kwenye kura za maoni ccm.
Hakuna sababu ya kuwa na mtu ambae sio muumini wa mabadiliko ila anafuata fursa tu ya kugombea kupitia mwamvuli wa chama makini, watu wa namna hii ni mzigo kwa chama, mfano Shibuda sio mwanamabadiliko lakini Fred Mpendazoe yuko siriasi na kazi ya kuleta mabadiliko.
 
Bado hajawa na hoja thabiti za kuwashawishi wananchi juu ya uamuzi wake, ila ninachoweza kukisema tu ni kwamba kama umewasha moto shamba la mabua unatarajia kuuzima kwa kikombe cha maji? La hasha haiwezekani hata kidogo, wewe umeshiriki kuwasha moto sasa umeshika kasi unatamani kuuzima tena kwa vifaa duni - haiwezekani hata kidogo
 
huyo amedanganywa na Mwigulu kwa maneno tu na kupewa lift mpaka dom. akili ndogo, upeo mdogo atjuta baadae kwasababu Mwigulu mwenyewe hatarudi 2015 na CCM haitakuwepo Iramba magharibi.
 
Hata wakati wana wa israel wanatolewa utumwani misri kuna ambao walimlalamikia musa kuwa amewapeleka ili wakafie jangwani na walitamani kurudi misri kwa hiyo siyo ajabu kwa huyu diwani kurudi misri (ccm)
<br />
<br />

marakhabaa
 
CCM wanaweza kuwa nunua madiwani na baadhi ya wabunge wa cdm, ila kamwe hawawezi kuwanunua wafuatao ambao ndiyo mwiba kwao.
1.Mbowe
2.Dr Slaa
3. Mnyika
4.Lisu
5.Mdee
6.Mchungaji Msigwa
7. Nyerere
8. dogo wa mbozi
9.wenje
10. Mchungaji Natse

CCm wachukue akina shibuda,akina Mallah na wegingene wote. Kama hawajaweza kuwanunua japo mmoja ya hao hapo juu basi kazi yao ni bure na hawataweza kuzuia kifo kinachowakabili sasa.
 
kuna wale watano waliofukuzwa na leo asubuhi watatanga msimamo wao, CCM jiandaeni kuwapokea..
 
Mbona walishaondoka akina Kaborou CDM haijaanguka? Huyu Diwani upeo wake umekaa kimagamba! Ndani ya "utulivu na amani" kuna ufisadi wa kutisha na bila kuwapelekesha mchakamchaka Magamba yatakula bila kufuta midomo!

Yaani ukiwa na baba la hivyo ni aibu kubwa hata kwa marafiki zako!

Utafikiri linatumia ****** kufikiria. Nchi inaibiwa lenyewe linatuhumu maandamano!! Bila maandamano ya CDM lini Wasukuma wangeamka?

Aliuta continua!!
 
WAKATI ikiwa katika mgogoro na madiwani wake wa Arusha, Chadema imepata pigo baada ya mmoja wa madiwani wake Singida kujiengua na kurudi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), akidai hataki kuwa sehemu ya machafuko nchini.

Diwani huyo, Simon Tyosela wa kata ya Urughu, Iramba Magharibi, alisema hayo jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, mbele ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia masuala ya Uchumi na Fedha, Mwigulu Mchemba.

Tyosela aliyehamia upinzani wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 baada
ya kuanguka katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema hakushawishiwa kuihama Chadema na kurejea CCM, bali amenusa hatari kwa taifa katika siku za usoni.

Alisema, maandamano yenye sura ya uchochezi kila kukicha, yamemkosesha amani na
kujiona msaliti mbele ya Watanzania.

“Haya ya kushinikiza wananchi kuiga maandamano katika nchi za wenzetu, tena yasiyo ya amani, binafsi yamenishinda. Chadema hakuna demokrasia ya kweli na nilitarajia ingekuwa mstari wa mbele kuhangaikia maendeleo ya wananchi. Nimejiondoa kwa sababu mimi ni mpenda amani kwa nchi yangu.

“Kwa mtindo huu niliona kabisa hatuwezi kufikia malengo ya millennia, kwa sababu
kila kukicha ni maandamano, hakuna la maana linalofanyika kwa ustawi wa nchi
yetu,” alisema diwani huyo.

Alisema, hana cha kujutia kwa sababu wananchi ndio waliokuwa wamemshawishi kuingia Chadema wakitaka atumie chama kingine chochote kuingia madarakani, baada ya kushindwa kura za maoni.

Mchemba alimpongeza na kuitaka jamii kutokubali kuburuzwa na vyama vingine vya siasa kwa maslahi ya watu wachache wenye mwelekeo wa kulazimisha kushika madarakani kwa nguvu.
Huyu Diwani hakuwa katika kusimamia haki za Watanzania shida yake ni uongozi na kuzitafuna haki za Watz, hao ndio wale wale, Gamba la kuvua, amepima akaona CDM hakuna za kutafuna, akaona arudi kwa system aliyoizoea, tazama kauli yake ya mwanzao "Nimeamua kujiuga Chadema bila kushawishiwa na mtu" alafu kauli ya pili "Nilijiuga kugombea kupitia CDM nilishawishiwa na wananchi" je ajatujuza kurudi CCM ni nani amemshawishi, na kauli ya kuwa huko anapotoka kunachochea vurugu au uvunjifu wa amani, ni kauli ya nani!??? Hawa ni baadhi ya viongozi ambao Watz wanatakiwa kuwa makini nao sana, hawa ni mizimu inayokunywa damu ya Watz. hata huko walipomtosa wanamfahamu ya kuwa huyo jamaa ni kipofu wa mawazo ni mcheza karata asiyekuwa na turufu.
 
diwani mbona mtu mdogo sana huyu njaa inamsumbua mbona wapo madiwani wengi
sana maslahi ndani ya chadema walitumwa kufanyia upelelezi waliomtuma wamemwita
kwa heri wasalimie huku waambie magamba kuwa .

kikupacho raha na uchungu kitakupa
 
Mbona huyu diwani alia hama mdamrefu sana kwa bahati mbaya haikulipotiwa kwny vyombo vya habari mwezi ule zaidi ya habali leo.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom