Diwani CHADEMA arejea CCM

Vyama vya siasa vijifunze kutafuta watu waaminifu, na wenye uzalendo wa kweli, watu kama hawa wanaweza kushusha sifa ya chama kwa kutokuwa wavumili katika harakati!!!

Nafikiri huo ndio mtihani mkubwa sana kwa CHADEMA maana uaminifu haupimwi kwa kauli za juu juu tu. Nadhani uaminifu unaweza kupimwa kwa dhamira ya dhati ya mtu ya kutaka kuleta maendeleo kwa wananchi wake. Na hii haijifichi kwa sababu inaonekana katika uzalendo wa mtu. Hatetei hoja kwa vile zimeletwa na chama chake bali anatetea maslahi ya taifa.

Nimesoma hoja nyingine katika thread hii zinasema CDM wajihadhari kuchukua watu wanaokuwa wameachwa/ kubwagwa kutoka CCM. Mimi natoafautiana nao. Maana kama ni hivyo basi leo tusingekuwa na Dr. W. Slaa.

Nadhani CDM inahitaji kuangalia kwa dhati dhamira ya watu itakaowasimamisha kugombea nafasi mbalimbali kwa kuangalia track record zao. Je wana dhamira ya kweli ya kuwasaidia wananchi wao na taifa kwa ujumla? Na hii haitajalisha ama wako ndani ya CDM au ni wahamiaji. Hakuna chama kitakachoepuka kupata wahamiaji wakati wowote. CDM hivi majuzi wamempata Profesa Safari ambaye ametokea CUF; tusemeje hapo?

CDM inao kina Shibuda sasa hivi ambao wamekuwa mwiba sana kwa chama.Track record ya Shibuda ni ya uchu wa madaraka. Naomba kurudia, Shibuda (mkazi wa upanga, mtaa wa Kalenga) ana uchu wa madaraka. Hii imeonekana alipokuwa kwenye vyama vya wafanyakazi na ndani ya chama kilichomlea. Mtu kama huyu hakufaa kukaribishwa kwenye chama chochote na hasa chama makini kama CHADEMA.
 
huyo diwani upeo wake ni mdogo sana. anadai cdm wanafanya maandamano badala ya maendeleo, angejiuliza kabla ya maandamano ya cdm kuna maendeleo gani yaliyopatikana na hasa mkoa singida ndio mikoa ya mwisho kwa maendeleo. leo tunakwenda miaka 50 ya uhuru nchi ipo gizani, vijana hawana ajira, wastaafu wanataabika imefikia hadi wazee EAC wanalala barabarani huku wamevua nguo hayo ndio maendeleo? na afadhali ametoka mapema huyo mamluki akapotee kama alivyopotea kabouru,lamwai na wengine. atuache cc tuendelee kutoa elimu ya uraia kwa waliolala. maendeleo hayapatikani bila ya maandamano ya chadema peoplesssssssssssssssssssssssss................
 
makamanda msijali saa ya ukombozi inakaribia, lazima tukutane na majaribu kama hilo gamba lililojipenyeza kwa ajili ya tumbo lake. jipeni moyo huko ccm giza limezidi mno na hivyo karibu kunapambazuka kwa cdm..............freedom is on ur door
 
nenda baba wasalimie wote ila usije toka tena na wewe ukasema siasa uchwara
 
WAKATI ikiwa katika mgogoro na madiwani wake wa Arusha, Chadema imepata pigo baada ya mmoja wa madiwani wake Singida kujiengua na kurudi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), akidai hataki kuwa sehemu ya machafuko nchini.

Diwani huyo, Simon Tyosela wa kata ya Urughu, Iramba Magharibi, alisema hayo jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, mbele ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia masuala ya Uchumi na Fedha, Mwigulu Mchemba.

Tyosela aliyehamia upinzani wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 baada
ya kuanguka katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema hakushawishiwa kuihama Chadema na kurejea CCM, bali amenusa hatari kwa taifa katika siku za usoni.

Alisema, maandamano yenye sura ya uchochezi kila kukicha, yamemkosesha amani na
kujiona msaliti mbele ya Watanzania.

“Haya ya kushinikiza wananchi kuiga maandamano katika nchi za wenzetu, tena yasiyo ya amani, binafsi yamenishinda. Chadema hakuna demokrasia ya kweli na nilitarajia ingekuwa mstari wa mbele kuhangaikia maendeleo ya wananchi. Nimejiondoa kwa sababu mimi ni mpenda amani kwa nchi yangu.

“Kwa mtindo huu niliona kabisa hatuwezi kufikia malengo ya millennia, kwa sababu
kila kukicha ni maandamano, hakuna la maana linalofanyika kwa ustawi wa nchi
yetu,” alisema diwani huyo.

Alisema, hana cha kujutia kwa sababu wananchi ndio waliokuwa wamemshawishi kuingia Chadema wakitaka atumie chama kingine chochote kuingia madarakani, baada ya kushindwa kura za maoni.

Mchemba alimpongeza na kuitaka jamii kutokubali kuburuzwa na vyama vingine vya siasa kwa maslahi ya watu wachache wenye mwelekeo wa kulazimisha kushika madarakani kwa nguvu.


chadema siyo chama cha maslahi.
 
Wakuu hebu tuchungulie AKAUNTI yake katika kipindi cha siku 90 zilizopita; kapokea bei gani toka kwa magamba huyu bwana????????????

Siku zote si mchezo kuleta mabadiliko kamili katika nchi bila JUDAS ISKARIOTA kujitokeza.


WAKATI ikiwa katika mgogoro na madiwani wake wa Arusha, Chadema imepata pigo baada ya mmoja wa madiwani wake Singida kujiengua na kurudi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM), akidai hataki kuwa sehemu ya machafuko nchini.

Diwani huyo, Simon Tyosela wa kata ya Urughu, Iramba Magharibi, alisema hayo jana katika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM mjini Dodoma, mbele ya Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa ya CCM anayeshughulikia masuala ya Uchumi na Fedha, Mwigulu Mchemba.

Tyosela aliyehamia upinzani wakati wa mchakato wa Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2010 baada
ya kuanguka katika kura za maoni ndani ya CCM, alisema hakushawishiwa kuihama Chadema na kurejea CCM, bali amenusa hatari kwa taifa katika siku za usoni.

Alisema, maandamano yenye sura ya uchochezi kila kukicha, yamemkosesha amani na
kujiona msaliti mbele ya Watanzania.

“Haya ya kushinikiza wananchi kuiga maandamano katika nchi za wenzetu, tena yasiyo ya amani, binafsi yamenishinda. Chadema hakuna demokrasia ya kweli na nilitarajia ingekuwa mstari wa mbele kuhangaikia maendeleo ya wananchi. Nimejiondoa kwa sababu mimi ni mpenda amani kwa nchi yangu.

“Kwa mtindo huu niliona kabisa hatuwezi kufikia malengo ya millennia, kwa sababu
kila kukicha ni maandamano, hakuna la maana linalofanyika kwa ustawi wa nchi
yetu,” alisema diwani huyo.

Alisema, hana cha kujutia kwa sababu wananchi ndio waliokuwa wamemshawishi kuingia Chadema wakitaka atumie chama kingine chochote kuingia madarakani, baada ya kushindwa kura za maoni.

Mchemba alimpongeza na kuitaka jamii kutokubali kuburuzwa na vyama vingine vya siasa kwa maslahi ya watu wachache wenye mwelekeo wa kulazimisha kushika madarakani kwa nguvu.
 
Katika mapambano wapo watu kama Musolini ambao kwa mtazamo wao wako radhi kuingia utumwani kuliko kujitoa mhanga. Tusiwalaumu sana inapofikia kuchumia tumbo..Hata ktk historia ya kupigania Uhuru wetu wapo watu wengi sana waliokuwa upande wa mkoloni na walimtumikia Malkia kufanya ukachero dhidi ya chama cha TANU na viongozi wake...Yap! fikiria mtu kuwasaliti wananchi wote na kuungana na Mkoloni kwa visingizio kama hivi.. Na hata hao ukiwauliza wangesema Nyerere na TANU wana - sura ya uchochezi kila kukicha, yamemkosesha amani na
kujiona msaliti mbele ya Watanganyika!.

 
Na wengine wa aina hiyo kama wapo waondoke woote! Kuwa na wapiganaji shupavu 10 ni bora kuliko wenye asili ya magamba 100. Hatutishiki.
 
Kuna yule wa songea kahamia CDM ! mbona Magamba hamkusema kitu! na yeye anafuata furugu CDM!

" sintokufa mpaka CCM itakapokufa" Rest in peace Mzee Mahimbo
 
Sasa ni hivi nauomba uongozi wa CDM waache kupokea hawa mamluki,kutoka chama cha magamba kwani wakinyimwa madaraka huko,wanakimbilia CDM kupoza maumivu yao, WAMESHAONA KAMA CDM NI YA KUPUNGUZIA MACHUNGU?tunaomba hiyo tabia iwe mwisho wawe wanaenda CUF.
 
Nampongeza kwa kushindwa kuwa mwanamapinduzi wa kizazi hiki
Atavuna alichopanda na siku si nyingi ataanza kujuta kwa hili
 
Huyo hana maana kwani inaonesha ni jinsi gani alivyo mroho wa madaraka baada ya kushindwa kwenye kura za maoni(ccm)ndio akahamia cdm tena kwa kushawishiwa!ni bora alivyojitoa cdm hakuna wanafiki kuna makamanda.Tena vitani m2 kama huyu anapigwa risasi,wakati makamanda wa cdm wako mstari wa mbele yeye anarudi nyuma!HAKUNA KULALA MPAKA KIELEWEKE.
 
Wapi kina Kaborou?tabia ya kuchumia tumbo hiyo

Ngoja tukutane Igunga,mbivu na mbichi tutajua
 
Alizoea pesa za bure kwa magamba ila nina wasi wasi na upeo wake maana haki haiji hivi hivi kwa nchi zetu hizi "You have to fight for it". Salimia Iramba.

upeo hautazamwi kwa mlengo ulionao wewe ndugu yangu, na siku zote you need to be a go between na siyo single sided figure kiasi cha kuona mawazo ya huyo diwani hayana nafasi, kumbuka ni juzi tu Mbeya Jiji kata ya nzovwe diwani mwingine wa chadema kajiuzulu kwa mtazamo unaofanana na huo, nadhani ni wakati sasa cdm kuja na utafiti wa kina/kisayasi si majibu tena ya akina Makamba " MAJIBU RAHISI KWA MASWALI MAGUMU"
 
Bora kaondoka. Alisaidia angalau kusaidia chama chake kipendwa CCMagamba kukosa udiwani katika hiyo kata aliyogombea. Naamini wana wa Iramba sasa wataweka mpiganaji wa kweli. Twende Tundu twende.........
 
Yule wa mbeya vpi maana alikuwa mguu ndani mguu nje,hawa jamaa wamezoea hela za bure but hii inatakiwa ifanyiwe kazi na cdm.
 
Mbona walishaondoka akina Kaborou CDM haijaanguka? Huyu Diwani upeo wake umekaa kimagamba! Ndani ya "utulivu na amani" kuna ufisadi wa kutisha na bila kuwapelekesha mchakamchaka Magamba yatakula bila kufuta midomo!

tatizo la tanzania si mfumo na nachelea kusema si magamba bali ni WATANZANIA wenyewe wengi ni waoga hata wakipokwa HAKI zao hukaa kimya kwa kisingizio cha AMANI na UTULIVU.umeme mafuta nk na bado tupo kimya tu aman utulivu,acha magamba watumie vijisenti walivyotupoka waendelee kutunyonya
 
Back
Top Bottom