Tamaa ,kotojipanga na kuridhisha wazazi,vijana wengi wanajua wakishapata mkopo wa vitz kazini na akishanunua flat screen na blackbery tayari anatangaza ndoa,atasumbua michango mbaya,kumbe ajui cost za kuishi wawili,Wasichana nao wanataka mtu mwenye pesa,sasa anakutana na kijana amepata kajimkopo kazini na ana mark2 analazimisha ndoa,baada ya miezi 6 ya ndoa msela kaishiwa msichana anaanza umapepe.wengine wanajua kabisa kuwa maisha bado ayajakaa level anakubaliana na wazazi aoe ili wapate wajukuu,kwa hofu anaingia ktk ndoa baadae wanachemka
Lack of commitment. Watu hawataki kukabili changamoto zinazotokea kwenye maisha, kama alivyosema ndugu chipukizi. Na hii si katika ndoa pekee iko pia katika nyanja mbalimbali. Unaonaje mwanafunzi anapopewa assignment badala ya kufukua vitabu na kupata majibu anakimbilia kuomba msaada kwa watu wengine?
Ni ufinyu wa watu kutofahamu kwamba marriage is an institution which we define to be a contract between man and woman which is intended to last for the rest of their lives!
Ndoa za siku hizi ni fashion, wanaume wanapoteza nguvu ya kiuchumi kwa kufanya harusi ya siku moja kwa milioni 40 wakati hata hana investmen yeyote, akitoka hapo anarudi kusubiri vilaki tano kwa mwezi.
Mwanamke nae kamuona kijana handsome, amesoma, ana kazi, anajitegemea na kanyumba ka kupanga pale sinza kana HED au LCD, amepaki GX110, anavikochi vya mlimani city pale, dada anaona huyo ndiye mwanaume, kumbe jamaa alipewa na wazazi wakati anaanza maisha.
Binti ana kazi yake, kila anachoambiwa na bwanake anasema 'am independent' i got my job, my car, my education, and the guy say the same too!
Kazaa, amependeza kapata kamwili kakiutu uzima, amejazia kang'ara, kakutana na exboyfriend akamsifia na kumuomba namba, wanachat eti friends on facebook, mume kaona, then guess what is next?
TUBADILIKE.
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.