Cheguemtz
New Member
- Aug 7, 2011
- 2
- 0
Wafanyakazi TBL tunaomba serikali iingilie kati swala lililopo kati ya Management ya TBL na wafanyakazi la sivyo wazawa tutazidi kunyanyaswa ndani ya nchi yetu! Makaburu wamewatunuku madaraka baadhi ya wazawa na hivyo kushindwa kututetea hata pale tunapokuwa na madai ya msingi.
Na hii mimi naiita "DEVIDE AND RULE" kwani hawa viongozi wazawa wanadanganywa kwa mishahara mikubwa ya nafasi wanazozawadiwa pasipokuwa na elimu na sifa za nafasi husika.
Mnamo tarehe 04 August 2011 Mwenyekiti wa chama cha wafanyakzi(TUICO) tawi la TBL Dar amesimamishwa kazi eti kwa tuhuma ameshinikiza mgomo wa wafanyakazi siku ya tarehe 03 August 2011.
Suala lilipo hapa ni madai ya maslahi kwa wafanyakazi kulingana na hali ya kampuni kwani kila baada ya miezi minne MD hutoa brief ya muelekeo wa kampuni na huwa anaelezea faida kubwa TBL inayoipata lakini ukifika wakati wa negotiation kati ya Management na TUICO kuhusu maslahi ya wafanyakazi huwa wagumu kutupatia kiwango kinachoendana na hali ya kampuni... Why?
Mwenyekiti wa TUICO alituhumiwa kuwa anatumiwa na chama cha siasa kuandaa maandamano ya wafanyakazi TBL kitu ambacho sio kweli. Media nyingi nchini huwa hazireport uozo wa TBL kwa kuwa kuna tetesi kuwa TBL huandaa tafrija kwa ajili ya wafanyakazi wa media nchini kama ilivyokuwa hapo mwaka huu iliyojulikana kama Media Funny Day ambapo walivalishwa T-Shirt zenye nembo ya TBL. Hivi kweli tutafika kama hali yenyewe ndivyo ilivyo?
TBL kuna uozo mwingi sana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa na serikali ama wadau wake... Serikali inayakumbatia maovi ya TBL kwa sababu shria ya uwekezaji nchini ina mapungufu mengi. Tunaomba msaada wenu Jamii Forum ili tujikomboe wazawa kwani serikali yetu imeshindwa kumlinda mwananchi wake.
Cheguemtz!
Na hii mimi naiita "DEVIDE AND RULE" kwani hawa viongozi wazawa wanadanganywa kwa mishahara mikubwa ya nafasi wanazozawadiwa pasipokuwa na elimu na sifa za nafasi husika.
Mnamo tarehe 04 August 2011 Mwenyekiti wa chama cha wafanyakzi(TUICO) tawi la TBL Dar amesimamishwa kazi eti kwa tuhuma ameshinikiza mgomo wa wafanyakazi siku ya tarehe 03 August 2011.
Suala lilipo hapa ni madai ya maslahi kwa wafanyakazi kulingana na hali ya kampuni kwani kila baada ya miezi minne MD hutoa brief ya muelekeo wa kampuni na huwa anaelezea faida kubwa TBL inayoipata lakini ukifika wakati wa negotiation kati ya Management na TUICO kuhusu maslahi ya wafanyakazi huwa wagumu kutupatia kiwango kinachoendana na hali ya kampuni... Why?
Mwenyekiti wa TUICO alituhumiwa kuwa anatumiwa na chama cha siasa kuandaa maandamano ya wafanyakazi TBL kitu ambacho sio kweli. Media nyingi nchini huwa hazireport uozo wa TBL kwa kuwa kuna tetesi kuwa TBL huandaa tafrija kwa ajili ya wafanyakazi wa media nchini kama ilivyokuwa hapo mwaka huu iliyojulikana kama Media Funny Day ambapo walivalishwa T-Shirt zenye nembo ya TBL. Hivi kweli tutafika kama hali yenyewe ndivyo ilivyo?
TBL kuna uozo mwingi sana lakini hakuna hatua zinazochukuliwa na serikali ama wadau wake... Serikali inayakumbatia maovi ya TBL kwa sababu shria ya uwekezaji nchini ina mapungufu mengi. Tunaomba msaada wenu Jamii Forum ili tujikomboe wazawa kwani serikali yetu imeshindwa kumlinda mwananchi wake.
Cheguemtz!