Disemba 9 kila mwaka: Tunasherehekea uhuru wa nchi ipi?

Tanganyika ilijifia wakati wa muungano 1964 na toka wakati huo hakuna nchi kama tanganyika in short ile sehemu ya nchini inayojulikana kama tanzania bara katika katika katiba ya sasa ilisurrender sovereignity yake na ndio maana hata kwenye katiba huwezi kukuta neno Tanganyika.

Mkuu,
Tukirudi kwenye kuungana, uhalisia tunajua kuwa Tanganyika na Zanzibar waliunaganisha baadhi ya mambo tu, siyo yote...Jee kulikuwa na umuhimu wa ku-surrender sovereignity yote? mbona Zanzibar waliendelea kushughulikia yale mambo yao ambayo amabyo hayakuwa ya muungano.
Nafikiri sababu ya Mambo ya Tanganyika kushughulikiwa na Bunge na serikali ya Muungano kwa sababu aliyoitoa Mwalimu ilikuwa ni kuepuka gharama ya kuwa na serikali tatu na hilo lilikuwa Rahisi kutendeka kwa sababu yeye ndiye aliyekuwa Rais wa Tanganyika na pia alikuwa Rais wa Muungano... na aliendelea kuwa hivyo mpaka alipoona mambo magumu, nchi inatokomea kwenye umasikini na ufukara, akaamua "kung'atuka". Lakini kila aliyehoji kasoro za Muungano katika utawala wake alionekana kuwa ni mhaini.

Hivi ni sheria ipi ilifuta nchi ya Tanganyika na nani aliidhinisha kifo hicho?
 
Baba%2BWa%2BTaifa%2BMwalimu%2BNyerere%2Bon%2BTanganyika%2BIndependent%2Bday.jpg

BABA WA TAIFA WA TANGANYIKA MWALIMU NYERERE ON TANGANYIKA INDEPENDENCE DAY 1961

The multi-racial first cabinet of newly independent Tanganyika on 1961
 
Mwaka 2011 ni miaka hamsini tangu uhuru wa Tanganyika ulipopatikana. Naomba niulize: Tutasheherekea kivipi? Uhuru wa Tanganyika au wa nji hii ya Tanzania ambayo inatimiza miaka 47?

Tumeambiwa tukae kimya bila kuhoji asili ya makubaliano ya muungano huu, ukiongea unaambiwa wewe ni mhaini. sasa wacha twende kama mikondoo.
 
Kumbe unasubiri siku wazanzibari waseme wanataka serekali moja.Utasubiri sana wala bado!Mie mzanzibari mmoja, count me in "SITAKI MUUNGANO NA TANGANYIKA".Huo ndio msimamo wangu, and I stand by it to death.Assuming I have seen alot in the past 50.

Miungano ninayounga mkono mie ni shirikisho tuu e.g EA, AU,EU etc.Lakini masuala ya kupoteza utaifa wangu...I am not ready and I dont think consciously I will ever come to a point and say forget about Zanzibar....Lets be Tanzania, ooops I forgot you think it is Tanzania already....Well, thats a fact I consider myself as a Zanzibari till today.

MrFroasty, We jiite hata Mchina who cares? ni haki yako ya msingi kujiamlia utaifa!! kama una feel Ok kuitwa Mzanzibar whats the problem? hamna matata, unaupenda au huupendi muungano that's you right as long as haumsumbui wala kumbughuthi mtu its OK. Just be happy and enjoy your life!
 
Tanganyika.je nchi hii ipo?(haipo)je tunasherekea uhuru wa nchi gani?(sijui) Tanzania haijawahi pata uhuru(kwa maana ilizaliwa baada ya nchi huru 2 kuungana)
 
Mwaka 2011 ni miaka hamsini tangu uhuru wa Tanganyika ulipopatikana. Naomba niulize: Tutasheherekea kivipi? Uhuru wa Tanganyika au wa nji hii ya Tanzania ambayo inatimiza miaka 47?

Usibate tabu fungua hapa kwanza number 1 TANGANYIKA INDEPENDENCE - British Pathe

Pia angalia hapa number 2 TANGANYIKA INDEPENDENT - British Pathe

Pia angalia hapa number tatu, ( TAGANYIKA ELECTIONS ) - British Pathe

sasa mimi sijui uhuru gani ambao hutumia kwa nija la tanzania,tanzia imepata uhuru mwaka gani ? Au ndo ile ile tanganyika kuitwa tanzania kuwafumba macho wazanzibari ? Ni sawa zaire kuita congo.

Kwa mujibu wa sheria na makubaliano ya muungano ilikuwa muungano ukijulika kama hivi .....jamuhuri ya muungano wa tanganyika na zanzibar.

Lakini wajanja wakaiyuwa tanganyika na kuita tanzania,kila pale palipokuwa na jina la tanganyika kukafutwa na kuitwa tanzania hadi nyerere akaijichanganya,pia wakachukua katiba ya tanganyika na kuchukua yale makubaliano ya muungano na kuyaingiza humo katika katiba moja,yamechanganyika hapa vipi ?

HAIWEZIKANI NCHI MOJA IFUTE UTAIFA WAKE,moja ibaki huu ni usaniii,tanzania sio nchii jamani ni muungano tu kama wa east africa mashariki ila wajanja hapa wametucheza.
 
wazalendo,,,,mulikuwa musipate tabu kujadili kulikuwa na video nimeweka hapa lakini wamezitoa hiii inaonyesha zahiri kabisa kuwa watanganyika wanapotoshwa na history ya kweli,kwani video hizo ukweli wote umo humo,hasara kwenu watanganyika.
 
Kuhsherekea miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika ni sawa sawa tu na kusherekea siku ya kuzaliwa ya mpendwa wako ambae hayupo tena duniani. Una sheherekea tu lakini umri wa huyo mtu hausogei tena. hausemi ana miaka mingapi una sema angakua na miaka fulani.
 
Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu umuhimu wa hii sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, wakati hata hilo jina la hiyo nchi linaogopwa kutajwa. Tanzania ina mika 47 tu haijafikisha miaka 50. Sasa kwanza tuelezwe vizuri, kama Tanganyika ilishakufa tuafanya maombolezo au tunasherehaka. Hii sherehe inabidi ifutwe tu. USA leo wakishehekea uhuru wao, hawazungumzii uhuru wa states. La basi Tannyika ijulikane kama state na siku hiyo ya sherehe iwe imetoka msukuleni. Sijui lakini, yaani sielewi kabisa.


Sasa bendera gani itakayopandishwa wakati wa sherehe, Tanganyika?
Wimbo gani wa miaka 50 utapigwa na kuimbwa?
Raisi gani atakaekuwa mgeni wa heshima? Tanganyika haina raisi
Mafanikio gani yatazungumzwa, tanganyika?

Na wewe unaesema ati tunachokoza muungano, ufikie kikomo sasa, kwanini zanzibar ina state na Tanganyika haina
Nani aliyeafiki?
Sisi wengine tulikuwepo, lakini hatukushirikishwa
Msituchukulie poa

Shere hiyo ifutwe, La siku hiyo state ya Tanganyika itambuliwe, na bendera yake , na wimbo wake wa Taifa.
Tanganyika = Tanzania? Dont fool anybody.

images
Je siku hiyo mtatupa ruksa ya kupeperusha vibendera vya Tanganyika, kwa majonzi?
 
BWana Sanga ukiwaza sana mambo ya wanasiasa unaweza kuumia kichwa. Mchungaji Mtikila huwa anaonekana kama chizi lakini vitu anavyosema huwa ni ukweli halisi.

Labda IKULU, ikupitia kurugenzi ya habari au Luhanjo anaweza kufafanua. Uhuru ulikua wa Tanganyika, ambayo kimsingi haipo kwa sababu iliacha kutambulika (ILIKUFA) miaka takribani miwili baada ya kuzaliwa.
Kumbuka miaka mitatu ijayo tutasherehekea tena miaka 50 ya uhuru (zanzibar-nafuu wao wapo na wanaendelea na sovereignity yao).
ILA KAMA WALIMUONA TUNDU LISSU KAMA MSALITI WAKATI AKIHOJI MUUNGANO BUNGENI, SASA NDO UMEFIKA WAKATI WAKE. Tutajua TANZANIA ni NINI na Nafasi ya Zanzibari ipo wapi. USHIRIKI WAO UTATUONESHA MANENO YA LISSU NA YALE YA WABUNGE WA ZANZIBARI YAPI YATASIMAMA
 
Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu umuhimu wa hii sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, wakati hata hilo jina la hiyo nchi linaogopwa kutajwa. Tanzania ina mika 47 tu haijafikisha miaka 50. Sasa kwanza tuelezwe vizuri, kama Tanganyika ilishakufa tuafanya maombolezo au tunasherehaka. Hii sherehe inabidi ifutwe tu. USA leo wakishehekea uhuru wao, hawazungumzii uhuru wa states. La basi Tannyika ijulikane kama state na siku hiyo ya sherehe iwe imetoka msukuleni. Sijui lakini, yaani sielewi kabisa.
kwa kweli ni kaobservation kazuri.
logically, hapa hakuna miaka 50 ya uhuu wa tanzania, labda miaka 47, au miaka 50 ya uhuru wa tanganyika.
 
Watu wakituambia ukweli kwamba muungano huu unahitaji kufanyiwa restructuring - wanakurupuka wengine eti mtaua muungano. Sasa jiulizeni watu mtakuwa mnasherekea miaka 50 ya nchi gani? Bendera gani?

Muungano huu ndiyo uliiua Tanganyika rasmi mwaka 64 na kuunda Jamhuri ya muungano wa Tanzania pamoja na serikali ya Zanzibar. Muungano wa nchi mbili unatengeneza nchi mbili mimi sijawahi kuona popote duniani.

Kama mnasema mnakumbuka miaka 50 ya uhuru basi lazima muikumbuke Tanganyika pia. kwa tafsiri yangu hakuna sherehe yoyote kama hutaitaja Tangayika, bendera ya Tanganyika na wimbo ambao ndiyo hasa uliimbwa siku ya uhuru wakati bendera ya mkoloni ikishuka tukipandisha yetu.

Wazanzibar ni wanjanja sababu hawajapoteza uraia wao, uhuru wao, jina la nchi yao na ndiyo maana wanatambia mapinduzi waliyopigana kuondoa utawala wa kisultani those years.

Tutaendelea kuwa na matatizo haya mpaka lini? tunataka Tanganyika yetu please!!!! --- Kuna tatizo gani kuwa na serikali 3? kama hamtaki 3 sababu ya uchu wa madaraka basi fanyeni iwe moja.

Nchi moja ina katiba 2, serikali 2, Marais 2, Mambunge mawili -- Kazi kweli kweli.
 
Tanganyika ilizaliwa 9th Dec, 1961. Baadaye ikaungana na Zanzibar kufanya muungano wa Tanzania. Serikali ya Tanganyika iliunganisha kwenye serikali ya muungano, kwa hiyo hapo tunasherekea Uhuru wa Tanganyika ambayo ni Tanzania vilevile. Tar 26.04.2014 tutasherekea Muungano wa Tanzania na wala siyo Uhuru wa Tanzania. Kwa kifupi Tanganyika ilipata jina la Tanzania, lakini umri unabaki palepale. Kuna Uhuru wa Tanzania na Muungano wa Tanzania.
 
Hapo hapo,je bendera ya Tanganyika ndiyo hiyo inayotumika kama ya Tanzania?Wimbo wa Tanganyika ndiyo unaotumika kama wimbo wa Tanzania ya sasa?Katiba ya Tanganyika iliwahi kuwepo maana Zanzibar walianza na presidential decree,je katiba hiyo inafaa?

WANA JF nakumbuka wakati ninasoma UDSM niliwahi ongea na kujadiri kitu kuhusu Tanganyika lkn ndugu zangu wanafunzi wengi waliniita mimi msaliti na mkabila mpaka wakarefer kabila langu. Sasa LISSU msishangae anapoambiwa maneno kama hayo.

Kiufupi Tanganyika ilikufa na hakuna watu wa Tanganyika labda Watanzania Bara, je hii ni sahihi? IKUMBUKWE TULISHANGILIA SANA KUZALIWA SOUTHERN SUDAN, LINAPOKUJA KWETU BASI TUNAONA TABU, POLITICAL HYPOCRACY.
 
Tanganyika ilizaliwa 9th Dec, 1961. Baadaye ikaungana na Zanzibar kufanya muungano wa Tanzania. Serikali ya Tanganyika iliunganisha kwenye serikali ya muungano, kwa hiyo hapo tunasherekea Uhuru wa Tanganyika ambayo ni Tanzania vilevile. Tar 26.04.2014 tutasherekea Muungano wa Tanzania na wala siyo Uhuru wa Tanzania. Kwa kifupi Tanganyika ilipata jina la Tanzania, lakini umri unabaki palepale. Kuna Uhuru wa Tanzania na Muungano wa Tanzania.
Serikali ya Zanzibar yenyewe haikuunganishwa kwenye muungano? mbona ipo separate na ina viongozi wake na katiba yake?
 
Haya ni mambo ya kisiasa sana,
ukitaka kutumia akili sana ndio unapasua kichwa,
kwenye siasa kila kitu kinawezekana kwa kulazimisha au la,
Tanzania miaka 50 tangu Uhuru,
kwa akili ya kawaida hakuna kitu kama hicho lakini kwa akili za kisiasa ndio inasheherekewa hivyo nchi nzima
 
Nimekuwa nikijiuliza sana kuhusu umuhimu wa hii sherehe ya miaka 50 ya uhuru wa Tanganyika, wakati hata hilo jina la hiyo nchi linaogopwa kutajwa. Tanzania ina mika 47 tu haijafikisha miaka 50. Sasa kwanza tuelezwe vizuri, kama Tanganyika ilishakufa tuafanya maombolezo au tunasherehaka. Hii sherehe inabidi ifutwe tu. USA leo wakishehekea uhuru wao, hawazungumzii uhuru wa states. La basi Tannyika ijulikane kama state na siku hiyo ya sherehe iwe imetoka msukuleni. Sijui lakini, yaani sielewi kabisa.

Una hoja ya msingi, lakini simpo mathematics ukihesabu miaka hamsini kufikia Desemba 9, 2011 unajua ni nchi gani inazungumzwa. Tusichokoze Muungano.
 
Wananchi si tumeshazoeshwa kupelekwa pelekwa tu bila hata kuwa na haja ya kuhoji kwanini jambo hili liko hivi na sio vile au kwanini huyo ana hiki na huyu hana??!! basi ndo tumeshachelewa wameshatuwahi haoooo wanaotuamulia (hata kama ni pumba) nini cha kufanya, nini cha kuhoji, nini uulize na staili gani ya maishi tuishi!!
 
Back
Top Bottom