Dira ya Maendeleo ya Taifa 2025 (Tanzania Development Vision 2025)...

Sisi watanzania tuna elimu ya viwango tofauti lakni kuwepo kwa elimu hiyo hatuna elimu ya utawala bora. Leo hii ukiwaambia wananchi wenye shida ya maji, umeme na miundo mbinu wamuulize kiongozi wao maswali, hakika wengi watatoa pongezi.

Mgombea akisimama jukwaani anajinadi nitawajengea barabara, maji nitawaletea na umeme mtapata. Hakuna wa kumuuliza utafanya hayo yote kwa pesa yako au ya wananchi? Hakuna wa kumuuliza kuwa atatumia mbinu gani kupunguza ukali wa maisha japo kidogo, tunatoa kodi kubwa je, inamalengo yapi kwa taifa?
Ukishakuja kwenye suala la utawala bora,kwakweli hata hao viongoz hawajui,wao wanasema utawala bora ni uwazi na utawala wa sheria,hawataji principles nyingine za utawala bora,na bahat mbaya miongoni mwa wananchi ndo hatujui kabisaa UTAWALA BORA,wananchi wanautamani 2015 kwa kuneemeka na fulana,pilau na pombe,
 
Yeye asema tutaipeleka Tanzania kuwa nchi ya kipato cha kati 2015-2025.
Naibu waziri wa fedha aliyetokea kugusa mioyo ya watanzania masikini na kufufua matumaini yao ndg Mwigulu Nchemba juzi alikonga nyoyo za wananchi wa Tabora waliofurika Igunga kumsikiliza. Mwigulu aliyekuwa akishangiliwa kila alipofafanua hoja aliwaacha wanaigunga wakibaki makundi makundi mpaka giza lilipoingia wangali viwanja vya Sokoine kutafakari hotuba yake iliyokuwa na sura ya kiongozi wa taifa.

Katika hotuba yake mwigulu alirudiarudia neno "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI IFIKAPO 2025" na kushangiliwa kwa kishindo.

Mwigulu alibainisha kuwa mambo ya msingi kufikia hatua hiyo kuwa ni

1) Maadili na uzalendo wa wasimamizi wa rasilimali za taifa. Mwigulu alisema wanahakikisha kwamba kila fedha inakwenda kutoa huduma iliyokusudiwa, tunahakikisha kodi za wananchi zinakwenda zilipokusudiwa. Tukikusanya fedha kwa ajili ya umeme, tunasimamia iende kwenye umeme, tukikusanya fedha ya barabara tunahakikisha zinakwenda kwenye barabara, hivyohivyo kwenye Afya, elimu nk. Mwaka jana tumegundua tulitoa zaidi ya 48bil kwa ajili ya dawa mawilayan lakkni ni 7bil zilitumika kununua dawa huku kila mgonjwa akienda hospital anahundulika na homa na kuambiwa kanunue dawa kiosk kile, huu ni wizi, kiosk kinatoa wapi dawa ambazo serikali haiwezi kupata kama sio kufanyia biashara dawa zilizonunuliwa kwa kodi za watanzania. Naagiza hili likome na hatua zitachukuliwa, madiwan na vyombo vya dola simamien hili. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

2) Kuachana na kufanya kazi kwa mazoea.

Mabadiliko ni vitendo na yanaonekana kwa kubadili style ya kufanya kazi ili kulinda fedha za umma. Timebadili ulipaji wa mishahara kipambana na mishahara hewa. Tumebaini zaidi ya wafanyakazi elfu kumi na nne (14,000) walioyeyuka tjlipoomba akaunt zao na 1,900 wa keshi nao wameondolewa kwenye malipo. Tumeokoa zaidi ya bilion 40. Naagiza maofisa wote wahakiki watimishi waliopo kazini na walete akaunt. Tukibaini makosa yule aliezembea atafute kazi ya kufanya na hatua zitachukuliwa. Mpk sasa waliozembea tumewapeleka polisi na TAKUKURU wafikishwe mahakamani.

Tumekagua madai tukagundua udanganyifu, kwenye bilion 500 tumegundua halali ni bilion m100 tu, tumeokoa bilion 400 na tumewapeleka polisi wote waliodanganya. Naagiza wakaguzi watimize wajibu wao kabla ya kuleta madai wizani kwangu. Wakileta tutskagua, Tukigundua udanganyifu aliyeleta hiyo atafute kazi nyingine ya kufanya na tutamburuza mahakamani. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

3) Tutapunguza pengo kati ya walionacho na wasionacho kwa kutekeleza vyema sera za kodi.

Tutawatoza kodi matajiri ili fedha hizo tuwasomeshe watoto wa masikini. Tutatoza kodi matajiri ili fedha hizo tupeleke huduma za maji, madawa, umeme na barabara vijijini. Hatuwezi kuwasamehe kodi matajiri mabilioni ya shilingi, wakwepe mabilioni ya shilingi halafu sisi tukimbizane na wajane wanauza matembere kulipa ada elfu 20 mashuleni. Tumefuta misamaha kwa matajiri tuache kuwssumbua wajane na masikini kutafuta elfu 20 za sekondari. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

4) Tutasimamia mgawanyo wa rasilimali ili keki ya Taifa iwanufaishe watanzania wote kwa usawa.

Tumebana matumizi ya serikali yasio ya lazima ili fedha hizo ziende kwenye miradi ya maendeleo. Tutahakiki bajeti za kila taasisi ya umma na kufuta matumizi ya anasa. Hatuwezi kuwa na shirika la umma linatumia fedha kwa anasa huku watoto wakikaa chini. Kupewa kuvuna rasilimali za umma ni dhamana tu sio shamba binafsi na mashirika na taasisi zote za umma mnaokusanya fedha tokea rasilimali za Taifa mlielewe hili. Hatuwezi kuwa na watanzania hapa wanaishi tanzania na wengine wakiishi kama ulaya wakiwa hapahapa kisa wamepewa dhamana ya kusimamia shirika la umma. "TUTAIPELEKA TANZANIA KUWA NCHI YA KIPATO CHA KATI"

5) Tutatoza kodi kwa matajiri, tuwapinguzie kodi walimu na wafanyakazi wengine, tutatoza kodi tuziwezeshe sekta zinazotoa maisha kwa watanzania wengi ili KUONDOA UHUSIANO WA KUKUA KWA UCHUMI HUKU UMASIKINI NAO UKIKUA.

Tukiwedha fedha kwenye sekta zinazolisha na kuendesha maisha ya watu wengi tutakuza uchumi huku umasikini wa watu wa chini ukipungua.

6) Kuna watu walinunua viwanda vyetu, wamelipa, wamewekeza, wameendeleza, wametengeneza ajira, wameheshimu mikataba, wanalipa kodi nawapongeza sana. Lakini nimeangalia kumbukumbu kwenye mafaili kuna watu walinunua viwanda, hawajawekeza, hawajaviendeleza, wamegeuza viwanda kuwa magodauni, wameuza vyuma chakavu, wamepeperusha ajira, wameua mazao ya wakulima kwa kuua viwanda vya nguo, wameua mazao ya mifugo kwa kuua viwanda vya ngozi, viatu, hawajaheshimu mikataba, hawajalipa serikalini, wametajirika kwa kuchukua mali ya umma. Nawambia wakaangalie upya mikataba inasemaje, vinginevyo wajiandae kisaikolojia.Video inakuji soon

Umepewa sh ngapi ili kumpigia debe huyo savimbi?
 
Nchi hii inasheria lakni inaongozwa kisiasa siasa, mfano fundi ujenzi umpe tenda ya kukujengea nyumba vifaa vyote umpe halafu mwisho wa siku fundi auze simenti yote, na wewe umwambie fundi nimekusamehe endelea na ujenzi unadhani atajenga vipi bila simenti.

"Tumewasamehe misamaha ya kodi" kesho utasikia taifa linadaiwa mabilioni, sasa mnataka azilipe nani?.

Umesahau wezi wa Epa walivyosamehewa na kuamlishwa warudishe fedha walizo iba?
 
Barabara, maji, umeme na vinginevyo ni kodi za wananchi sio hela ya mtu mmoja au chama. Kinachofanya watu waongee ni usimamizi na matumizi ya kodi zetu, unatoa kwa masikini unapeleka kwa matajili. Wamepandisha bei ya umeme ikawa haitoshi wakaongeza service charge ya umeme na maji. Hapo naona hajatatua tatizo bali ameongeza.

Mkulima anaandaa shamba tangu mwanzo,anapalilia,akisha vuna mazao yake ndio wanakuja na ngonjera ya stakabadhi gharani,wizi mtupu!
 
Mtoto wa mfugaji kaimu Waziri wa fedha mh Mwigulu Nchemba sasa anaenda kuitoa nchi kutoka katika hali ya sasa kuelekea katika nchi ya kipato cha kati na hili amelidhihirisha wakati akiongoza mafunzo ya takwimu jana trh 18/sept mjini Morogoro
Ambapo alichukuwa nafasi hiyo kusisitiza ufuatiliaji wa hali ya Umasikini katika kaya kwa Vitendo na na kuacha hadithi kwenye utendaji wa kumkomboa Mtanzania katika lindi la umasikini, na kuongeza kuwa Uhimalishaji wa ofisi za TAKWIMU ni muhimu ili serikali iweze kuwa na mipango ya maendeleo ambayo ni linganifu na Takwimu zilizopo wakati ambao Serikali inafunga mkanda kwa ajili ya kuwa nchi ya kipato cha kati, ni lazima tuwe na takwimu bora na sahihi alisema Mwigulu Nchemba. Pamoja na mambo mengine mh Mwigulu Nchemba ambaye anafananishwa na Sokoine kwa utendaji wake wa kazi alichukua nafasi hiyo kuipongeza ofisi ya TAKWIMU kwa namna inavyoendelea kufanya kazi na kusaidia wadau mbali mbali na kuendelea kuchangia shughuli za maendeleo na kuwaomba wananchi kutoa taarifa sahihi wanapofanyiwa udadisi ili zisaidie kupanga mikakati ya maendeleo. Na kuhitimisha kuwa ili katika Usimamizi wa Kodi na Matumizi yake ni lazima Takwimu ziwiane na kipato na kule fedha zinakoelekea, ili kuondoa gap kati ya walionacho na wasionacho ni muhimu kuwepo na takwimu sahihi.
 
Alikuwepo wapi miaka tisa yote iliyopita ? Wakati ufalme wa CCM umebakiza mwaka mmoja kuangushwa ?
 
Mtoto wa mfugaji kaimu Waziri wa fedha mh Mwigulu Nchemba sasa anaenda kuitoa nchi kutoka katika hali ya sasa kuelekea katika nchi ya kipato cha kati na hili amelidhihirisha wakati akiongoza mafunzo ya takwimu jana trh 18/sept mjini Morogoro
Ambapo alichukuwa nafasi hiyo kusisitiza ufuatiliaji wa hali ya Umasikini katika kaya kwa Vitendo na na kuacha hadithi kwenye utendaji wa kumkomboa Mtanzania katika lindi la umasikini, na kuongeza kuwa Uhimalishaji wa ofisi za TAKWIMU ni muhimu ili serikali iweze kuwa na mipango ya maendeleo ambayo ni linganifu na Takwimu zilizopo wakati ambao Serikali inafunga mkanda kwa ajili ya kuwa nchi ya kipato cha kati, ni lazima tuwe na takwimu bora na sahihi alisema Mwigulu Nchemba. Pamoja na mambo mengine mh Mwigulu Nchemba ambaye anafananishwa na Sokoine kwa utendaji wake wa kazi alichukua nafasi hiyo kuipongeza ofisi ya TAKWIMU kwa namna inavyoendelea kufanya kazi na kusaidia wadau mbali mbali na kuendelea kuchangia shughuli za maendeleo na kuwaomba wananchi kutoa taarifa sahihi wanapofanyiwa udadisi ili zisaidie kupanga mikakati ya maendeleo. Na kuhitimisha kuwa ili katika Usimamizi wa Kodi na Matumizi yake ni lazima Takwimu ziwiane na kipato na kule fedha zinakoelekea, ili kuondoa gap kati ya walionacho na wasionacho ni muhimu kuwepo na takwimu sahihi.
"Mwigulu Nchemba sasa anaenda kuitoa nchi kutoka katika hali ya sasa kuelekea katika nchi ya kipato cha kati"!!!!!?????? Really?

Ungeripoti tukio ukatuachia nafasi wasomaji wako watoe tathmini...


Au amekutuma umpigie propaganda?
 
Alikuwepo wapi miaka tisa yote iliyopita ? Wakati ufalme wa CCM umebakiza mwaka mmoja kuangushwa ?

Alikuwa katibu wa uchumi na fedha wa chama baadaye naibu katibu mkuu wa chama bara sasa ndiyo naibu waziri wa fedha tanzania,nadhani umeelewa.
 
Maendeleo haya husemwa kabla ya uchaguzi ukipita tu wanatangaza mpango mpya wa kurudisha pesa walizotumia katika uchaguzi hasa kuhonga....ndoto za mchana nchi yangu kupata maendeleo chini ya CCM..Haiwezekani
 
mwigulu chapa kazi usiangalie pembeni watanzania wanaheshimu kazi yako.
 
Waliitoa wapi 2005 na sasa wamefikisha wapi... kuelekea 2025?
Au walikuwa hawajaanza mwendo?
 
Wanasiasa ni majanga matupu waliomba wapewe kura,wawaletee maisha bora watanzania ndani ya miaka5,miaka 5 ikapita hakuna cha maisha bora kwa kila mtanzania hata mimba ya maisha bora haikuonekana,wakaomba waongezewe kipindi kingine cha miaka 5 ambacho kiko ukingoni napo hamna kitu.Walichofanikiwa zaidi ni kulitoa Taifa kwenye unafuu wa madeni na kuwa kinara wa madeni.Sasa wamekuja na kali zaidi ya kulifanya taifa kuwa lenye kipato cha kati tena siyo leo mwaka 2015 sijui nani atakuwepo kipindi hicho.
 
Maendeleo haya husemwa kabla ya uchaguzi ukipita tu wanatangaza mpango mpya wa kurudisha pesa walizotumia katika uchaguzi hasa kuhonga....ndoto za mchana nchi yangu kupata maendeleo chini ya CCM..Haiwezekani

Km mpaka hapa uoni kazi ya chama cha mapinduzi hakika na wewe utakuwa miongoni mwa wale ambao kazi yao kubwa ni kubeza.
 
Tutasikia uongo wa kila aina kuelekea 2015, miaka 53 na utajiri wa kumwaga hamjaweza kufanya lolote la maana katika kuinua viwango vya maisha ya W atanzania walio wengi, sasa mnadai kwa hii miaka 11 hadi kufikia 2025 ndio mtafanya maajabu!!!! Tumechoka na uongo wenu wa miaka nenda miaka rudi huku mkiendelea kuiangamiza Tanzania.

 
Tutasikia uongo wa kila aina kuelekea 2015, miaka 53 na utajiri wa kumwaga hamjaweza kufanya lolote la maana katika kuinua viwango vya maisha ya W atanzania walio wengi, sasa mnadai kwa hii miaka 11 hadi kufikia 2025 ndio mtafanya maajabu!!!! Tumechoka na uongo wenu wa miaka nenda miaka rudi huku mkiendelea kuiangamiza Tanzania.


Tutoe taarifa sahihi ili vipaombele vya serikali viwe revealed
 
Back
Top Bottom