Dark City
JF-Expert Member
- Oct 18, 2008
- 16,253
- 11,598
Kihirizi?
Misukule
Kihirizi?
Babu DC huwezi ukawa na perfect partneship na mtu ambae sio perfect kwaajili yako. Sema tatizo ni kwamba watu wanatumia vigezo ambavyo sivyo kujidanganya kwamba huyu ndie anaefaa kwaajili yangu.
Kihirizi?
Astaghafirullah....mstaafu Dark City upo wapi kaka?
...wakati tunafunga mwaka 2011, tuliazimia mwaka 2012 uwe ni mwaka wa kuokoa na kudumisha ndoa, full stop!
MwanajamiiOne maneno gani tena haya unayaleta january hii, ewe soulmate?
Lizzy, hakuna mtu perfect 100% bana...
mimi hilki neno perfect linanikera...
hebu nipe vigezo vya ukweli vya huo u perfect(achilia yule gentleman uliyemuanzishia thread labda kwa kumsoma tu mtandaoni..)
kabla hatujaendelea na huh mdahalo wa mwj1...
Mimi binafsi sijawahi kuwa kwenye relationship na imperfect partner bana...hebu nikosoe uelewa wangu.
Kwahiyo watu wanatakiwa walazimishe?
Lizzzy,
Tunaongelea mitazomo miwili tofauti kabisa ambayo naamini huwezi kunielewa,
Let me say this...
Siku moja, baba na mama yetu alikuwa wanataniana baada ya kumuona mwanamume mmoja mchafu mchafu amepita mbele yao (bahati mbaya nilikuwa karibu nao ingawa hawakujua)!!...Wakawa wanakumbushana kuwa yule mwanamume alikaribia kabisa kumuoa mama yetu, kwa kuwa wazazi wake walienda kwa babu yetu na kuomba kutoa posa. Hata hivyo baba yangu ndiye akapewa mke....Kwa jinsi yule baba alivyoonekana hopeless, niliumia sana na kusikitika kama ingetokea akawa baba yangu....!!
Does this kind of thing make sense with you???
Babu DC
...lol....mwj1, i take back my words, samahani soulmate, nisamehe, nimekosea...
haikuwa nia yangu kutoutendea haki huu mdahalo.
...na tuendelee...
MJ1,
Unajua nini,..... kila anayefuga misukule, huamini kuwa haiweza kuamka hata siku moja...Ndiyo maana msukule ukiamka lazima mmiliki abaki kinywa wazi!!
Babu DC!!
Soulmate jamani, wapi nimevunja? hapa nacheza na Preventive Measures. Badala ya kudeal na healing najaribu kuzuia kabisa pains!
Ukimheshimu, thamini, penda penzi litadumu.
Soulmate jamani, wapi nimevunja? hapa nacheza na Preventive Measures. Badala ya kudeal na healing najaribu kuzuia kabisa pains!
Ukimheshimu, thamini, penda penzi litadumu.
Aksante Babu kwa kuwa mstari linear nami. Imagine, Darl nilikupenda, ninakupenda bado ila mambo yako nimeshindwa mimi, hebu nisiwe mchoyo na mbinafsi niwaachie na wengine wajaribu.....anang'aka na kushangaa. as if alipokuwa anafanya madudu hakuwahi kuhisi kuwa iko siku utaufunga mlango wa moyo na kuutupa ufunguo baharini. !!!
Tatizo la vijana wa dot com ni kutafuta perfect partners kwa kutumia vigezo vya kufikirika!!
Umm sindo maana ya kuchagua hapo ama? Yani alichaguliwa yule aliyeonekana anamfaa zaidi bila kujali nani alitanguliza mahari.
Nadhani tunachoongelea ni kitu kimoja isipokua kwa namna tofauti.
Tena sasa hivi wameandaa na checklist
kuna kama vitu 27 vya kucheck
Should be
1. Inteligent
2. Exposed
3. Educated
4. Loaded
5. Smart
7. Presentable
8. Artist in bed
9. Civilised
10. Stylist
11. Fashionist
12. Faithfull
13. Humanitarian(marfuku kofi)
14. Vegetarian unless timetable imekuruhusu(wikiend mchana, siku nyingine kachoka)
15. Helper at home
16. Mfungua mlango
17. Mtengeneza kiti, hasa mkiwa out
18.Lover, admirer wake
19. Plumber
20. Electrician
21. Kubeba mizigo yote mkitoka shopping
22. Garderner
23. Listener
24. mute, no argument hata kama unaibiwa
25. Companion
26. friend
27. Confidant
na bado revised version ya 2012
Mbu sijaongelea mtu ambae ni perfect kwenye macho ya watu, bali naongelea mtu ambae ni perfect FOR (NOT TO) a certain person. Kwamba mnaendana, unayokosa wewe anaongezea yeye na mwisho mnapata picha inayoangalika.
Alafu Gentleman is so NOT perfect, he has his flaws just like the rest of us. Sema tu mapungufu yake hayo binafsi naweza kuyakubali na kukabiliana nayo kuliko ya watu wengine wengi. Kwahiyo mtu wa aina yake ni perfect kwaajili yangu na sio kwangu.
Babu basi tu mnapenda kufikiria wana dot com wote hatufikirii mambo kiundani. Kuendana ndio chanzo cha uimara wa mahusiano yoyote yale, na kuendana huko kwaweza hata kuwa "kumpata mwanaume anarudi nyumbani saa mbili badala ya saa kumi na moja right after work, au ambae ni mkali kidogo" tofauti na ambavyo watu wanaweza wakawa wanadai wanataka iwe.Hongea (Ahsante) sana Lizzy kama tinaelewana....
Unajua watu tunafikiria kwa kutumia kamusi ya 1947 (kutoka Oxford University Press) ni tofauti sana nyie mnaotumia online dictionary!!
Babu DC!!
mnh, kwa ajili yako, sio kwako!...?
anyway, acha nielewe nielewavyo mie na hii akili ya uzee...
Kwenye haya mahusiano, kuna mambo (kutokana na malezi/makuzi) naya identify toka kwa mwenzangu kuwa ni kero/mapungufu...
Wakati huo huo, kutokana na expewriences naamini na yeye kuna anayoyatambua kumkera kuhusu mimi/mapungufu yangu...
...[being perfect partners kwa mtazamo wangu] ni jinsi ninavyoweza kuyavumilia hayo mapungufu kwenye maisha yetu, na yeye anavyoweza kuyavumilia yangu...
Muhimu kutambua tuna tofauti ya mitazamo, na hilo wala sio jambo la ajabu kiasi litufanye litugombanishe,
muhimu...heshima mbele!
Babu basi tu mnapenda kufikiria wana dot com wote hatufikirii mambo kiundani. Kuendana ndio chanzo cha uimara wa mahusiano yoyote yale, na kuendana huko kwaweza hata kuwa "kumpata mwanaume anarudi nyumbani saa mbili badala ya saa kumi na moja right after work, au ambae ni mkali kidogo" tofauti na ambavyo watu wanaweza wakawa wanadai wanataka iwe.
Umenielewa Mbu. . .
Ishu sio yeye kutokua na mapungufu bali ni wewe kuweza kuhimili mapungufu yake na kuwa tayari kuyakubali.
Kwahiyo mtu anaetolerate cheating anaweza akapata Mr. Right wake anaemfaa yeye japo anacheat kwasababu anaweza kumvumilia, wakati mimi nisieweza/taka kutolerate cheating hanifai hata kama amekamilika kiasi gani ukitoa hiyo tabia ya kucheat. Ndio maana nikasema kila mtu yupo anaemfaa yeye na sio mwingine. Ingekua kila mtu anamfaa kila mtu kusingekuwa na misukosuko ya kila aina kwenye mahusiano. Wote tungevumiliana maisha yakaenda.
Nazungumzia wale wapenzi wenye kuwafanyia wenzi wenu visa mfano : Kupiga, kuabuse, dharau, jeuri, dharau, cheating e.t.c kiasi kwamba mwenzi anaona sasa basi, Yatosha, I'm OUT. Then unaanza kushangaa what went wrong?? Didn't you see it coming?