Ochu
JF-Expert Member
- May 13, 2008
- 975
- 47
- Thread starter
- #21
Dida alikamatwa majuzi (Jumatatu) na wanausalama wa Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere, akidaiwa kumeza dawa za kulevya, tayari kuzipeleka sokoni nchini China.
Akipiga stori na gazeti hili, Dida ambaye kwa sasa yupo nje kwa dhamana alisema kuwa, tukio la kukamatwa kwake ni njama za mwanamke aliyemtaja (jina tunalihifadhi) ambaye alikuwa na ugomvi naye siku nyingi zilizopita hadi kufikia hatua ya kufikishana polisi.
Kila kitu nakijua. Hizo ni njama za kunimaliza, lakini naamini kwa uwezo wa Mungu nitashinda, alisema Dida na kuongeza:
Tuliwahi kugombana naye (jina tunalihifadhi) hadi kufikia hatua ya kunipeleka polisi na kunifanyia mambo ya kifedhuli sana, kisa alidai eti mimi namchukulia mume wake ambapo tulikuwa marafiki wa kushibana.
Hata hivyo, Dida alisema kuwa, alishangaa kuona anashikwa mkono na mtu asiye mfahamu Uwanja wa Ndege na kuambiwa kuwa, yuko chini ya ulinzi kwa kufanyiwa upekuzi wa kina kwa tuhuma za kuwa na dawa za kulevya.
Ni kweli nilikuwa chini ya ulinzi, najua ni mbinu za watu wasiyopenda maendeleo yangu wanabaki kila kukicha wananitafutia matatizo kinguvu ili yanikute, na ni juhudi zangu za maisha ndizo zinazonifanya niwe na maadui wengi, alisema Dida.
Aliendelea kusema kuwa, siku hiyo ya tukio baada ya kuachiwa huru, alipata habari kuwa, kuna mtu alipiga simu kwenye kituo hicho cha
Ndege akitoa taarifa kuwa, Dida anasafiri siku hiyo na achunguzwe kwa makini kwani huwa anakwenda China kwa ajili ya kupeleka dawa za kulevya.
Eti nichunguzwe kwa makini kwa sababu huwa nasafirisha dawa za kulevya kwa kumeza. Mtu huyo alijifanya ananijua vizuri mimi,alisema Dida.
Kwa mujibu wa habari hizo, uchunguzi wa awali aliofanyiwa mrusha sauti huyo kwa kutumia haja kubwa ulionesha hakuwa na dalili za mihadarati tumboni.
Hata hivyo, Dida yuko nje kwa dhamana uchunguzi zaidi ukiendelea na huku akiwa amekatishwa safari yake ya nchini China.
the saga continues
Akipiga stori na gazeti hili, Dida ambaye kwa sasa yupo nje kwa dhamana alisema kuwa, tukio la kukamatwa kwake ni njama za mwanamke aliyemtaja (jina tunalihifadhi) ambaye alikuwa na ugomvi naye siku nyingi zilizopita hadi kufikia hatua ya kufikishana polisi.
Kila kitu nakijua. Hizo ni njama za kunimaliza, lakini naamini kwa uwezo wa Mungu nitashinda, alisema Dida na kuongeza:
Tuliwahi kugombana naye (jina tunalihifadhi) hadi kufikia hatua ya kunipeleka polisi na kunifanyia mambo ya kifedhuli sana, kisa alidai eti mimi namchukulia mume wake ambapo tulikuwa marafiki wa kushibana.
Hata hivyo, Dida alisema kuwa, alishangaa kuona anashikwa mkono na mtu asiye mfahamu Uwanja wa Ndege na kuambiwa kuwa, yuko chini ya ulinzi kwa kufanyiwa upekuzi wa kina kwa tuhuma za kuwa na dawa za kulevya.
Ni kweli nilikuwa chini ya ulinzi, najua ni mbinu za watu wasiyopenda maendeleo yangu wanabaki kila kukicha wananitafutia matatizo kinguvu ili yanikute, na ni juhudi zangu za maisha ndizo zinazonifanya niwe na maadui wengi, alisema Dida.
Aliendelea kusema kuwa, siku hiyo ya tukio baada ya kuachiwa huru, alipata habari kuwa, kuna mtu alipiga simu kwenye kituo hicho cha
Ndege akitoa taarifa kuwa, Dida anasafiri siku hiyo na achunguzwe kwa makini kwani huwa anakwenda China kwa ajili ya kupeleka dawa za kulevya.
Eti nichunguzwe kwa makini kwa sababu huwa nasafirisha dawa za kulevya kwa kumeza. Mtu huyo alijifanya ananijua vizuri mimi,alisema Dida.
Kwa mujibu wa habari hizo, uchunguzi wa awali aliofanyiwa mrusha sauti huyo kwa kutumia haja kubwa ulionesha hakuwa na dalili za mihadarati tumboni.
Hata hivyo, Dida yuko nje kwa dhamana uchunguzi zaidi ukiendelea na huku akiwa amekatishwa safari yake ya nchini China.
the saga continues