Leak
JF-Expert Member
- Feb 22, 2012
- 52,205
- 42,066
"DIAMOND YA FOREVER" ndio jina la show babukubwa inayo andaliwa na msanii wa bongo fleva Diamond platinum,itakayofanyika Mlimani city hiv karibuni kwa kiingilio cha Tsh 50,000.Ni hatua kubwa sana kwa wasanii wetu wa kibongo kuweza kuanda ma concert yanayolipa kuliko shoo za nyanya zenye wasanii kibao na malipo kidogo. concert inapendeza sana kwa wasanii wenye uwezo wa kulishambulia jukwaa ipasavyo! sina shaka na Diamond akiwa jukwaani na ndio maana ameweza kuandaa shoo ya pekeyake kuonesha uwezo wake.Tumezoea kuona shoo za wasanii kumi ,lakn hii ni yapekee na nimeikubali. bila shaka itakuwa mwanana pia changa moto kwa wasanii wengine kujifunza kuburudisha mashabiki wao.