huyo diamond analipwa kiasi gani kwenda huko arusha...huyu diamond ana dili gani na jk/serikali? maana issues za chama/serikali anaitwaga yeye...mbona a town wana wanamuziki wengi tu kwanini wasiwatumie wao?
kwani kwenye huo uchaguzi wa daraja2 JK ndio aliekuwa anagombea? ushaur kwa JK apeleke wana hiphop watajaa.na mwana hiphop hawez kuwa CCM HATA siku moja.
Asije akaleta hii maneno kwa machalii wa R...
Mie huwa napata wasi wasi sana na akili za watanzania na hasa watu wa arusha, kitu anacho kuja kufanya JK ni kwa faida yenu na vizazi vyenu, kumsusia mtu kuna maana gani sasa? hebu watanzania tupevuke akili zetu , kwani kwenye masuala ya maendeleo huwa hakuna uhasama. Na isitoshe hao mnao wakumbatia hawajawafanyia chochote na mwisho wa siku mnarudi kwa JK kumpigia magoti awafanyie hayo myatakayo
Uongozi wa mkoa wa Arusha umelazimika kumleta Bongo Fleva, Diamond ili asaidie kukusanya watu wakati Rais Kikwete atakapohutubia umma wa mji wa Arusha siku ya alhamisi mchana.
Kikwete atazindua rasmi jiji la Arusha siku hiyo.
Vyanzo vya ndani vimebainisha kuwa jitihada za viongozi kuhamasisha mahudhurio zimekuwa zikigonga mwamba katika ngazi za kata kwani watu wengi wamekuwa wakisema wazi kuwa hawatakwenda Stadium!
Diamond ambaye ni kipenzi cha wanawake wengi hususan mabinti wa shule atasaidiana na za komedi kujaza uwanja kabla ya hotuba.
Wakati huo huo wasanii wa Arusha wameandamana hadi ofisi za meya wa jiji kupinga kuenguliwa kwenye tamasha hilo huku uongozi ukiwakumbatia ma bongo fleva wa Dar.