tunduruboy
JF-Expert Member
- Mar 16, 2013
- 423
- 218
MWENYEKITI wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Mwanza, Dk Antony Diallo, amesema anatamani rais wa awamu tano awe dikteta, lakini anayepatikana kwa njia ya kura ili awatie adabu Watanzania.
Dk Diallo aliyasema hayo wakati akizungumza na watendaji wa ngazi za juu wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, katika kikao alichokiitisha kwa ajili ya kubadilishana mawazo ya namna ya kuboresha shughuli za jiji la Mwanza.
Mwenyekiti huyo wa CCM, alisema kuwa hivi sasa taifa linakabiliwa na tatizo la wananchi, hasa wanasiasa la kutotii sheria na kujiamulia mambo kiholela na hivyo kuleta hofu kwa wananchi.
"Ninatamani sana rais ajaye wa awamu ya tano awe dikiteta, lakini ambaye atakuwa amechaguliwa kwa kura na wananchi, ili aje atutie adabu, kwani taifa liko katika hali mbaya, kila mmoja ni mjuaji na yote haya yamekuwa yakisababisha uvunjifu wa amani," alisema Dk Diallo.
"Watanzania ni waoga sana, wakisikia mlio wa bunduki wengi watakimbilia uvunguni mwa kitanda, tunataka Rais ajaye awe dikteta ili ainyooshe nchi hii, kwani imefikia katika hali mbaya, kuna watu wanaichezea amani yetu na ni mabingwa wa kuhamasisha vurugu na wanazungumza mambo wasiyoyajua," alisema Dk. Diallo, ambaye pia amewahi kuwa Naibu Waziri na Wizara katika serikali za awamu ya tatu na nne.
Mwenyekiti huyo pia alisema kuwa sheria za nchi pia zinapaswa zitazamwe upya katika kuilinda nchi hii kuepuka kupata viongozi wasiofaa na kuitaka Idara ya Usalama wa Taifa kuhakikisha inaisaidia serikali katika kupata viongozi bora na wasio na kasoro.
Alisema kuna baadhi ya maeneo baadhi ya watu wamejipenyeza kugombea uongozi na kushinda, huku wakiwa si watu safi, hali ambayo inaiyumbisha nchi.
"Kuna baadhi ya wabunge na madiwani ni X Criminals, ni wahalifu sugu wamefanikiwa kushika nafasi hizo, hapa unatarajia nini na kuna kiongozi mmoja hivi sasa ni kiongozi wa chama cha siasa katika ngazi ya wilaya huyu siyo Mtanzania, tatizo hapa katika siku za karibuni vyombo vyetu vimelegalega," alisema Dk Diallo.
Chanzo: Mtanzania
Dk Diallo aliyasema hayo wakati akizungumza na watendaji wa ngazi za juu wa Halmashauri ya Jiji la Mwanza, katika kikao alichokiitisha kwa ajili ya kubadilishana mawazo ya namna ya kuboresha shughuli za jiji la Mwanza.
Mwenyekiti huyo wa CCM, alisema kuwa hivi sasa taifa linakabiliwa na tatizo la wananchi, hasa wanasiasa la kutotii sheria na kujiamulia mambo kiholela na hivyo kuleta hofu kwa wananchi.
"Ninatamani sana rais ajaye wa awamu ya tano awe dikiteta, lakini ambaye atakuwa amechaguliwa kwa kura na wananchi, ili aje atutie adabu, kwani taifa liko katika hali mbaya, kila mmoja ni mjuaji na yote haya yamekuwa yakisababisha uvunjifu wa amani," alisema Dk Diallo.
"Watanzania ni waoga sana, wakisikia mlio wa bunduki wengi watakimbilia uvunguni mwa kitanda, tunataka Rais ajaye awe dikteta ili ainyooshe nchi hii, kwani imefikia katika hali mbaya, kuna watu wanaichezea amani yetu na ni mabingwa wa kuhamasisha vurugu na wanazungumza mambo wasiyoyajua," alisema Dk. Diallo, ambaye pia amewahi kuwa Naibu Waziri na Wizara katika serikali za awamu ya tatu na nne.
Mwenyekiti huyo pia alisema kuwa sheria za nchi pia zinapaswa zitazamwe upya katika kuilinda nchi hii kuepuka kupata viongozi wasiofaa na kuitaka Idara ya Usalama wa Taifa kuhakikisha inaisaidia serikali katika kupata viongozi bora na wasio na kasoro.
Alisema kuna baadhi ya maeneo baadhi ya watu wamejipenyeza kugombea uongozi na kushinda, huku wakiwa si watu safi, hali ambayo inaiyumbisha nchi.
"Kuna baadhi ya wabunge na madiwani ni X Criminals, ni wahalifu sugu wamefanikiwa kushika nafasi hizo, hapa unatarajia nini na kuna kiongozi mmoja hivi sasa ni kiongozi wa chama cha siasa katika ngazi ya wilaya huyu siyo Mtanzania, tatizo hapa katika siku za karibuni vyombo vyetu vimelegalega," alisema Dk Diallo.
Chanzo: Mtanzania