Dhurumu kwa walimu wa secondari halimashauri ya wilaya ya ileje

chiwanda

Member
Apr 1, 2011
26
6
Ndungu wanajavyi wenzangu nimeona niwajuze hii habari ili mjue linaloendelea kwa walimu wa secondari wa halimashauri ya wilaya ya ileje,nimesukumwa kuandika habari hii kutokana na kauri ya waziri wa elimu na mafunzo ya ufundi juzi bungeni kwamba serikari imeripa mishahara kwa walimu wote wario ajiriwa mwaka wa fedha uliokwisha.jamani si kweli hapa ileje tuna walimu 9 hawajalipwa mishahara yao hata mwezi mmoja hizi ni siasa za serikali ya CCM,Vijana hawa wanaishi maisha magumu sana wamekopa madeni mpaka wanaogopa hata kwenda madarasani kufundisha,kibaya zaidi hata mshahara wa mwezi huu wa sita hawamo kwenye orodha ya wanao takiwa kulipwa(pay roll].Nimerifuatiria hiri suara kwa umakini mkubwa sana kujaribu kubaini Tatizo ni nini?nimebaini kuwa mbali na mfumo mbovu wa namna mishahara inavyo shughurikiwa pia kuna tatizo la kiutendaji ndani ya harimashauri watendaji wanao husika na hili suala hawajalishughurikia kabisa mbaya zaidi hawakai ofisini wanashinda mbeya mjini wanafanya kazi siku tatu yaani juma tatu hadi juma tano.ukienda ofisini kuanzia alihamisi hawapo ofisini.Niharimashauri ambayo nafikiri watendaji wake wanafanya kazi kwa mazoea zaidi kuliko halimashauri zote nchini mbaya zaidi pamoja na harimashauri hiyo kuwa na upungufu mkubwa wa walimu mwalimu anapowataarifu kwamba anaacha kazi kwa sababu mshahara umegoma kutoka,wanamjibu nenda zako.harimashauri ilipangiwa warimu wapya zaidi ya ishirini lakini mpaka sasa waliobaki vituoni hawazidi 17.kunahitajiaka hatuwa za haraka kuwasaidia hawa vijana vinginevyo wataondoka wote.
 
Back
Top Bottom