Dhana ya Uwekezaji kwa mapana yake

Abdulhalim

Platinum Member
Jul 20, 2007
17,193
3,011
Wakuu heshima mbele,

Nina swali linalonitatiza. Nawasihi mniwie radhi kama litaonekana la kijinga kwa baadhi yenu. Nataka kuitumia fursa ambayo jamvi linatupatia kujielimisha, if possible.

Kuna hili suala la kuvutia wawekezaji. Nchi zote ulimwenguni, masikini kwa tajiri zinazungumzia kuhusu hili suala.

Kwa mujibu wa uelewa wangu mwekezaji ni mtafuta faida. Ni kweli anapokuja kuwekeza huleta kiasi cha mtaji (fedha, mitambo, ujuzi n.k) lakini kama atafanikiwa, ina maana baada ya muda huchuma faida kutoka sehemu aliyowekeza. Kwa maana rahisi ni kuwa atakuwa amechuma kutoka sehemu au nchi aliyowekeza, yaani atakuwa na mtaji alokuja nao jumlisha na faida amabyo hakuwa nayo hapo awali.

Kwa upande wa nchi inayomwalika mwekezaji, baada ya muda huo huo, kiwango cha utajiri(overall wealth) kitakuwa kimepungua kwa kiwango sawa na faida alopata mwekezaji.

Sasa hapa, inakuwaje watu wanang'ang'ania kuvutia wawekezaji na mitaji kutoka nchi za nje? Nini faida zake?
 
Bro. Abdul,
Mimi si mchumi, lakini ninavyofahamu kuna faida na hasara zake. inategemea na mchumaji mwenyewe. Ikiwa mchumaaji kama TRL, hawa ni wanyonyaji tuu na kilasiku ni malumbano tuu. Na kama mchumaji ni mzuri (faida kwa pande zote, mwekezaji na mkaribishaji na uwajibikaji) litakuwa na manufaa kwa maendeleo ya nchi. Manufaa yenyewe kama vile Ajira nyingi kwa wananchi, kupunguza umasikini, ....nk.
 
Binafsi ninaposikia viongozi wakihubiri na kupapatikia wawekezaji ninakuwa na maswali zaidi ya yale aliyonayo Abdulhalim. Nyerere aliwahi kusema atayaacha madini hadi Watz tutakapokuwa tayari kuchimba wenyewe. Watanzania hatujawa tayari kuchimba wenyewe, je! tumeshakuwa tayari kukaribisha wawekezaji? Nina maana kuwa na waandaaji wa sera, wataalam wa kusaini mikataba, wasimamiaji wa sheria za uwekezaji kwa lengo la kuhakikisha watz tunapata faida kubwa iwezekanavyo? Watz tulishaelimishwa kiasi cha kutosha kujua nini uwekezaji?

Yapo mambo mengine ya msingi ya kuangalia, kama wataalam wa kuajiriwa kwenye haya makampuni, watoaji huduma na wauzaji wa bidhaa kwa hawa wawekezaji, tuko tayari kiasi gani?

Wanaofuatilia maslahi ya Taifa uadilifu wao uko je? Kwani inaonekana tatizo kubwa la Watz wengi ni Uzalendo(Patriotic) na Uadilifu(Integrity).
 
Bro. Abdul,
Mimi si mchumi, lakini ninavyofahamu kuna faida na hasara zake. inategemea na mchumaji mwenyewe. Ikiwa mchumaaji kama TRL, hawa ni wanyonyaji tuu na kilasiku ni malumbano tuu. Na kama mchumaji ni mzuri (faida kwa pande zote, mwekezaji na mkaribishaji na uwajibikaji) litakuwa na manufaa kwa maendeleo ya nchi. Manufaa yenyewe kama vile Ajira nyingi kwa wananchi, kupunguza umasikini, ....nk.

Mkulu Kisu, hata mimi sio mchumi, najaribu ku-argue from naivette point of view. Kama nilivoelezea hapo juu kwamba nionavyo...kwa sisi nchi maskini uwekezaji holelaholela hautatufikisha popote kwa maana kwamba FAIDA TUNAYOBAKIWA NAYO NI FINYU SANA. Chukulia mfano wa Uchina, wanakaribisha wawekezaji wa mathalan mambo ya electronic, wale wawekezaji wakija wanakuja ku-exploit Chinese cheap labor, ambao kabla ya hapo hawakuwa na kazi (mfano) na mwisho wa siku Wachina wanapata ujuzi kwa njia halali au njia ya reverse engineering (mahodari sana kwa huu uwizi) ambao wanakuja baadae kuutumia kuanzisha makampuni yao wenyewe..na mwisho unakuta zile bidhaa haziwi flooded tu kwenye soko la Uchina, bali zinakuja kuuzwa ulimwenguni pote..mfano nikiiangalia hii mashine yangu ya DELL, vitu kibao inaonekana vimetengezwa Uchina...na trend ipo kubwa kwenye bidhaa nyingi ..Ktk situation kaa hii, ni wazi aina hii ya uwekezaji inaingia akilini kidogo.

Kwa upande mwingine hali ni tofauti kwa nchi ambayo inasubiria mwekezaji wa nje bila ya kuwa na mikakati yake yenyewe kuhusu mbeleni. Sasa hivi pamoja na kuwa huru kwa miaka zaidi ya 40 ya uhuru bado tunasubiri Mchina achukue tenda za kujenga nyumba za ghorofa moja au hata barabara za vumbi kule kwenye halmashauri. Hii ni aibu. Ukitembelea jiji la Dar utakuta kila kona vijana wamekaa tu hawana shughuli yeyote ya kufanya, thanks kwa ujinga wetu wa kudhani bila kuwa protectionists tunaeza kuupiga vita umaskini. Ninachoweza kusema ni kwamba serikali inafanya makosa sana kujivua jukumu la kuwekeza kwenye miradi ya maendeleo, na kuruhusu nguvu za soko zichukue mkondo, bila kumpa ulinzi wowote mwananchi wa kawaida. Inachofanya ni sawa na kumuweka mtoto mchanga mchana upenuni kwenye jua la saa nane bila mwamvuli bila uangalizi wowote.
 
Uwekezaji ni wa lazima ili nchi iweze kuendelea!
Uwekezaji kwa kifupi ni kutumia resources zilizopo kuboresha maisha.
Nchi zinatafuta wawekezaji coz zinaamini wanauelewa mkubwa wa utumiaji wa resources tofauti tofauti ambazo nchi husika inazo. Kukaa kwa resources bila kutumika hakuna faida kwa nchi husika.

Kwa mfano kuwa na ardhi nzuri ambayo haitumiki na wananchi wa nchi husika hawana mpango nayo, just an idle land!

Hapo serikali inaweza kutafuta muwekezaji atakae itumia hiyo ardhi effetively na kuboresha maisha. Ataboresha maisha kivipi? Atalipa kodi, ataajiri wafanyakazi, atanunua vitendea kazi, atajenga nyumba, godowns, mashines za kuprocess nafaka, etc).
Hivi vyote vitakosekana kama muwekezaji hata jitokeza. Kwa maana hiyo muwekezaji asipojitokeza hiyo rasilimali itakuwa haina faida kwa nchi husika zaidi ya kuwa hasara, coz serikali itadb iiangalie hyo idle land kwa expense ya vitu vingine.

Hyo ndio concept rahisi ya uwekezaji kwa layman!
Nadhani nimesaidia kwa kiasi fulani!
 
Back
Top Bottom