Bob Nyanga Makani ni mmoja wa waasisi wa CHADEMA, ni Msukuma, Mwislamu kutoka Kutoka Shinyanga na katibu mkuu wa Kwanza wa CHADEMA.
Katibu mkuu ndiye mwenye siri zote Chama, ndiyo anakaa na mafaili yote, ni mwajiri wa wafanya kazi wa makao makuu nk.
Nimejifunza mambo yafuatayo.
Mosi, Kama waanzilishi wa CHADEMA wangekuwa na agenda udini wasingemchagua Bob Makani kwa sababu yeye ni Mwislamu. ( Binafsi nimejua dini yake wakati wa msiba)
Pili kama waasisi wa CHADEMA wangekuwa wanaagenda ya Ukanda wasingemchagua Bob Makani kwa sababu hatoki kanda ya kaskazini.
Tatu, Kama waasisi wangekuwa na agenda ya ukabila wasingemchagua Bob Makani kwa sababu si Mchaga.
Kitendo cha kumchagua Msukuma, Muislamu, kutoka kanda ya Shinyanga katibu mkuu na baadaye kuongezewa cheo na kuwa Mkiti ina maanisha kuwa alifanya kazi vizuri na alikuwa anakubalika na wajumbe wote bila kujali dini, ukanda wala ukabila.
Wale waliokuwa wanacheza CD ya udini, ukanda na ukabila dhidi ya CHADEMA sasa inabidi watafute CD nyingine ya kucheza dhidi CHADEMA vinginevyo hii ya Ukanda, . ukabila na udini sasa zimechuja. Haiuziki tena.
Ni mawazo yangu tu.
Katibu mkuu ndiye mwenye siri zote Chama, ndiyo anakaa na mafaili yote, ni mwajiri wa wafanya kazi wa makao makuu nk.
Nimejifunza mambo yafuatayo.
Mosi, Kama waanzilishi wa CHADEMA wangekuwa na agenda udini wasingemchagua Bob Makani kwa sababu yeye ni Mwislamu. ( Binafsi nimejua dini yake wakati wa msiba)
Pili kama waasisi wa CHADEMA wangekuwa wanaagenda ya Ukanda wasingemchagua Bob Makani kwa sababu hatoki kanda ya kaskazini.
Tatu, Kama waasisi wangekuwa na agenda ya ukabila wasingemchagua Bob Makani kwa sababu si Mchaga.
Kitendo cha kumchagua Msukuma, Muislamu, kutoka kanda ya Shinyanga katibu mkuu na baadaye kuongezewa cheo na kuwa Mkiti ina maanisha kuwa alifanya kazi vizuri na alikuwa anakubalika na wajumbe wote bila kujali dini, ukanda wala ukabila.
Wale waliokuwa wanacheza CD ya udini, ukanda na ukabila dhidi ya CHADEMA sasa inabidi watafute CD nyingine ya kucheza dhidi CHADEMA vinginevyo hii ya Ukanda, . ukabila na udini sasa zimechuja. Haiuziki tena.
Ni mawazo yangu tu.