Dhana ya polisi jamii na mauaji ya polisi dhidi ya raia

meningitis

JF-Expert Member
Nov 17, 2010
8,349
4,674
mara nyingi kwa siku za karibuni tumesikia kampeni ya kipolisi inayoenda kwa jina la polisi jamii.kampeni hii pamoja na mambo mengine imelenga kujenga ukaribu wa polisi na raia ili kuzuia uhalifu.kampeni ilitakiwa kuwa kiunganishi na sio ukuta kati ya polisi na raia.
Vilevile kumekuwepo na ongezeko la ripoti za matukio ya polisi kuwatwanga raia risasi zinazopelekea vifo au majereha.mifano ni pamoja na arusha,tarime,mbeya,dodoma,iringa na leo hii songea.
Kuna taarifa kadhaa kulingana na vyombo vya habari mbalimbali zimeonyesha mafanikio ya polisi dhidi ya uhalifu yametokana na taarifa zinazotolewa na raia wema.

Ukijaribu kufuatilia utekelezaji wa dhana hii unaonyesha mafanikio kwa raia kutimiza wajibu wao......lakini jeshi la polisi halijafanya hivyo,bado jeshi la polisi linataka kuonekana wao ndio wao,kwa maneno mengine polisi hawajaonesha ushirikiano kwa raia.

Je tatizo ni elimu ya watendaji wa polisi?

je tatizo ni siasa za nchi yetu?

Je tatizo ni viongozi(waziri wa mambo ya ndani,IGP,RPCs)
 
Mi nadhani bado hawa polisi hwajafundishwa vya kutosha kuwa uaskari sio ung'ombe. Bado wana dhana ya kutumia ng'uvu mno kuliko akili na majadiliano. Wanadhana kuwa ukishakuwa askari wewe unatakiwa uogopwe. Haya mapungufu ukijumlisha na viwango vya elimu kwa walio wengi ni lazima uwe na tabia hizi chafu za kuua ovyo. Hawajui kuwa raia wanaweza pia kuwafanya vivyo hivyo. Nadhani kuna kazi kubwa ya kufanya kuondoa huu ufinyu wa kufikiri hasa kwa vijana wetu wanaojiunga na form four failures, ambao hawana exposure kubwa kwenye maisha ya kutegemezana.
 
tukiassume kwamba wanachokifanya polisi kinatokana na tabia au hulka ya kitanzania basi tutegemee vita kali kati ya raia na vyombo vya usalama na hii ni vita hatari sana.nashangaa kuona polisi wakitumia ubabe au nguvu katika kukamata makundi mbalimbali ya kijamii,imagine mtutu unatumika kumkamata jambazi,kibaka,mwanafunzi,mwanamke mwanaharakati au kiongozi wa chama flani!
 
mara nyingi kwa siku za karibuni tumesikia kampeni ya kipolisi inayoenda kwa jina la polisi jamii.kampeni hii pamoja na mambo mengine imelenga kujenga ukaribu wa polisi na raia ili kuzuia uhalifu.kampeni ilitakiwa kuwa kiunganishi na sio ukuta kati ya polisi na raia.
Vilevile kumekuwepo na ongezeko la ripoti za matukio ya polisi kuwatwanga raia risasi zinazopelekea vifo au majereha.mifano ni pamoja na arusha,tarime,mbeya,dodoma,iringa na leo hii songea.
Kuna taarifa kadhaa kulingana na vyombo vya habari mbalimbali zimeonyesha mafanikio ya polisi dhidi ya uhalifu yametokana na taarifa zinazotolewa na raia wema.

Ukijaribu kufuatilia utekelezaji wa dhana hii unaonyesha mafanikio kwa raia kutimiza wajibu wao......lakini jeshi la polisi halijafanya hivyo,bado jeshi la polisi linataka kuonekana wao ndio wao,kwa maneno mengine polisi hawajaonesha ushirikiano kwa raia.

Je tatizo ni elimu ya watendaji wa polisi?

je tatizo ni siasa za nchi yetu?

Je tatizo ni viongozi(waziri wa mambo ya ndani,IGP,RPCs)

Tatizo ni kwa wote uliowataja kila mmoja anachangia kwa sehemu yake
 
kadri siku zinavyoenda ndivyo hali hii inavyozidi kuota mizizi.hakuna polisi anayewajibishwa!

Kwani wameweza kuwawajibisha hao walio karibu nao kama mawaziri, manaibu na makatibu wakuu ndo waweze kuwafuatilia hawa waliopo mbali nao yani police
 
Kwani wameweza kuwawajibisha hao walio karibu nao kama mawaziri, manaibu na makatibu wakuu ndo waweze kuwafuatilia hawa waliopo mbali nao yani police
kwa hiyo tuanze kumuwajibisha Nahodha
kwani nadhani kitakwimu vifo vingi vimetokea katika uongozi wake.
 
Ifike wakati uaskari iwe taaluma yenye maadili na si kuchukua watu mbumbumbu na waliokata tamaa kielimu na kimaisha.
 
Ifike wakati uaskari iwe taaluma yenye maadili na si kuchukua watu mbumbumbu na waliokata tamaa kielimu na kimaisha.

Hakika, askari polisi walio wengi kwa sasa ni wale watoto ambao aidha walishindikana majumbani kwa wazazi wao na walikwenda CCP wazazi wakitegemea watabadilishwa tabia na hapo hapo kuwin ajira au wale waliofanya vibaya shuleni na ikawa polisi ndio dampo yao. Matokeo yake vijana hawa wameanza kazi wakiwa nunda kuliko yaani ni makauzu kufa.

Lakini pili lawama ziende kwa viongozi wao, kwa sababu hata jamii inapotoa taarifa juu ya matendo na mwenendo isiyoridhisha ya polisi hawa hakuna ufuatiliaji wowote. Mfano ni tukio lililotokea usiku wa tar 18/02. Polisi mmoja ambaye anaitwa PC Magesa wa kituo kikuu cha polisi Mtwara alimbaka, kumwagia maji mwili mzima na hatimaye yeye na polisi mwenzake wanayekaa naye nyumba moja kumpiga kipigo cha mbwa mwizi dada mmoja aliyeomba kampan kwao akitoka matembezi ya usiku kwa kuamini wao ni watu wa usalama. Mashuhuda wa tukio hilo walipomhoji askari huyo kwa nini alifanya kitendo hicho cha udhalilishaji, alisema kwa nyodo kuwa ndo ameshafanya na hawawezi kumfanya chochote.
Pamoja na taarifa hizo kufika kituoni hakuna chochote kilichofuata na magesa yupo mtaani kama kawa.

Kwa hili nadhani ingekuwa vema kama uadilifu ungeanza kwa viongozi wao, hawa masaidia wangeweza kukopi kitu.
 
kwenye sekta ya afya kuna utaratibu kwamba kila kifo cha mama mjamzito(maternal mortality) ni lazima kitolewe ufafanuzi wizarani,je utaratibu huu ufanyike kwa wizara ya mambo ya ndani?kwamba kila tukio la polisi kuua raia lifafanuliwe kwa kina wizara ya mambo ya ndani?
 
hizi risasi za moto hutolewa wakati gani ? mbona kila siku risasi za moto , TZ kama Syria
 
afadhali nimesikia kwamba polisi wanne wamekamatwa kwa mauaji ya songea.wasiwasi wangu ni kwamba baada ya miezi kadhaa utasikia polisi hawa hawana hatia.
 
afadhali nimesikia kwamba polisi wanne wamekamatwa kwa mauaji ya songea.wasiwasi wangu ni kwamba baada ya miezi kadhaa utasikia polisi hawa hawana hatia.

mkuu hiyo ni boshen tu.
Wanafunika kombe mwanaharam apite.

Sijui wale majambazi wetu watumiao siraha kali za kivita wapo wapi.Ni bora waludi kwa kasi iliwatu saidie kuwaadabisha hawa mbweha wa MWEMA.
Na hii dhana ya ulinzi shilikish ni bora ivunjwe.
 
Back
Top Bottom