Nakapanya
JF-Expert Member
- May 22, 2012
- 2,096
- 708
Nyoka anapojivua gamba;hufanya hivyo ili kuondoa gamba lile lililochoka ambalo haliwezi tena kutenda kazi ya kumlinda,kujongea na hata kumwezesha katika harakati za kuendeleza maisha yake kwa ujumla,hivyo hujivua gamba la zamani lilichoka ili kupata jipya ili kutimiza hayo hapo juu.CCM walipokuja na dhana ya kujivua gamba walikuwa na dhamira ileile kama ya nyoka yaani kuvua magamba(viongozi na wanachama)ambao wamechoka na hawana uwezo tena wa kukisaidia chama kutimiza malengo yake ya kila siku ya kuwaletea wananchi maendeleo.CHADEMA wamekuja na kampeni yao ya kuvaa gwanda(nijuavyo mimi ni askari tu ndio huvaa magwanda),nadhani wanavaa gwanda ili kuingia katika vita na mapambano ya kushika dola mwaka 2015,lakini katika vita hiyo wanataka kutumia sungusungu kupamban,hakikia mtashindwa;kwanini nasema hivyo;CCM wamevua magamba na kuyatupa kwa kuona hayafai tena,ila sasa hao CHADEMA wana pita nyuma na kuyaokota yale MAGAMBA NA KUYAVIKA MAGWANDA ili yakapigane,hakika mtashindwa milele na CCM itaendelea kutawala milele.Ni hayo tu na ni mtazamo wangu wa ki-shallow.