Hydrocephalus
Member
- Feb 6, 2012
- 27
- 5
Leo asubuhi hii, nilifika pale ukumbi wa CPL muhimbili, ambapo imesemekana tunatakiwa kukutana na PM Pinda. Lakini baada ya kufika hapo ili nipate nafasi, Tumekuta watu ambao walitufukuza na kutueleza kuwa hatutakiwi hapo tuende MUHAS tukakaekae huko kwanza. Sasa najiuliza, huyu pinda anakuja kukutana na nani???. Na, in the first place anakuja kututangazia solutions ambazo serikali imezidevelop in accordance with our grievancies? au anakuja kuanza kujadiliana na hao watu anaotaka kukutana nao. Kwanza ni kwa nini amesema tukutane nae CPL wakati anajua ukumbi ule ni mdogo na hauwezi ku accomodate makundi ya madaktari yote aliyoyataja kuwa yakutane nae. Hapa nagundua kuna mchezo wa hadaa unataka kufanyika hapa. ninachoweza kuiambia serikali ni kwamba, Jumuiya ya madaktari, kama zilivyo jumuiya za kisomi nyinginezo, ni jumuiya ya watu wenye uelewa wa hali ya juu, na tunajua ni nini tunachokifanya. Huu si wakati wa kufanya suluhisho za hadaa au za vitisho. Hakika hizi damu za watanzania zitawamwagikia ninyi na vizazi vyenu.
Ngoja nirudi tena CPL nikajaribu kuangalia kama kunaingilika, kwa maana ninataka nikae mbele kabisa niweze kusikiliza kwa makini pumba za PM, na niweze kumpasha yale niliyonayo moyoni!!
Ngoja nirudi tena CPL nikajaribu kuangalia kama kunaingilika, kwa maana ninataka nikae mbele kabisa niweze kusikiliza kwa makini pumba za PM, na niweze kumpasha yale niliyonayo moyoni!!