Gaijin
JF-Expert Member
- Aug 21, 2007
- 11,812
- 5,284
Mjukuu mai dia, mimi siko lawamani,
Mila naizingatia, tangu enzi utotoni,
siwezi kuichenjia, nitakuwa matatani,
mwanaume kaumbiwa, kuishi na wake wengi.
Mwanaume kwa yakini, infi kwake asilia,
Acha mwanamke ndani, wa nje kuhudumia,
Kuweka sawa mizani, wanawake mezidia,
Mwanaume ameumbwa, kuishi na wake wengi.
Mwanamke kibishia, kisasi talipizia,
Hiyo ndio chakachua, mjukuu anasemea,
Infii haina nia, kuanzisha chakachua,
Mwanaeme kaumbiwa, kuishi na wake wengi!:welcome::welcome::welcome:
kwanini si chakachue, naye fikiri aweza?
ubunifu kwake yeye, upo umejituliza
mwanamme si pekee, faida anae waza
kama ni kuchakachua, wote wana nguvu sawa.
mwanamke siku hizi, ni mjasiriamali
hesabu haimkwazi, sio kama wa awali
chakachua ya mapenzi, mtaji wafika mbali
kama ni kuchakachua, wote wana nguvu sawa.