KIJANA mmoja anayejishughulisha na kubeba abiria kupitia usafiri wa pikipiki ametekwa na kuuawa.
Kijana huyo anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 20 hadi 22 ameuawa kwa kuchinjwa na abiria ambao aliwabeba kuwapeleka sehemu husika.
Tukio hilo limetokea maeneo ya Kimara Golani.
Kijana huyo ambaye jina lake kamili halikuweza kupatikana mara moja anayejulikana kama Chinga alikodishwa na watu wawili awapeleke huko Kimara Golani.
Inasemekana kuwa wakati wako njiani akiwapeleka wateja wake hao ndipo walipomtaka ashuke na wao waondoke na pikipiki hiyo.
Taarifa zilizomfikia mwandishi wa Nifahamishe, zilisema kuwa kijana huyo alipotakiwa aachie pikipiki hiyo alikuwa anasita kuachia mali yake hiyo, na ndipo walipotoa shoka na kumpiga nayo sehemu za kichwa na kufariki papohapo.
Baada ya kuona kijana huyo amefariki dunia wezi hao ambao walikuwa ni abiria waliondoka na pikipiki hiyo na kumuacha kijana huyo mahali hapo.
Source: http://www.nifahamishe.com
Kijana huyo anayekadiriwa kuwa na miaka kati ya 20 hadi 22 ameuawa kwa kuchinjwa na abiria ambao aliwabeba kuwapeleka sehemu husika.
Tukio hilo limetokea maeneo ya Kimara Golani.
Kijana huyo ambaye jina lake kamili halikuweza kupatikana mara moja anayejulikana kama Chinga alikodishwa na watu wawili awapeleke huko Kimara Golani.
Inasemekana kuwa wakati wako njiani akiwapeleka wateja wake hao ndipo walipomtaka ashuke na wao waondoke na pikipiki hiyo.
Taarifa zilizomfikia mwandishi wa Nifahamishe, zilisema kuwa kijana huyo alipotakiwa aachie pikipiki hiyo alikuwa anasita kuachia mali yake hiyo, na ndipo walipotoa shoka na kumpiga nayo sehemu za kichwa na kufariki papohapo.
Baada ya kuona kijana huyo amefariki dunia wezi hao ambao walikuwa ni abiria waliondoka na pikipiki hiyo na kumuacha kijana huyo mahali hapo.
Source: http://www.nifahamishe.com