Deni la Taifa: Kutoka trilioni 10.5 hadi trilioni 14.4 kwa mwaka?

Mkuu TUME naomba pia kupitia uzi wako kama utaweza utueleze mwinyi aliacha deni kiasi gani na mkapa aliacha kiasi gani na sasa ni tr22
 
Taifa kukopa kwa sana nchi za nje kunahatarisha amani na uhuru wetu kama nchi. Hili ni jambo lisilohitaji kujadiliwa kisiasa siasa vile.
 
Viongozi wetu ni wagonjwa wa kufikiri me benafsi naonerea hivyo.sababu nchi hii ni tajiri sana hiyo haipingiki. Sasa hayo madeni wanayokopa ata siwaelewi sabu wanakopa kwa maendeleo je ni maendeleo yapi?.mimi kwa akili yangu ya kipimbi ningeweza kujiulize ivi uyu anayenipa samaki baadaya kunifundisha kuvua samaki is he right? This is a basic to those takers of loan and grant from outside to reason themselves.kama wangekua na upeo wa kufikiri kama huu wa kujireason before action wasinge ileta Tanzania walipoifikisha apa ilipo.
 
Deni la taifa limefikia zaidi ya Sh. Trilioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, lakini Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa amesema hakuna sababu ya kupaniki kwa kuwa sehemu kubwa ya deni hilo limewekezwa kwenye miradi ya nishati na maji.

Dkt. Mgimwa amesema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita, Tanzania ilipata mkopo wa karibu sh. trilioni moja kutoka China kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar Es Salaam.

Amesema kuwa mradi huo ukikamilika utazalisha nishati zaidi na kwa gharama nafuu. Mradi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 18 ijayo.

Pia amesema Tanzania imepokea dola za Kimarekani milioni 178.2 kwa ajili ya mradi wa maji Ruvu, kwa hiyo hakuna haja kuogopa kuongezeka kwa deni la taifa.

Some reflections

[video=youtube_share;T3wgDb2PRAI]http://youtu.be/T3wgDb2PRAI[/video]
 
Umewahi kujiuliza kuhusu fedha ulizo nazo zinatoka wapi, na hizo zimetoka na mwendelezo unaofanana na huo? Bila deni hakuna fedha -- ni lazima kama nchi tukope! Deni kwa nchi yeyote halikwepeki, namna ambayo fedha zilizoleta deni zilivyotumika ladba ndio swala la kujadili.
 
.......................................................................
namna ambayo fedha zilizoleta deni zilivyotumika ladba ndio swala la kujadili.
nakuunga mkono hili ndilo la kuangaliwa!
 
2006 deni lilikuwa ni 6 Trillioni miaka 6 mingine limeongezeka kwa kasi ya kutisha. Na hakuna chochote cha kujivunia kilichofanywa ndani ya hiyo miaka sita. Kweli Kikwete na Serikali yake ni dhaifu.
 
Umewahi kujiuliza kuhusu fedha ulizo nazo zinatoka wapi, na hizo zimetoka na mwendelezo unaofanana na huo? Bila deni hakuna fedha -- ni lazima kama nchi tukope! Deni kwa nchi yeyote halikwepeki, namna ambayo fedha zilizoleta deni zilivyotumika ladba ndio swala la kujadili.

Kauli yako ina mtizamo wa watu wengi ambao huenda kukopa kabla ya ku-plan namna ya kutumia huo mkopo au plan ya mkopo haina tija na wala haina faida ya kurudisha deni na kutengeneza faida. Nchi nyingi zakopa lkn sio jambo la kuzoea hata kidogo. kwa nini tusifike mahali pa kutumia tunachozalisha? Hata wewe binafsi wapaswa kuishi kulingana na kipato chako na kama unataka maisha ya juu zaidi kabla ya kuishi hayo maisha ongeza kipato chako kwanza kitakacho kuwezesha kuishi hayo maisha.

Issue ya deni la Taifa nina maana kuwa hata kama tukaendelea kukopa, tukope kwa sababu za msingi na ile pesa itumike kwa tija. CCM hawawezi kufanya hili. Tunahitaji watu serious. Na tutakapowata watu serious hii ndo namna ya kuwawezesha, tuchange kulipa deni, sio lazima wapeleke tunakodaiwa, fedha hizo zinaweza kuwa invested e.g. mining of minerals, gas or oil. Tukainua uchumi wetu kwanza. Lakini hii ikawa approach ya kuonyesha uzalendo.

NB. WAZALENDO BADO TUPO LKN SERIKALI YA CCM INAKATISHA TAMAA SANA.
 
Pamoja na Deni lote hilo utashangaa Paul Sozigwa anazunguka kwa miaka 30 hazina kufuatilia mafao yake ukipiga hesabu karibu kila mtanzania ana deni la laki sita duh tutauza watoto
 
Nishati na maji ambayo ni kizungumkuti kikubwa mwaka hadi mwaka katika kila kona ya nchi yetu. Tungekuwa na mikataba halali yenye maslahi kwa Tanzania na Watanzania na makampuni toka nje ya uchimbaji wa madini nchini deni hili lingefutwa kirahisi sana, lakini kutokana na mikataba ya kifisadi litazidi kuongezeka kwa kasi ya kutisha na kuongeza ugumu wa maisha kwa Watanzania walio wengi.

Deni la taifa limefikia zaidi ya Sh. Trilioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, lakini Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa amesema hakuna sababu ya kupaniki kwa kuwa sehumu kubwa ya deni hilo limewekezwa kwenye miradi ya nishati na maji.

Dkt. Mgimwa amesema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja ulioyopita, Tanzania ilipata mkopo wa karibu sh. trilioni moja kutoka China kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar Es Salaam.

Amesema kuwa mradi huo ukikamilika utazalisha nishati zaidi na kwa gharama nafuu. Mradi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 18 ijayo.

Pia amesema Tanzania imepokea dola za Kimarekani 178.2 kwa ajili ya mradi wa maji Ruvu, kwa hiyo hakuna haja kuogopa kuongezeka kwa deni la taifa.
 
aiseeeeeeeeeeeeeeeeeeee babayangu bado pesa za dowans hatujalipa tutakufa c c m ikibaki madarakani
 
Hawa jamaa wanazidi kutukamua tuu....usikute hapo nusu ya deni imeingia mifukoni mwao na efficience ya matumizi ya hiyo nusu iliyobaki ni only 40%
 
kutoka 5trillion hadi 20 trillion kwa kipindi kisichozidi miaka saba. je,kwa kasi hii hadi 2015, deni litakuwa shillingi ngapi?
 
Na hii inatokea kwenye nchi ambayo GDP yake ni USD 23bn!

Miradi ya umeme - I have lost count! Kila kukicha utasikia 'tuna mradi x,y,z na mara utakapo kamilika gharama za kuzalisha nishati zitakuwa bei nafuu"!!!

Hilo bomba la gesi/mkopo wa mchina: Kuna mkataba wa mgodi wa makaa ya mawe ambao Tanzania wamewapa wachina 80% na sisi tukabaki na 20% (umangungo - maoni yangu). na Makataba huu wa mgodi uligusia ujenzi wa bomba la gesi, sasa, hili deni tunaloambiwa linaingiaje kwenye deni la taifa, na mkataba wa makaa ya mawe unakuwa wapi?
 
Hivi Sultani pale magogoni anafanya nini?,kazi kuwaza safari na kwenda kupumzika serengeti tu!
 
Kwa utawala huu wa kifisadi wa kwapua kwapua, tujiandae kuendelea kushuhudia deni likipanga huku maisha ya wananchi yakizidi kuporomoka hadi kukosa maana. Shame on Kikwekwe and his cabal of thugs.
Deni la taifa limefikia zaidi ya Sh. Trilioni 20 mwishoni mwa mwaka huu, lakini Waziri wa Fedha Dkt. William Mgimwa amesema hakuna sababu ya kupaniki kwa kuwa sehumu kubwa ya deni hilo limewekezwa kwenye miradi ya nishati na maji.

Dkt. Mgimwa amesema kuwa katika kipindi cha mwaka mmoja ulioyopita, Tanzania ilipata mkopo wa karibu sh. trilioni moja kutoka China kujenga bomba la gesi kutoka Mtwara kwenda Dar Es Salaam.

Amesema kuwa mradi huo ukikamilika utazalisha nishati zaidi na kwa gharama nafuu. Mradi huo unatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 18 ijayo.

Pia amesema Tanzania imepokea dola za Kimarekani 178.2 kwa ajili ya mradi wa maji Ruvu, kwa hiyo hakuna haja kuogopa kuongezeka kwa deni la taifa.
 
Tanzania Tanzania Tanzania Tanzania Tanzania Tanzania Tanzania Tanzania Tanzania................:confused:
 
Back
Top Bottom