Mhache
JF-Expert Member
- Jun 20, 2008
- 345
- 24
Katika pitapita yangu jijini Dar es Salaam nimekutana na gazeti la UWAZI likionyesha mama mmoja aliyepoteza maisha baada ya kufika kwenye za DECI na kukuta kufuli kubwa mithili ya Kichwa cha ng'ombe. Mama huyo ilikuwa ni siku yake ya kwenda kuvuna mapesa kutokana na fedha au mbegu alizopanda. Ghafla alidondoka na kufariki papo hapo. Hii ni habari iliyopo ndani ya gazeti hilo la uwazi. Wanajamii forum ambao mlikuwa wanachama wa iliyokuwa DECI je habari hizo ni za kweli?
Cha kushangaza ni kwamba mama huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alitoka home asubuhi na kusema anaenda kwenye shughuli zake za kila siku. Mume hakujua kwamba mkewe ni mwanachama wa DECI. Alijua baada ya kifo kumkuta mumewe. Kuna haja ya kuwa na mawasiliano baina ya wanandoa.
Cha kushangaza ni kwamba mama huyo ambaye kwa sasa ni marehemu alitoka home asubuhi na kusema anaenda kwenye shughuli zake za kila siku. Mume hakujua kwamba mkewe ni mwanachama wa DECI. Alijua baada ya kifo kumkuta mumewe. Kuna haja ya kuwa na mawasiliano baina ya wanandoa.