DECI Tanzania: Ilivyoanza, ilipo na hatma yake

kama mnajiuliza jinsi inavyofanya kazi, nendeni pale mabibo mkaulize, sio mnakaa kusikiliza mambo ya wachangiaji wa hapa ambao hata hawajui kinachoendelea kule. wengi hapa walikuwa hata hawajui iko ofisi za wapi, kinachoonyesha kuwa hamuijui kabisa hivyo msichangie hadi mwende mkafanye utafiti. mimi nitaishia hapo. isipokuwa, mtu ukipanda kule Deci, unakaa miezi mitatu na nusu ndio unaenda kuvuna, sio mwezi mmoja kama wengine walivyosema hapa. asante.
 
tatizo, hili jambo halikuwa kwa watu wote ninyi, lilikuwa kwa watz wachache ambao ni walokole, hata halikuwa linawahusu. Tumewahusisha mmeanza kutuchefua? Tutarudisha liwe kwa walokole tu. Sisi kama walokole tunaridhika, na maadam tumesha vuna kwa mara nyingi tukapata faida, hatuna shida. Hata ikiisha leo hatuna hasara. Pilipili usoila inawawashia nini? Wanaotumia wamenyamaza kimya, ninyi ambao hamjatumia mnaongea. Mnaweza mkamkomvisi vipi mtu ambaye ameshavuna pesa mara kibao, aliweka laki mbili amesha vuna mle takribani million nne tayari, sasa. Tunapata faida, na hatutaiacha, na hata kama watu watasema sana, mnachelewa bure, mtasema matokeo yake mtakuja kuujua ukweli wake muda wakati umeisha na ninyi nafasi ya kufaidika imefungwa. Kalaga baho.

nina mashaka na ulokole wako. Yesu hakuwa mfanyibiashara, asilani. Na hakutumia dini wala sinagogi kufanyia biashara. Bali nyumba ya baba yake itaitwa nyumba ya sala, yaonekana mmegeuza kuwa pango la wachuuza fedha!
 
c. Sasa Benki haiwezi kutoa fedha tu za faida bila yenyewe kutengeneza faida vile vile. Hivyo kwenye hii DECI maswali yanayokuja ni kwamba hao jamaa wao wanapata faida gani?




TATIZO:
Kwa kadiri ya kwamba mtindo huo unategemea wateja wapya na unaendelea kuahidi mavuno makubwa, basi hatima yake ni kuanguka au kuporomoka kwani baada ya watu wote kujiunga na mtandao huo wale wanaoingia mwisho watajikuta hakuna wa kuwalipa wakati wale walioingia mwanzoni watakuwa wameshakuwa matajiri wa haraka haraka!
QUOTE]


HAPO TU MIMI PAMETOSHA KABISA KUNIFUNGUA MACHO!haswa haswa.KWENYE TATIZO.

sasa wanajamii wenzangu tuwasaidie wenzetu wasio na access ya mtandao!walau kutoa ANGALIZO KWA WATU WAWILI TU,ili taarifa zisambae
 
Watanzania tumeambukizana ugonjwa mbaya wa kuamini, na kujaribu kutafuta njia za mkato za kufanikiwa. Hii inaenda kwenye mambo mengi: kuiba mitihani, kughushi vyeti, ufisadi, utapeli na mengine menngi. Kwetu ukipata mpango kama DECI unaona umetibu tatizo la umaskini.

Mimi naona ndugu aliyeanzisha thread hii ana point. Ni vema kujiuliza, huyo anayeweza kukupa faida 100% ndani ya miezi mitatu, yeye anazalishaje???? na hii bila kujali kama ni mlokole au nani. Nina hakika mchezo huu hautakuwa na muda mrefu. Na pale utakapoishia kutakuwa na shida kama hii hapa iliyotokea Columbia: http://www.latinalista.net/linkinglatinas/2008/11/colombia_pyramid_money_scams_fall_down_a.html
Kwa sasa si DECI tu. Kuna POWER CLUB, na vingine vingi. Na unakuta anayeshabikia mchezo mmoja ana mwelekeo wa kuingia na mwingine.

Msingi wa michezo hii unaelezwa katika link hii: http://en.wikipedia.org/wiki/Pyramid_scheme

Ndugu zangu Watanzania: Walokole kwa wasiomjua Mungu: Siri ya mafanikio ni Hard Work. Hakuna njia ya mkato. Hata Kitabu mnachokiamini walokole kinasema "Asiyefanya Kazi na asile ...."

Well mnafaidika kwa sasa, lakini future ya mpango ambao hauleweki unazalishaje ni vema kuifikiria.
 
Unajaribu kutuaminisha kuwa walokole ni malaika? Kama umekiri kuwa sasa walokole wako kwenye madhehebu mengi, na kama unakumbuka kuwa kuna baadhi ya wachungaji walokole ambao wako jela au kesi zao bado zinaendelea kwa makosa ya wizi, una ushahidi gani wa kutueleza kuwa hawa ni tofauti? Ningefurahi sana kama ungejibu hoja za watu wenye wasi wasi na DECI badala ya kutuletea hadithi za walokole katika mambo ambayo yanaonekana ni wizi mtupu!!

someni alichoandika mwanakijiji ndicho sahihi. after all mmesahau kuwa yule mchungaji aliyekamamtwa na viungo vya albino ni mlokole?
 
DECI ilianzishwa kusaidia watu wasiojiweza ambao kipato chao ni kidogo hivyo wao waliweka taratibu kama hiyo atttachment DECI.doc inavyoonyesha ili mtu yeyote ambaye kipato chake ni kidogo awekeze huko na kupata hiyo faida kama ilivyoonyeshwa kwenye jedwali hilo. Ni taasisi ya kidini ya watu wa pentecoste ambao waliianzisha ili kuwezesha maskini. Attachment hii haionekani vizuri lakini unaweza kuwaandikia through decitanzania@yahoo.com.

Mimi ni member wa kule na nimeshavuna mara moja kwani nimejiunga mwaka jana kwenye July. Hawa jamaa wana simu kama zinavyooneka na email pia hivyo kuondoa mikanganyiko mtu ambaye anataka kuelewa kwa undani awapigie watamueleza au awaandikie email watamjibu.

Ukiisoma vizuri utaona kuwa kuna kiingilio unacholipa na pia kuna makato kila unapovuna.

Kusema kweli nilitake a risk maana sikuwa na muda wa kufuatilia kwa undani wanafanya kazi vipi. Kazi zilinibana nikakosa muda wa kwenda kuulizia in detail. Nimewawekea hizo attachment ili kila mmoja kwa muda wake awasiliane nao na kuuliza chochote.

DECI imesaidia watu sana japo mwanzo ilikuwa kidini zaidi lakini sasa ni watu wote wanapewa huduma. Mimi nimeisikia kama miaka mitano hivi iliyopita.

Fuatilieni kwanza kabla ya kuanza kuwalaumu jamaa. Sidhani kama wana nia mbaya maana miaka yote hiyo wangekuwa wameshaingia mitini.

Ni mara yangu ya kwanza kutuma thread so may be kutakuwa na makosa or else mapungufu chukueni content hasa hizo attachment.

Nawashukuru na nawakilisha.
 

Attachments

  • ELIMIKA SCHEME.doc
    40 KB · Views: 113
  • DECI.doc
    126.5 KB · Views: 65
Kwa kifupi waungwana, mchezo huu unachezwa kwa kushawishi watu wawekeze na wabadilishe muda wa kuchukua ili kuweza kusubiri wawekezaji wapya.

Hii ilianzishwa na mwekezaji Billionaire Charles Ponzi baada ya WW II.

Ili huu mchezo uendelee, inabidi dola isiingilie na watu waishi kwa matumaini kama wale wenye VVU.

Kuna sharti moja katika hii DECI linasema, masharti yanaweza kubadilika wakati wowote jiulize mara mia mbili???
 
Mugerezi,

Wewe ulipanda shilingi ngapi na mpaka sasa umeshavuna bei gani kama faida ...July 08 to date?
 
Last edited:
Hii ni sawa na kamari ni kula na kuliwa.Watanzania tunawenzwa kwa kuwa tunataka utajiri wa haraka haraka.Fanya kazi kwa bidii na kwa malengo utafanikiwa ila kutaka cha haraka utakosa haraka pia.
 
nina mashaka na ulokole wako. Yesu hakuwa mfanyibiashara, asilani. Na hakutumia dini wala sinagogi kufanyia biashara. Bali nyumba ya baba yake itaitwa nyumba ya sala, yaonekana mmegeuza kuwa pango la wachuuza fedha!

hahaha, we ni kaduguda kweli. kwasababu ulichoandika hakina hata mantiki. kwa taarifa yako, Yesu anataka watu wawe matajiri, alileta uhuru tutoke kwenye umasikini twende kwenye utajiri. alikuja kutukomboa na utumikishwaji wa shetani anayependa watu waamini kuwa shetani na uchawi ndio huleta utajiri.

Yesu anataka watu waone na kuamini kuwa mtu anaweza kutajirika bila kutumia kiungo cha albino wala kusoma kuran ili kuita majini ya kuiba nyota za watu. ndio maana hata sasa, watu wengi wanatajirika bila hata kutumia uchawi wala nini. wanafanya biashara na wanafanikiwa sana, na Yesu anawasaidia kufanya izo biashara. watu wapinga kristo kama wewe ndio vibaraka wa shetani, hutumiwa na mwovu kupinga mambo ya Mungu. pata hiyo?
 
tunaweza kuassume kuwa hawa DECI ni kama wale watumishi waliopewa Talanta na bwana wao. Mmoja talanta 5000, mwingine 1000 na mwingine 100. Yule bwana aliporudi kutoka safari ya mbali aliwaita wote na kuwauliza "mlifanyia nini talanta zile, leteni mahesabu yenu".

yule wa Talanta 5000 akasema "bwana mimi nilianzisha kituo cha mafuta, duka la viyoyozi na pia nimejenga shule ya chekechekea". Akaendelea "kutoka zile talanta 5000, nimepata faida ya talanta 10,000 so hizi hapa hela zako.

Akamwita yule wa pili, naye akasema "mimi nilianzisha ujasiriamali wa shamba la vitunguu kwenye mabonde ya Tukuyu, na pia nimelima viazi na kutoka zile zile talanta 1000 nimekuwa nikiagiza matunda toka kwa Mkapa huko Lushoto. Kutokana na kiasi kile nimepata faida ya talanta 5000!, hizi hapa fedha zako".

Yule bwana akamuita yule aliyepewa talanta 100 naye atoe hesabu zake. Yeye akaja na kusema "bwana mimi nilijua wewe ni mtu katili, unakula usivyopika, na unavuna usivyopanda. Kwa kukugwaya wewe niliamua kuzifukia ardhini hadi utakaporudi".

Yule bwana akamuuliza "haya nipe kilicho changu". Jamaa akasema "twende mnisaidie kufukua."

Walipoenda na kufukua wakakuta talanta 100 zimeongezeka na kuwa talanta 100,000!

Yule bwana akamuuliza "umewezaje hili?"

Yule mtumishi akasema "nilianzisha mchezo wa Deci!"

Bwana akashikwa na mshangao akamuambia "hakika na wewe ni fisadi!"
It is unclear, but it was used in a study by America's Federal Reserve bank as far back as 1967.
 
This is typical a PYRAMID SCHEME - inapoanza watu wanapata hela - lakini watu wanavyozidi kuwa wengi - inakuwa tabu kuwalipa - INAFAA KUFAHAMU KUWA UNAPOPANDA MBEGU UNACHOVUNA NI MBEGU WALIZOPANDA WENZAKO - NDIO MAANA KUNAKUWA NA TIME SPAN YA KUVUNA - DECI WAO WANAPATA WAPI HIZO HELA ZA KUVUNA? INGEKUWA WANAZICHUKUA NA KUNUNUA LABDA BONDS - ZINAPOMATURE NA FAIDA NDIO WANAGAWA MAVUNO AFADHALI - LAKINI JUST LIKE THAT???? NOT POSSIBLE - NI KWELI KENYA WALISHINDWA NA WATU WALIPOTEZA FEDHA ZAO - HUU NI UPATU NA MWISHO WA UPATU WA NAMNA HII SIO MZURI - ILA KAMA WASEMAVYO"SIKO LA KUFA HALISIKII DAWA" - UBISHI UTAKOMA PALE WATU WATAKAPOLIZWA NA KUONA KUMBE NI UKWELI -
 
Mh!wizi mtupu.huu ni ujasiliamali au?a proffessional entrepreneur hawezi kufanya vimbwanga hivi,tujihadhari sana jamani.
 
Swala la DECI mie nadhani uwaachie wahusika kwa sababu najua kwamba mpaka mtu afikie hatua ya kutoa fedha zake na kujiunga atakuw ana akili timamu.

Kwenda DECI hulazimishwi sasa ambacho chakutia wasiwasi ni nini? Ninchokushauri wewe ni kufanya uchunguzi then ndo uje umwage data zako.
"No Research, No Right to speak"
 
Swala la DECI mie nadhani uwaachie wahusika kwa sababu najua kwamba mpaka mtu afikie hatua ya kutoa fedha zake na kujiunga atakuw ana akili timamu.
Kwenda DECI hulazimishwi sasa ambacho chakutia wasiwasi ni nini? Ninchokushauri wewe ni kufanya uchunguzi then ndo uje umwage data zako.
"No Research, No Right to speak"

Kama tungekuwa tunatumia philosophy kama za kwako hatukuwa na sababu ya kuwa hapa kwani mambo mengi tunayoongea hapa hayatuhusu moja kwa moja, wewe ndio hujafanya research yeyote watu wanachosema ni kweli.

in reality unaweza kuinvest pesa ikaleta faida wanayolipa wapi au kwa jina la yesu kristo ndilo linaleta hizo pesa. usiongee kwa hasira na jaziba kama una data wapi wanawekeza pesa zao na kuzaa kiasi hicho hatuna tatizo na hilo lakini otherwise hatutakaa kimya kusubiri wawaibie wadanganyika ndio tuseme.

Kama wewe ni kiongozi hapo tafuteni njia nyingine kwani sasa hivi mtaanza kujificha baada life cycle ya pyramid yenu kufikia mwisho.
 
Mugerezi,

Wewe ulipanda shilingi ngapi na mpaka sasa umeshavuna bei gani kama faida ...July 08 to date?

Well mimi katika DECI nimepanda 2Million ambazo zimepelekwa kwa laki 2 kila mpando so mpaka sasa zote zimeshatoa mavuno ya kwanza ambayo ukishatoa makato ya 15% nimepata 2,550,000 ambayo ni kutoka July 08 mpaka Jan 09. Nilipovuna nilipanda tena so kati April na June 09 nitavuna tena 2,550,000. Ukilinganisha hizo hela kama ningeziweka bank nisingeweza kupata hiyo faida. Hivyo si lazima uweke mahela kibao weka kidogo ikusaidie katika mambo madogo kama fees za watoto au hata biashara za kawaida.

Mimi ushauri wangu ni kuwa ni kweli hii system haileweki kwa undani lakini office ziko wazi pale mabibo na kwenye attachment zangu za jana nimeonyesha kuna simu wapigie watakupa majibu.

Hawa jamaa wanautaratibu kwani ukilipa unapewa receipt ambayo utakwenda nayo ukienda kuvuna na pia kuna registration ambayo unapewa kitambulisho. Kwenye receipt yao kuna mpaka TIN NUMBER kwahiyo wanafanya kazi ya halali kabisa.

Tufuatilie kwa undani tusiwakatishe tamaa wengine ambao kwa kweli wana mahitaji ya kweli katika huduma kama hizi. Tusiwe sana negative katika kila kitu. Tufuatilie ili kama kuna utata tuambiana.

Thanx
 
hahaha, we ni kaduguda kweli. kwasababu ulichoandika hakina hata mantiki. kwa taarifa yako, Yesu anataka watu wawe matajiri, alileta uhuru tutoke kwenye umasikini twende kwenye utajiri. alikuja kutukomboa na utumikishwaji wa shetani anayependa watu waamini kuwa shetani na uchawi ndio huleta utajiri. Yesu anataka watu waone na kuamini kuwa mtu anaweza kutajirika bila kutumia kiungo cha albino wala kusoma kuran ili kuita majini ya kuiba nyota za watu. ndio maana hata sasa, watu wengi wanatajirika bila hata kutumia uchawi wala nini. wanafanya biashara na wanafanikiwa sana, na Yesu anawasaidia kufanya izo biashara. watu wapinga kristo kama wewe ndio vibaraka wa shetani, hutumiwa na mwovu kupinga mambo ya Mungu. pata hiyo?



.....And then HE said ' Ni rahisi kwa Ngamia kupita katika Tundu la Sindano kulio Tajiri kuingia Ufalme wa Mbingu....!:eek:
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom