Ehud
JF-Expert Member
- Feb 12, 2008
- 2,685
- 337
Spika wa Bunge Mh. Anna Makinda
Na Mwandishi Wetu
Spika wa Bunge, Anna Makinda na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu, Sera na Bunge, William Lukuvi wamewaonya wabunge kuhusu mavazi na kujiheshimu.
Makinda alisema kuwa katika bunge analoliongoza ni marufuku wanawake kujipodoa kupita kiasi na kuvaa sketi fupi (vimini) wakati Lukuvi alionya vikuku na kuwataka wanaume kufunga zipu za suruali.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Makinda na Lukuvi waliyasema hayo Jumanne iliyopita kwenye Semina ya Wabunge iliyochukua siku 10 na kumalizika Alhamisi iliyopita.
Ni kanuni za kawaida kuhusu uvaaji. Unajua siyo heshima mwanamke kuvaa sketi iliyo chini ya magoti, kwa hiyo Makinda alikuwa anasisitiza, kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kiliendelea: Kuhusu vipodozi, Makinda ametaka hizi makeup zisizidi, wabunge wajitofautishe na wahudumu. Wasijipodoe mpaka rangi ibadilike.
Kuhusu kauli ya Lukuvi, chanzo chetu kilisema: Lukuvi ndiye alikuwa mwenyekiti wa semina, siku hiyo aliwaambia kwamba kuvaa vikuku (cheni za miguuni) ni kuwakwaza wanaume.
Akasema wanaume wawe wanafunga zipu, siyo kukurupuka na kuingia viwanja vya bunge hawajafunga zipu mpaka mambo ya ndani yanaonekana.
Mkazo ulitolewa pia kwenye vikao vya bunge. Watu wanaweza kuvaa wanavyotaka kwenye mambo yao binafsi lakini bungeni na kwenye mikutano inayokutanisha nchi lazima wafuate kanuni.
WABUNGE WAAMBIWA WAFUNGE ZIPU - Global Publishers
Na Mwandishi Wetu
Spika wa Bunge, Anna Makinda na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Uratibu, Sera na Bunge, William Lukuvi wamewaonya wabunge kuhusu mavazi na kujiheshimu.
Makinda alisema kuwa katika bunge analoliongoza ni marufuku wanawake kujipodoa kupita kiasi na kuvaa sketi fupi (vimini) wakati Lukuvi alionya vikuku na kuwataka wanaume kufunga zipu za suruali.
Kwa mujibu wa chanzo chetu, Makinda na Lukuvi waliyasema hayo Jumanne iliyopita kwenye Semina ya Wabunge iliyochukua siku 10 na kumalizika Alhamisi iliyopita.
Ni kanuni za kawaida kuhusu uvaaji. Unajua siyo heshima mwanamke kuvaa sketi iliyo chini ya magoti, kwa hiyo Makinda alikuwa anasisitiza, kilisema chanzo chetu.
Chanzo hicho kiliendelea: Kuhusu vipodozi, Makinda ametaka hizi makeup zisizidi, wabunge wajitofautishe na wahudumu. Wasijipodoe mpaka rangi ibadilike.
Kuhusu kauli ya Lukuvi, chanzo chetu kilisema: Lukuvi ndiye alikuwa mwenyekiti wa semina, siku hiyo aliwaambia kwamba kuvaa vikuku (cheni za miguuni) ni kuwakwaza wanaume.
Akasema wanaume wawe wanafunga zipu, siyo kukurupuka na kuingia viwanja vya bunge hawajafunga zipu mpaka mambo ya ndani yanaonekana.
Mkazo ulitolewa pia kwenye vikao vya bunge. Watu wanaweza kuvaa wanavyotaka kwenye mambo yao binafsi lakini bungeni na kwenye mikutano inayokutanisha nchi lazima wafuate kanuni.
WABUNGE WAAMBIWA WAFUNGE ZIPU - Global Publishers