Dear mama....

Pole yaliyokufika, e ndugu magulumangu
Hujafa hujaumbika, hiyo kazi ya mungu
Acha kusikitika, najua una machungu
Mola atamrehemu,alale pema peponi

Dunia ni ya kupita,yeye ametangulia
Na sisi tutafuata, punguza ndugu kulia
Ya mema atayapata,mola atamjaalia
Mola atamrehemu, alale pema peponi

Busara alokwachia, hilo la kujivunia
Fuata yake tabia, pepo utakuja ingia
Sifuate ya dunia, hofu yatakupatia
Mola atamrehemu, alale pema peponi

Futa machozi machoni, mama amepumzika
usiwe mwenye huzuni, najua wataabika
tumuombee kaburini,aishi ka malaika
Mola atamrehemu, alale pema peponi

Pole yako ni amali,kwani yatoka moyoni,
nitailinda ka mali,hujatoa kimatani,
imetulia ka asali,mwangu ikae moyoni,
Nakushukru mkuu,pamoja daima tupo,
 
Pole malenga wetu, kwa msiba wa mama
Amlaze mola wetu, mahala palipo pema
Subira ibaki kwetu, kifo cha mama chauma
Huu ndio mwisho wetu, hakuna wa daima

Pole mkuu magulumangu, RIP mama

DEDICATED TO ALL MAMAZ
Ewe mama mpenzi, shairi nakutungia
Yako mema malezi, sina cha kukulipia
Daima nitakuenzi , hadi mwisho wa dunia
Ewe wangu mzazi, zawadi yangu pokea

Miezi tisa tumboni, mwako ulivumilia
Chakula hukutamani, udongo ulijilia
Usiku ni hamkani , usingizi ulipotea
Umbo lako la thamani, shepu ilikupotea

Ladha hukujionea, ukila ulitapika
Homa za kujirudia, hakika uliteseka
Miezi tisa katimia, uchungu nikakutwika
Ulichukia dunia , wakati mimi natoka

Mara ulifurahia, kwa mimi kunipakata
Wala hukujutia, jina zuri uliniita
Nikaanza na kulia, usingizi hukupata
Uliacha ya dunia , huduma niweze pata

Malezi ukayatunza, maisha niyakabili
Mengi uliyonifunza, sasa nimeyakubali
Nina mengi kueleza, muda haunikubali
Mama sitotelekeza, wosia wako ni mali

Kaditamati wa tama, kalamu naweka chini
Tuwaenzi wetu mama, hima hima jamani
Hata akiwa rikwama, walisema wa zamani
Vibaya wakitusema, basi tumo laanani

Sina la kuongezea,yote umeyatimiza,
kila mtu analegea,kusikia zako miza,
nami ndo nazipokea,moyoni kuzitimiza,
Wewe ni wangu kaka,ndugu wa fani na vina,
 


Magulumangu huishi nikosha , kwa yako matamu maneno
Mimi leo tena wanikosha, kwa yako kwa mama maneno
mama nami huitwa , mamayo wamuita kwa yako maneno
mimi kama mama nahakiki, mama kapokea yako maneno

Samahani Magu naishia, shairi darasa bado napewa
Lizzy mwalimu nasifia, kwa uvumilivu wote napewa….



Will be cont...
 
Duniani we ndo MUNGU wangu mama/
jinsi navyokupenda moyoni hutanihama/
chozi lako linapotoka moyo unanichoma/
tangu a,e,i,o,u vidudu niliposoma/
hadi chuo kikuu maujanja nasoma/

huwa nanumia unapokuwa mbali/
ninapokumiss nalia kama sina akili/
kitu gani nikupe cha kifahari/
hela,nyumba,au gari la kifahari/
naomba usinitenge hii maisha kamari/
 
kamwe sijekuchelewa,kwako mama ninasema,
miezi tisa kulelewa,na wewe tumboni mama,
maneno ulirushiwa,mbele na ulitizama,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

Wengi waliyasema,ni utazaa jambazi,
Jibu kwao hukusema,maneno yako ni tenzi,
Ulienda kwa neema,ukayaacha mapenzi,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

Najua mama ulipo,umelala kwa salama,
Muumba daima na yupo,zake mbawa dhahama,
watoto wako na wapo,kukukosa we daima,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

najua nawahi mama,kukwambia siku yako,
kumbuka we ulisema,kuwahi chelewa mwiko,
ulienda kwa heshima,zote mpaka na uliko,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

sina zaidi kukupa,mpaka siku tuwe wote,
ila kwako ulinipa,mapenzi wakati wote,
miezi tisa ulinipa,tumboni wakati wote,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

maua nimeyaweka,tayari siku ifike,
ulipo kuyatandika,harufu kwako ifike,
siku pia nitafika,mungu na anialike,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

Nakumbuka lipotoka,chozi lilitiririka,
miaka kupukutika,kichwani nakukumbuka,
tabasamu nakumbuka,kabla haujatoka,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

Chozi laanza nitoka,anifuta malaika,
hata yeye akumbuka,siku ulipong'atuka,
mafuta alikupaka,kwa heri hutafufuka,
Hii ndio siku yako,ishiri sita wa tano,

Tukiamua kueleza , mateso alopitia
Kurasa tutamaliza, wala hatutoishia
Mama hana mwenza, aspirin nakwambia
Naiona miujiza, kwa yote alovumilia

Wakwangu nae pia, akhera katangulia
Magulu kakumbushia, namimi namalizia
Dua ninamuombea, daima taendelea
Urithi aloniachia , bado ninajivunia

Na nyie ndugu zanguni, mnaniliza jamani,
Ninaumia moyoni, hili pigo maishani,
Jamani sana poleni, yatoka kwangu moyoni,
Mametu hawa wawili, walale pema peponi.

Walale pema peponi, Semeni wote amina,
Waimbe sana mbinguni, itikieni amina,
Wakae nayo amani, Semeni tena amina.
Wote tena kwa sauti, tuitikie amina
 
NA HAKUNA KAMA MAMA

Malenga mmeandika, mama kumuelezea
Na mimi najumuika, machache kuongezea
Hakika twafarijika, malezi waliotugea
Na hakuna kama mama, mama ndiye namba wani

Na hakuna kama mama, malenga twakubalia
wapata nyingi dhahama, usiku twawalilia
Hawastahili lawama, mengi wametupatia
Na hakuna kama mama, mama ndiye namba wani

Bila mama duniani, tungepata shida nyingi
Leo tupo furahani, sababu wao msingi
Mama yangu natamani, uone miaka mingi
Na hakuna kama mama, mama ndiye namba wani

Mama umejaaliwa, wema uliozidia
Nahisi changanyikiwa,roho itapokimbia
Nitageuka mfiwa, milele takulilia
Na hakuna kama mama, mama ndiye namba wani

Mdau Yakuonea, Salamu nakutumia,
Kofia nakuvulia, ushairi waujua,
Vina unavipangia, kadhalika mizania,
Hakika wewe malenga, malenga ulotukuka.

Hakika wewe malenga, malenga ukotukuka,
Mashairi wayapanga, yametulia hakika,
Hakuna atayepinga, unazi sijauweka,
Hakika wewe malenga, malenga ulotukuka.
 


Magulumangu huishi nikosha , kwa yako matamu maneno
Mimi leo tena wanikosha, kwa yako kwa mama maneno
mama nami huitwa , mamayo wamuita kwa yako maneno
mimi kama mama nahakiki, mama kapokea yako maneno

Samahani Magu naishia, shairi darasa bado napewa
Lizzy mwalimu nasifia, kwa uvumilivu wote napewa….



Will be cont...

Asha D salamu,

Hauvumi lakini umo..... kaza buti mama!...........Nakufagilia!
 
Pole sana ndg, kilichobaki ni wewe sasa kujiandaa kiroho ili uwe safi muda wote. Kweli mama is the best how ever she is! Heshima kwa wamama woooote popote pale walipo including myself:dance::dance::dance:
 
NDUGU YANGU ASPRIN

Asante nakushukuru, malenga ulokomaa
Watupa tungo za nuru, na mengi yenye kufaa
Liongoze hili duru, wewe kweli kifaa
salamu nazipokea, ndugu yangu asprin

Ningali ni mwanafunzi, ushairi sijajua
Natamani niwe mjuzi, lugha kudadavua
Mola naomba nienzi, nichanue kama ua
Salamu nazipokea, ndugu yangu asprin

Asprin u mkongwe, hilo wote twatambua
Hufanyi yenye mizengwe, na fani unaijua
Tuongoze kwenye ngwe, fani ipate kukuwa
Salamu nazipokea, ndugu yangu asprin

Na pale kwenye makosa, naomba nisahihishe
Tafadhali anza sasa, nisije patwa kasheshe
Tupende yetu sanaa, ujumbe tuufikishe
salamu nazipokea, ndugu yangu asprin

Hapa ninaweka nanga, wewe uwangu mwalimu
Nitakuja hata Tanga, nipate yako elimu
Mola sikupe majanga, maisha yako yadumu
salamu nazipokea, ndugu yangu asprin


Mdau Yakuonea, Salamu nakutumia,
Kofia nakuvulia, ushairi waujua,
Vina unavipangia, kadhalika mizania,
Hakika wewe malenga, malenga ulotukuka.

Hakika wewe malenga, malenga ukotukuka,
Mashairi wayapanga, yametulia hakika,
Hakuna atayepinga, unazi sijauweka,
Hakika wewe malenga, malenga ulotukuka.
 
What is more important she found joy being who she was..........................nobody forced her into womanhood.......she knew a calling was hers alone when it came knocking at her door...........................................................
 
Na nyie ndugu zanguni, mnaniliza jamani,
Ninaumia moyoni, hili pigo maishani,
Jamani sana poleni, yatoka kwangu moyoni,
Mametu hawa wawili, walale pema peponi.

Walale pema peponi, Semeni wote amina,
Waimbe sana mbinguni, itikieni amina,
Wakae nayo amani, Semeni tena amina.
Wote tena kwa sauti, tuitikie amina

Dua zako twashukuru, amina twaitikia
Hata awe zeru zeru , Mama ndio dunia
Mama tukimkufuru, maisha tayachukia
Utazimaliza duru, dhalili utaishia
 
Kloro nimesikia, mama nguzo ya dunia
Utakuja jijutia, mama sipomsikia
Laana akikuachia, Maisha yatafifia
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Mama akikasirika, hima omba msamaha
Kweli utaabika, mama akikosa raha
Mwilini utadhurika, ubaki na majeraha
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Mama akifurahika, twapata nyingi thwawabu
Maisha yatanyooka, tazama kwenye vitabu
Na katu hutopotoka, usiwe ni mwenye tabu
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Mama zetu tuwaenzi, kwa mema yao malezi
Hawa kwetu ni wajenzi, tuwape nyingi pongezi
Tusifanye ya ushenzi, mama pokea mapenzi
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru


Dua zako twashukuru, amina twaitikia
Hata awe zeru zeru , Mama ndio dunia
Mama tukimkufuru, maisha tayachukia
Utazimaliza duru, dhalili utaishia
 
Kloro nimesikia, mama nguzo ya dunia
Utakuja jijutia, mama sipomsikia
Laana akikuachia, Maisha yatafifia
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Mama akikasirika, hima omba msamaha
Kweli utaabika, mama akikosa raha
Mwilini utadhurika, ubaki na majeraha
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Mama akifurahika, twapata nyingi thwawabu
Maisha yatanyooka, tazama kwenye vitabu
Na katu hutopotoka, usiwe ni mwenye tabu
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Mama zetu tuwaenzi, kwa mema yao malezi
Hawa kwetu ni wajenzi, tuwape nyingi pongezi
Tusifanye ya ushenzi, mama pokea mapenzi
Mama zetu ni dunia, hata awe zeruzeru

Ubarikiwe yakuonea, kwa mema maneno
Wengi tumekusikia, umenena kwa mifano
Uwazi umetuwekea,wala hukuuma meno
Mama ndie malkia , ameshinda mashindano

Sina la kuongezea, yote umeyamaliza
Atakae puuzia , dunia itamfunza
Ewe ulo maridhia, haya maneno sikiza
Alotupa yakuonea, yakutoe kwenye giza
 
Kila nikifikiria, machozi yanizidia
Hebu Kloro fikiria, mangapi walipitia
Shida ziliwazidia, bado walivumilia
Mama zetu mama zetu, bado ningali nalia

Roho taweka rehani, mamangu asidhurike
Napenda yake amani, mabaya yasimfike
Nasema kweli jamani, bora hai mnizike
mama zetu mama zetu, ningali bado nalia

Nashindwa hata andika, sijui niseme nini
Mama yangu kwa hakika, mfano wake sioni
Nitazusha patashika, mama kipatwa huzuni
Mama zetu mama zetu, ningali bado nalia

Ubarikiwe yakuonea, kwa mema maneno
Wengi tumekusikia, umenena kwa mifano
Uwazi umetuwekea,wala hukuuma meno
Mama ndie malkia , ameshinda mashindano

Sina la kuongezea, yote umeyamaliza
Atakae puuzia , dunia itamfunza
Ewe ulo maridhia, haya maneno sikiza
Alotupa yakuonea, yakutoe kwenye giza
 
Mkuu kloro yaani nimejikuta suddenly nime-fall in love na mashairi sikuwahi kuandika mashairi maishani mwangu lakini niliamini naweza na nilipojaribu kuandika nimejikuta niko in love
 
Kila nikifikiria, machozi yanizidia
Hebu Kloro fikiria, mangapi walipitia
Shida ziliwazidia, bado walivumilia
Mama zetu mama zetu, bado ningali nalia

Roho taweka rehani, mamangu asidhurike
Napenda yake amani, mabaya yasimfike
Nasema kweli jamani, bora hai mnizike
mama zetu mama zetu, ningali bado nalia

Nashindwa hata andika, sijui niseme nini
Mama yangu kwa hakika, mfano wake sioni
Nitazusha patashika, mama kipatwa huzuni
Mama zetu mama zetu, ningali bado nalia

Nasaha naziongeza, kwa walo ndani ya ndoa
Wenza wasijetuponza, mama tukamshushua
Mama yeye ni kwanza, wengine wanafatia
Sitochoka kuhimiza , mama namfagilia

Hisia zisikubebe , ndugu yangu yakuonea
Kula tena ushibe, uikabili dunia
Kwenye pengo tulizibe, Mama atakusifia
Uiname kama kobe, anapotunga sheria

Jihadi yahitajika , mama kumtetea
Bunduki nimejitwika, ya shairi sikia
Nawatafuta mateka, mama walomsusia
Tuwapige mweleka, njia kuwanyooshea.

Ni jukumu letu sote, JF na dunia
Slaa hata Kikwete, umuhimu waujua
Tusimameni kidete, mama kumhudumia
Tutabarikiwa wote , na muumba wa dunia
 
Back
Top Bottom