Magulumangu
JF-Expert Member
- Jan 7, 2010
- 3,047
- 452
- Thread starter
- #21
Pole yaliyokufika, e ndugu magulumangu
Hujafa hujaumbika, hiyo kazi ya mungu
Acha kusikitika, najua una machungu
Mola atamrehemu,alale pema peponi
Dunia ni ya kupita,yeye ametangulia
Na sisi tutafuata, punguza ndugu kulia
Ya mema atayapata,mola atamjaalia
Mola atamrehemu, alale pema peponi
Busara alokwachia, hilo la kujivunia
Fuata yake tabia, pepo utakuja ingia
Sifuate ya dunia, hofu yatakupatia
Mola atamrehemu, alale pema peponi
Futa machozi machoni, mama amepumzika
usiwe mwenye huzuni, najua wataabika
tumuombee kaburini,aishi ka malaika
Mola atamrehemu, alale pema peponi
Pole yako ni amali,kwani yatoka moyoni,
nitailinda ka mali,hujatoa kimatani,
imetulia ka asali,mwangu ikae moyoni,
Nakushukru mkuu,pamoja daima tupo,