DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

Bado sitta! Uraisi mchezo 2015 sina hamu mungu uniweke hai; ikiwezekan tuhairishe miaka ilitufanya huo uchanguzi
 
Tuhuma za, EPA, MEREMETA, RICHMOND na MWAKYEMBE kulishwa sumu zote ni uongo:lol::lol::lol:. Tanzania ni zaidi ya uijuavyo!!!!
 
Bado silioni kosa la DCI Manumba wana JF, Huyu Mwakyembe + Sitta ni wanafiki, wazandiki, wachochezi, tena wakuchomwa moto kabsa.

My take; Mwakyembe na Sitta kama wanaufahamu ukweli wa hili jambo kwa nini hawataki kufunguka kwa wananchi?
Wana JF swala la kuwekewa sumu sio jambo dogo la kuweza kukaa kimya kama anachofanya Mwakyembe, si aseme? unafiki hata mungu hapendi.
 
Wanabodi,
Hivi hili ni chunguzo la kwanza la namna hiyo kufanywa na intelijensia zetu?
Mlishawahi kupata aina ile ya matokeo mnayotarajia?

Hii mimi haijanishangaza bali nawashangaa wanaoshangaa matokeo haya.
 
DCI anachosema "hajarishwa sumu" iki ndo anachokipinga yawezekana tuuma ilikuwa "kulishwa sumu" kumbe "kapuliziwa sumu"!! Hajaonyesha kupinga kuusu Mwakyembe kusumbuliwa na sumu iliyoingia mwilini bali anapinga "kulishwa sumu".Haki tz iko wapi!!
 
Mkuu Pasco, kwa vile tukio hili lina hisia kali na limeleta sintofahamu katika jamii nina uhakika DCI ametoa amaelezo hayo kwa sababu hizo. Maelezo yake hayajitoshelezi na yanazidi kuchochea hisia zaidi ya kufafanua.

Tungeelewa endapo DCI angetuambia kuwa Dr Mwakyembe hakuridhia kueleza kinachomsumbua. Hiyo ni haki ya mgonjwa.
Hakufanya hivyo. Kwa maana nyingine natural justice haikutendeka. Amechukua kesi, ameendesha mashitaka na ametoa hukumu bila ya kusikiliza upande wa pili.

Dr Mwakyembe atakaposimama na kutoa maelezo na endapo atasema amelishwa sumu, basi DCI na serikali hawatakuwa na pa ksuimama kwasababu 'the disclosure rights lies with the patient' nasi tutachukua 'from horse mouth'.
Unapompa right ya ku disclose tatizo lake umetupa right ya kuamini atakachosema.
Right ni yake na haina mjadala lakini mazingira lazima yatazamwe.Suala la Dr Mwakyembe ni zaidi ya right za mgonjwa

Lakini pia usisahu kuwa serikali imekuwa inatupiana mpira, na DCI ni sehemu ya serikali. Kusikia tu kutoka kwao bila kusikia kauli ya Mwakyemebe kupitia kwao ni tatizo kubwa. Tulitegemea ima waseme wamepata au wamekosa ushirikiano ili tujue natural justice imefanyika. Alichokifanya DCI ni kuchochea moto na si kuzima.
Mkuu Nguruvi3, kumsababishia maumivu binadamu yoyote ni kosa la jinai, hivyo kumpiga mkeo pia ni kosa la jinai. Jirani yako kasikia kelele ya mkeo anakula kichapo na kusikia sauti yako ukisema "leo nitakuua wee mwanamke"!. Jirani katoka mbio kukuripoti polisi kuwa kuna jinai inatendeka jirani kwake!. Polisi na defenda mbio nyumbani kwako ili kuzuia jinai!.

Walipofika wakakuta ugomvi umeisha wakauliza kama kuna tatizo, wewe ukasema hakuna tatizo, unadhani polisi watafanya nini?. Hawata fanya lolote kwako wala kwa mke wako, bali huyo jirani yako aliyeripoti tukio, watarudi nae kituoni kumchukua maelezo!.

Aliyewekewa sumu ni Mwakyembe hajaripoti polisi kuhusu kuwekewa sumu. Aliyepayuka hadharani kuhusu jinai ya sumu ni jirani (Sitta). Polisi wamechukua maelezo ya Sitta na kufanya uchunguzi, wakakuta hakuna jinai ya sumu!. Mwakyembe mwenyewe wala familia yake hawajalalamikia sumu!. Kama ambavyo mkeo hajalalamikia polisi kuhusu kichapo alichokula!.

Sasa kinachofuatia ni Jirani kushitakiwa kwa kuisumbua polisi na kwa case ya Mwakyembe sio tuu kuisumbua polisi bali uchochezi ili wananchi waichukie serikali yao kwa kuiona ni serikali ya wauaji!.

Mkeo aliyekula kichapo kweli, kama hajakwenda kushitaki polisi, then wewe hauna kesi yoyote japo kichapo ulitoa!.

Mwakiyembe anaumwa, hajalalamikia kupewa sumu. Jirani ndio anae eneza uvumi wa simu ili kuwanyooshea kidole mahasimu wake wa kisiasa!. Sasa kwa vile issue ilikuwa ni kupewa sumu, imethibitika sio sumu!. Mwambieni jirani sasa na atoe uthibitisho, ila its high time Dr. akirudi toka matibabu ya India awaambie Watanzania ukweli wa anachoumwa!.
 
Je itakapokuja kujidhihirisha kwamba kinachomsumbua Dr. Mwakyembe ni Sumu awe amelishwa au aliwekewa kwa njia yoyote ile, atakuja kusemaje! Mijitu mingine bwana, itakuja kupelekwa The Hague bure kwa makosa ya watu wengine kutokana na ujinga wao!

Jamani ushahidi wa tuhuma hiyo haujapatikana!! na vipimo havioneshi!! na mgonjwa hajakiri kulishwa mihogo michunguu!! Sasa tulitaka serikali iseme uzushi?!!
 
hahahaha!!!!!!!!!!!!

Naona sasa tuko pamoja, yani kwenye ukurasa mmoja.

Kwa kifupi hii issue imefungwa rasmi, mliombwa mwende mkatoe ushahidi kama mnao lakini kumbe ilikuwa magilini tu.

Sasa mwendo mdundo, hahahahaha

T 2015 ENL
 
Mkuu Ngongo, the disclosure rights lies with the patient. Hivyo hilo ni jukumu la Mwakyembe mwenyewe!.

hivi huu ni uchunguzi au kuchukua taarifa kutoka wizara ya afya? Hivi waziri mkuu alishindwa nn kusema kwamba mwakyembe hajalishwa sumu.?
 
Well said! Anavuna alichopanda. Polis wamfungulie mashitaka Sita kwa kuhatarisha amani ya nchi na kutoa maneno ya uchochezi.

Hahaha, huyu mwalimu wa Pasco ni mnafiki sana:-

1. Alipika report na kujifanya kuwa ameisoma nusu bungeni na nusu ni siri ya kamati, kumbe kamba tupu
2. Alidai kuwa once akirudi kutoka India ataweka mambo hadharani lakini kaja kakaa kimya, huyu ni mnafiki hatari...

`sasa nadhani watanzania wote tuko kwenye page moja, safi sana Manumba na Wizara ya Afya....hahahhaha....
 
Wengine tunataka kulazimisha matokeo ya uchunguzi vile tunataka.
kumbuka kwenye uchunguzi huu tulitegemea ndiyo au hapana. sasa jibu limekuja hapana tunalalamika. Mwakyembe aseme mwenyewe anaumwa nini, kama alikanyaga moto aseme pia, kwani wangapi wanaumwa kama yeye na mbona hawakulishwa sumu?
 
hii ni kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari mchana wa leo. Katika maelezo yake, dci anasema kwamba:

"kutokana na uchunguzi wa kipolisi ulioshirikisha wizara ya afya na ustawi wa jamii, hakuna ushahidi juu ya hilo".

Alipoulizwa na waandishi wa habari:

je, dr. Mwakyembe anasumbuliwa na maradhi gani?


dci alijibu kwamba:

"kazi ya jeshi la polisi sio kuchunguza maradhi bali kuchunguza tuhuma, na baada ya uchunguzi wake kwa kushirikiana na wizara ya afya na ustawi wa jamii, jeshi la polisi limebaini kwamba tuhuma kwamba dr. Mwakyembe amelishwa sumu hazina ukweli
."
unategemea dci asemeje,kwanza intelligensia yake sufuri,mtu ataingiaje na radioactive material nchini bila yeye kujua si bora tuishi hivyo hivyo,hawezi sema kwa sababu au anajua game nzima au kuna uzembe mkubwa kiutendaji.MBONA REPORT ZINGINE ZA INTELIGENSIA WAKATI WA MAANDAMANO ZINATANGAZWA AU NI KUPIKA
 
hivi huu ni uchunguzi au kuchukua taarifa kutoka wizara ya afya? Hivi waziri mkuu alishindwa nn kusema kwamba mwakyembe hajalishwa sumu.?
Mwenye uwezo wa kusema kuhusu jinai au laa ni DCI tuu. Na kama wangekuta jinai then wangepeleka kwa DPP ndiye pekee mwenye kuamua aendeshe mashitaka au la. Na DPP angeamua kuendesha mashitaka, bado mahakama ingesikiliza ushahidi wa DPP na kuamua kama kuna kesi ya kujibu au laa!.

Tuna kitu kinaitwa the principle of separatiob of powers, PM sio kila kitu and has nothing to do with this!.
 
Mkuu Nguruvi3, Walipofika wakakuta ugomvi umeisha wakauliza kama kuna tatizo, wewe ukasema hakuna tatizo, unadhani polisi watafanya nini?. Hawata fanya lolote kwako wala kwa mke wako, bali huyo jirani yako aliyeripoti tukio, watarudi nae kituoni kumchukua maelezo!.

Aliyewekewa sumu ni Mwakyembe hajaripoti polisi kuhusu kuwekewa sumu. Aliyepayuka hadharani kuhusu jinai ya sumu ni jirani (Sitta). Polisi wamechukua maelezo ya Sitta na kufanya uchunguzi, wakakuta hakuna jinai ya sumu!. Mwakyembe mwenyewe wala familia yake hawajalalamikia sumu!. Sasa kinachofuatia ni Jirani kushitakiwa kwa kuisumbua polisi na kwa case ya Mwakyembe sio tuu kuisumbua polisi bali uchochezi ili wananchi waichukie serikali yao kwa kuiona ni serikali ya wauaji!.

Mwakiyembe anaumwa, hajalalamikia kupewa sumu. Jirani ndio anae eneza uvumi wa simu ili kuwanyooshea kidole mahasimu wake wa kisiasa!. Sasa kwa vile issue ilikuwa ni kupewa sumu, imethibitika sio sumu!. Mwambieni jirani sasa na atoe uthibitisho, ila its high time Dr. akirudi toka matibabu ya India awaambie Watanzania ukweli wa anachoumwa!.
Mkuu Pasco, nikukumbushe kuwa kuna mtu aliwahi kueneza tuhuma kuhusu wewe nadhani unakumbuka. Yeye alisema pasco ..... kwa kutumia vigezo na hisia.

Wewe ulikuja hapa jamii forum na kutoa maelezo ya kujitosheleza kuwa huna hulka ilitosemwa, ukaenda mbali na kutoa ushahidi wa wewe kuanzia makutopora, chuo kikuu n.k. Hukusema tu 'Sina tabia hiyo' bali ulienda mbali ku-prove beyond doubt.
Serikali imesema 'hakuna sumu' , je inatosha kukanusha madai mazito kama hayo ya maisha ya raia kiongozi?

Pili, kumbu kumbu zinaonyesha kuwa Dr Mwakyembe ameshawahi kufikisha madai ya ajali, na yale mazito sana ya kuuawa kule Morogoro. Serikali haijashughulikia madai hayo. Hii inaondoa kabisa hoja ya kuwa 'hajaripoti polisi' kwasababu hata angeripoti bado hakuna utashi wa kushughulikia kwasababu madai yake yanawagusa watu wazito waliomo na waliostaafu na waliojiuzulu.

Kama madai ya Sitta ni uongo serikali inawajibu wa kumshataki. Haijafanya hivyo na haitafanya hivyo kwa kujua kuwa Sitta anaweza kutoa ushahidi utakaoleta utata. Ndiyo maana PM na kila mkubwa wa serikali anaogopa kuzungumzia tuhuma hizo.

Huwezi kujua mazingira yanayomlazimisha Mwakyembe kukaa kimya. Unakumbuka Said Kubenea alipotoka India alitaka kuitisha mkutano na wanahabari! unajua nini kilitokea hadi leo hajazungumzia suala hilo? Walikamatwa vibaka ili kumzuia 'technically' asizungumzie suala hilo.

Kama madai ni kuisumbua Polisi, iweje polisi hiyo hiyo isisumbuke wakati wa utata wa ajali na tuhuma za mauaji Morogoro?
Kwanini serikali ichague mambo ya kushughulikia yanayomsibu Mwakyembe na si maisha yake as whole!
Hadi tutakapopata ukweli wa jaribio la kumuua kule Morogoro hatutakuwa na imani na taarifa yoyote hasa kutoka Polisi kuhusiana na Mwakyembe! Nitty gritty

Na mwisho, endapo serikali imethibitisha kuwa sio sumu, ilitakiwa iende mbali zaidi. 'Sio sumu' ni kauli inayoweza kutolewa na mtu yoyote. Haya ni madai mazito sana na tayari yapo vichwani mwa watu, huwezi kuyafuta kwa neno moja bila kukata kiu kwa maelezo yanayoeleweka.

Wewe hukusema 'mimi siyo..' ulienda mbali zaidi. Hapo mkuu huoni kuna upungufu kwa serikali hasa tukizingatia unyeti wa suala lenyewe
 
Ni kweli hata Kubenea hakumwagiwa maji yenye sumu kwenye uso wake. Hata Jerry Muro pia alimuomba rushwa ya Ml 20 ndg Wage. yote haya ni ya kweli kabisa
 
Tumuombee jamani apone, kisha tutajua mengi yaliyojificha kwa sasa ni mapema mno kusema kama alivyosema manumba, sasa akirudi mwenyewe na kusema kinaachomsibu akina manumba wataficha wapi nyuso zao? Nakuombea kwa Mungu upone haraka ili uendelee na majukumu ya kulijenga Taifa.
 
Polisi HAWASUBULIWI NDO KAZI YAO kulinda usalama wa raia na mali zao.. hata ka ripoti kauongo/utani ni lazima kafanyiwe kazi kama vile ni KWELI hadi wathibitishe vinginevyo...... Jamani hii ndo raha ya kulindwa..... kwa wenzetu ..mtu akilewa anapiga simu polisi.. atatoa visingiizio kibao ajuavyo kwamba hawezi kuendesha gari au kapotea na atapelekwa kwake.... Hivi ndivyo wanavyopaswa kufanya kazi....

Kuhusu ripoti ya Manumba yeye alipaswa kuripoti kwamba tuhuma hizo za kulishwa sumu zina kesi ya kujibu au hakuna kesi kwa vielelezo vya madaktari sio mujibu wa makachero wake kwamba hawajaona!!!!!..SOMETHING IS FISHY SOMEWHERE!!! Je watuhumiwa ni kina nani? ambao hawana kesi.. I think this will remain an unsolved case for many years mpaka Mwakyembe aanze kutupa mwanga
 
Back
Top Bottom