DCI Manumba: Mwakyembe hajalishwa sumu!

O-ho, Mwakyembe analo...Sasa ni moja, achague kati ya kusema ukweli kuhusu afya yake au kuwapa ushindi maadui wake. Sisi yetu macho. Siasa bana...
 
Serikali makini itamshughulikia Sitta haraka iwezekanavyo, scrap him his ninisterial positions na kumpandisha kizimbani kwa kosa la "uchochezi"!.

Kwa hiyo Serikali ipo makini katika hili linalomuhusu SITTA Lakini PINDA NA J. K waliposababisha wagonjwa kufa mahospitalini kwa kukosa huduma; pale serikali ilikuwa siyo MAKINI!!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

ACHENI TUSEME....................MNAPENDA KUTUMIA VITISHO ILI KUFICHA UKWELI. LAKNI MKOMBOZI ATAZALIWA NA KUTUKOMBOA....... ACHENI NISEME HATA MKI.......


MIZAMBWA
INANIUMA SANA!!!
 
Hivi polisi hao hao zile zile tuhuma alizotoa kwamba alshabaab wanataka kumuua walizifanyia kazi na kutoa maelezo km walivyoharakisha kukanusha hili la kulishwa sumu?
 
In a country notorious for impunity and pervaded with massive corruption like Tanzania, such facile answers from authorities are not entirely unanticipated. Whether DCI's remarks are believable or not, Sitta should equally be pinned down to elaborate and corroborate his poison allegations so that to balance things.
 
Sita ana kiherehere, alolishwa sumu hajasema yeye akaropoka! Hivi kweli Mwakyembe apewe sumu asiseme?. Mimi nionavyo labda alipewa kemikali fulani au anaumwa ngoma au sukari!. Kuna mgonjwa wa kisukari namfahamu ukimwona ngozi yake nayo inatoa ukurutu!.

Si hivyo anaogopa kuongea tena. Kuhusu EPA aliongea mkampa SUMU je, leo akiongea na hili si mtammwagia pilipili machoni awe kipofu asione tena uovu mkifanya................................

MWACHENI SITTA ASEME, SI WAMEFANYA KWELI...................



MIZAMBAWA
INANIUMA SANA!!!
 
Jeshi la polisi ni kama punda tu. kama muongozaji akisema nenda kushoto, punda lazima aende. Hata katika hili wachunguzi ambao ni polisi wakiambiwa watoe majibu fulani hawawei bisha.
 
mi nadhani mhusika aweke wazi kinachomsumbua,kwani anaogopa nini?si wana mafaili ya hospital wayaweke wazi! mi nafkiri mda si mrefu atajitokeza hadharani na kuzungumza
 
wote ni wasanii tu hawa,polisi nao wanatumiwa na wanasiasa sana,so si watu wakuleta majibu yenye akili
 
Siri aliyonayo Mh Mwakyemba ndiyo inayommaliza sasa,bora siri ile ya Richmond angeitoa tu watu tujue,atakufa siku siyo zake,mafisadi wana nguvu za ajabu!!!
 
Huyo Kanumba aweke humu vipimo vya yeye kuwa na uhakika wa uchunguzi wake.
 
Binafsi katika hili sijaona kosa la DCI Manumba, Manumba anadai kwa mujibu wa uchunguzi wao wamegundua mwakyembe ajapewa sumu, sasa ni wakati kwa Mwakyembe kujitokeza hadharani na kusema anasumbuliwa na nini!

Hila katika hili sagga kuna kitu kimejificha kwa pande zote (Mwakyembe vs Government) siku si nyingi tutasikia mengi kutoka pande zote. Lets wait
 
In a country notorious for impunity and pervaded with massive corruption like Tanzania, such facile answers from authorities are not entirely unanticipated. Whether DCI's remarks are believable or not, Sitta should equally be pinned down to elaborate and corroborate his poison allegations so that to balance things.
Tukubali sisi kama wananchi lazima tujue tunataka nini! Tunataka tu uthibitisho kama Mwakyembe kala sumu tu? Mbona inaweza kuja ripoti ya kupikwa mkachoka kuwa ni kweli ni sumu ila inapatikana kwenye vyakula na kama una allergy flani basi utadhurika! Then tutauliza nini? Polisi wamejibu pressure ya kwanza ili pressure ikizidi waseme hakula sumu bali allergy(may be)! Lazima tutengeneze base ya maswali ili si Polisi wala Mwakyembe wataocheza na ukweli kwa maslahi flani! All in All Mwakyembe amebaki na goli lisilo hata na kipa ni kupasia tu nyavu! Kama ni mjanja ajibu haraka kuhold pressure ya wananchi baada ya DCI kutoa ripoti!
 
Ingawa siombei kwa binadamu yamtokee kama yanavyoomtokea mwakyembe, mi nahisi ni zambi alizochuma kwa kutotuambia kilichokuwa kinaendelea richmond na ndio maana anashindwa kutuambia kuwa ni nini kinachomsumbua zaidi ya rafiki yake kumsemea kuwa amelishwa sumu, kama kweli mwakyembe anaufahamu ugonjwa wake atoke hadharani na kuuambia umma ni nini kinachomsumbua la sivyo mimi nitaamini ya dci manumba
 
Iko hivi Dr Mwakyembe ni kweli kabisa hakuwekewa sumu kwenye chakula. Sumu iliingiaje kwenye mfumo wa kimwili wa Harrison? Alikuwa akiviziwa sana na jamaa walimwekea sumu kwenye sabuni ya kunawia mikono Dodoma, mara baada ya kuitumia ile sabuni ilitoweka. Cartel ya waliohusika kufanya uharamia huo wa kumtegeshea sumu Mwakyembe inaongozwa na Mbunge wa Monduli, ambaye bunge lilimlazimisha aachie ngazi nafasi ya uwaziri mkuu. Wahusika wote waliisha lipwa kwa kazi hiyo na wana kiapo cha kutosema kwa mtu yeyote.
Ah! kweli kwa vile wewe ni Kasisi Rev Fr nitakuamini kabisa!
 
Je kuna aliyetaraji huyo DCI nani sijui aseme hivi

Manumba said:
"Mwakyembe amelishwa sumu, tena kalishwa sumu mbaya kabisa ambayo inaua taratibu na kabala hujafa huifanya ngozi yako imomonyoke na uchakae uwe kama takataka, tena sumu yenyewe inahitaju ujuzi mkubwa kuigundua ikiwa mwilini kwani mtu akishakula tu chemical composition zake hubadilika hivyi si rahisi kugundua ni sumu ya aina gani.

Uchunguzi zaidi umebaini waliohusika na kumlisha ni wale vinara waliojeruhiwa katika sakata la Richmond. Kwa kuwa bado wana mihela mingi na wanafahamu siri nyingi za kaka mkubwa hao watu hawatashughulikiwa labda kama Mwakyembe na wenzake wanaojifanya wanapambana na ufisadi waendelee kupambana nao.

Lakini sisi kama jeshi la polisi tunatoa wito kwa Mwakyembe na jamaa zake kuachana na hao jamaa kwani ni hatari sana, na bila kuficha tunapenda kumwambia Mwakyembe ana bahati sana, ashukuru Mungu wake alikuwa hajalala la sivyo angekiona cha mtema kuni, hicho kilichompata ni ni sawa kuonjeshwa karanga mbili na muuza karanga mwenye kapu la kilo ishirini. Sio sisi polisi tu ambao hatuwawezi hata hii nini hii yenyewe baraza la mawaziri hawaiwezi"
 
Back
Top Bottom