DC wa zamani hoi kitandani

Tatizo lake nadhani alikuwa anasema sana na kuitetea serikali lakini hakufikiria kuiba, angeiba asinge omba msaada wa serikali angejitibia mwenyewe....
 
sitokaa nimsahau alitaka kunifukuzisha kazi nikiwa nafanya kazi kwenye ndege akawa anasafiri kwenda mwanza akaenda kukaa kwenye sit akiwa na mabegi yake makubwa mawili,kwa wanaojua pale kati kuna emrgency exit ambayo wakati wa demo tunaomba wenye mzigo waweke juu,nikamwomba aweke juu akagoma katu katu,akaishia kuniuliza wewe unajua unaongea na nani nikamwambia siitaji kujua naongea nani wakati wa safety yako yangu na ndege kwa ujumla.akasema naomba jina lako nikamtolea bussiness card nikampa.akasema sitoi.nikamwambia kwa upole tena baada ya kunijulisha naitwa mh ngulume mkuu wa wilaya ya...nikamwambia sawa mama yangu labda in short naomba tuweke mizigo juu akagoma katakata akadai nikamwite bosi wangu nikamwambia hata nikimwita nakuhakikishia ndege aiondoki ama uhame hapa ama niweke mizigo juu,nikaenda kumwita CAPT MAZULA (marehemu) akamwambia mama nini tatizo jamani hilo ni swala la safety yako na yetu...mama nikaona ananyanyuka akahamia kiti cha tatu nyuma..huku akidai ndio mana napandaga PRECISSION AIR nikamwomba Mungu nisijibu kitu,WAKTI WA KUSHUKA akasema kijana nextytym jua wakubwa wako akiwa anashuka nikamwambia ahsante mama...the day after nikaitwa ofisini bahati capt aliandika nikaandika kwenye report so aikutuumiza kichwa,mama akaenda kupiga simu sijui kwa top gani nikaitwa nikajieleza nikamwambia na huyo bosi sitoenda kinyume na nilichofunzwa hasa wakati inapofika swala la safety ...akuhamini akasema ulikuwa right nikamwambia yeye nani..magufuli alikata economy sikuhiyo akakaa emergency sit akaweka mzigo nikamwelekeza poa akaelewa yule baba akataka aweke juu nikamwambia ntauweka mimi loh yule baba alishuka akashukuru niaksema nini ukuu wa WILAYA,wakipewa UWAZIRI si balaa we jiulize miaka 18 ukuu wa wilaya pekee ujiulizi una tatizo gani

tusilipe baya kwa baya mama MUNGU NINEMUAMINI ANAKWENDA KUKUAMSHA HAPO ULIPO LA MAANA TUBU DHAMBI NIMESOMA HAPO JJUU KUNA WENGI ULIWAKOSEA UJUI WALIONGEA NINI ILA MUNGU NI MUNGU WA MSAMAHA...AIJALISHI ULITENDA DHAMBI GANI KISHA MPOKEE YESU KAMA BWANA NA MWOKOZI WA MIASHA YAKO KIRI UPONYAJI NA KATAA KIFO ZAB 118

UBARIKIWE MAMA
 
Tatizo lake nadhani alikuwa anasema sana na kuitetea serikali lakini hakufikiria kuiba, angeiba asinge omba msaada wa serikali angejitibia mwenyewe....

Kule Bagamoyo alikuwa analimisha wafungwa....halafu fungu la mbio za mwenge la kwake bonafsi
 
DCs wapanguliwa na kustaafishwa
Habari zilizopatika na ni kuwa DCs wamapanguliwa na wengine kustaafishwa bila shaka tuna wanachama wa JF waliopewa SHAVU.
RAIS KIKWETE AFANYA MABADILIKO YA WAKUU WA WILAYA

RAIS Jakaya Kikwete amefanya mabadiliko ya Wakuu wa Wilaya chini kwa kuwateua wapya 15, kuwastaafisha wengine saba na kuwabadilisha vituo vya kazi 54.

Taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Waziri Mkuu (TAMISEMI) imeonyesha pia kuwa Wakuu wa Wilaya wawili watapangiwa kazi nyingine na wengine wawili wameteuliwa hivi karibuni kuongoza Jumuiya za Chama Tawala.

Mabadiliko haya yanatarajiwa kuongeza chachu katika usimamizi na ufuatiliaji wa shughuli za maendeleo ili kuiwezesha Serikali kufikia malengo yake, kwa mujibu wa taarifa hiyo.

Wakuu wapya wa Wilaya walioteuliwa ni Bi. Mercy Silla (Arumeru, Arusha), Bw. Norman Sigalla (Hai, Kilimanjaro), Col. Issa E. Njiku (Misenyi, Kagera), Bi. Angelina Mabula (Karagwe, Kagera), Dkt. Rehema Nchimbi (Newala - Mtwara), Francis Isaac (Mbulu, Manyara), Lt. Col. Benedict K. Kitenga (Rorya, Mara) na Lt. Col. Cosmas Kayombo (Mbarali, Mbeya).

Wengine ni Bw. Christopher Ryoba Kangoye (Kwimba, Mwanza); Bi. Queen Mwanshinga Mlozi (Ukerewe, Mwanza); Bi. Fatuma Mwassa (Mvomero, Morogoro); Bi. Fatma Ally (Nanyumbu, Mtwara); Bw. Juma Solomon Madaha (Tunduru, Ruvuma); Bw. Anatory Choya (Kishapu, Shinyanga) na Bw. Erasto Sima (Korogwe, Tanga).

Wakuu wa Wilaya waliostaafishwa na vituo vyao kwenye mabano ni Bw. Elias Maarugu (Misenyi, Kagera); Bw. Deusdedit Mtambalike (Muleba, Kagera); Bw. David Holela (Babati, Manyara); Bi. Hawa Ngulume (Mbarali, Mbeya); Bw. Mashimba H. Mashimba (Kyela, Mbeya); Col. Peter Madaha (Nyamagana, Mwanza) na Bw. Gilbert Dololo (Kibaha , Pwani).

Wakuu wa Wilaya ambao wamepangiwa kupewa kazi nyingine ni Bw. Patrick Tsere aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Ilala (Dar es Salaam) na Bi. Doreen Kisamo aliyekuwa Uyui (Tabora).

Bw. Martin Shigela aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Lindi (Lindi) aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UVCCM wakati Bi. Husna Mwilima aliyekuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai (Kilimanjaro) aliteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa UWT​
 
Alimpiga makofi mtendaji mmoja kule Mbarali...labda haya ndio malipo yenyewe...si aliolewa na kaka wa JK huyu?Na mbona Sheikh wa CCM hamsaidii ?

Sio hayo tu. Huyu mama alichowafanya wafugaji wa mbarali kwa kisingizio cha kuwahamisha ihefu, ni Mungu pekee anayejua. Kuna tume ya jaji mmoja ambayo iliundwa kuchunguza maovu ya zoezi la kuwahamisha wafugaji na ripoti haija anikwa hadharani mpaka leo. Nasikia waliwalazimisha Wasukuma kuuza ng'ombe kwa shs 5,000 ili kulipa faini hewa, halafu kaka yake anawanunua hao ng'mbe!!!! Pia kwenye sakata hili, Mkuu wa mkoa wa Mbeya, Mwakipesile alihusika kwa namna fulani.
 
2006-10-13 08:45:49
Na Nico Mwaibale , PST Mbarali


Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya, Bi. Hawa Ngulume, amemzaba kibao usoni, Mwenyekiti wa Wakulima wa Kijiji cha Kapunga baada ya wakulima hao kuuzuia msafara wa Kamati ya Bunge ya Kilimo na Ardhi.

Baadhi ya wabunge wa Kamati hiyo waliofuatana na Bi.Ngulume ni Bw. Fred Mpendazoe Tungu(Kishapu- CCM), Mwadini Jecha(Wete- CUF), Bw. Castor Ligalama (Kilombero- CCM) na Shally Raymond( Viti Maalum- CCM).

Wananchi hao waliuzuia msafara wa kamati hiyo, wakitaka wapewe ufumbuzi wa manyanyaso, waliyodai kuyapata kutoka kwa mwekezaji kampuni ya Export Trading Limited na kuwaondoa kwenye makazi yao.

Kitendo hicho kilisababisha mvutano mkubwa kati ya wakulima hao na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Bi. Hawa Ngulume.?

Mvutano huo ulidumu kwa takriban dakika 10, ndipo Bi. Ngulume alipopandwa na jazba na kumzaba kibao cha usoni Mwenyekiti wa Wakulima hao, Bw. Ofred Mkemwa.

Mbali na kumnasa kibao Mwenyekiti huyo pia Bi. Ngulume, aliwaniga kabali baadhi ya wananchi waliokuwa kimbelembele katika kufunga barabara hiyo, wakitaka kuzungumza na Wabunge wa Kamati hiyo.

Kwa mujibu wa wananchi hao, kampuni hiyo ya Export Trading Ltd, imewazuia kutumia mfereji wa maji, waliokuwa wakiutumia kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani na kumwagilia mashamba.

Walisema kitendo cha mwekezaji huyo ni kinyume na maelezo yaliyotolewa awali na viongozi wa Serikali, ambao walisema mwekezaji huyo atawasaidia wananchi na wakulima wadogo wanaoishi karibu na shamba lake.

Waliongeza kuwa mwekezaji huyo amewafukuza walimu wa Shule ya Msingi Kapunga kwenye nyumba walizokuwa wakiishi, zilizopo ndani ya shamba lake.

Walisema mwekezaji huyo ametaka walimu hao waende wakatafute makazi mengine, nje ya eneo la shamba, licha ya kwamba shule hiyo ni ya Serikali, ambayo ilijengwa kwa ajili ya watoto wa watumishi wa shamba hilo na wananchi wa jirani.?

Juhudi za Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw. Christopher Chizza za kujaribu kuwasihi wananchi hao kutulia, ziligonga mwamba kutokana na wananchi kupandisha jazba.

Hali hiyo pia ilimfanya Mkuu huyo wa Wilaya, kuwafokea na kuwasukuma wananchi hao wakati wakizuia njia ili Wabunge wateremke na kuzungumza nao.?

Katika kikao cha majumuisho kilichofanyika kwenye ukumbi wa shamba hilo, Bi. Ngulume aliwaeleza Wabunge hao kuwa, wasiwe na wasiwasi na maneno ya wananchi kwa kuwa yote ni majungu ya kupikwa na baadhi ya watu na yasiyokuwa na ukweli wowote.?

SOURCE: Nipashe
 
Kwanza nampa pole huyu mama na ninamsikitikia sana. Pili, amekuwa practical lesson kwa waliobahatika kukutana naye alipokuwa na madaraka. Kupiga watu makofi ilikuwa kawaida yake, na wala sikusikia amekamatwa na kushitakiwa kwa shitaka la 'shambulio' (kumbuka yule kijana aliyempiga Mzee Ruksa kofi alishtakiwa kwa kosa hilo na kufungwa jela mwaka mmoja). Huyu mama alipokuwa mkuu wa wilaya moja ya Dar es salaam alimzaba makofi kijana mmoja mwanafunzi wa chuo kikuu alipokuwa anamlaumu huyo mama kwa kuchelewa kumsainia fomu yake ya kuomba mkopo wa shule. Maneno 'tumeshinda hapa kutwa nzima hadi tumekosa masomo' yalimuudhi sana huyu mama, akamzaba vibao vya nguvu kijana wa watu akajiondokea amejiinamia, na ikatangazwa kwenye magazeti kama vile ni habari njema sana! Na tena kuna hiyo kesi ya huko Mbarali ambako mama huyuhuyu alimzaba vibao kiongozi wa kijiji mbele ya ushahidi mzito wa kamati ya bunge. Baba wa watu akabaki anajisitikia na aibu ya kupigwa hadharani. Mama Ngulume hakushtakiwa, badala yake vyombo vya habari viliripoti kama vile ni Twiga Stars imeifunga Brazil, akaendendeleza ubabe!

What goes around comes around. Pengine ni zamu yake leo kuonja japo kidogo mateso ya binadamu wenzake. Haifai kushangilia hata kidogo, hata walipopigwa makofi hao watu sikushangilia, lakini tulitaarifiwa. Na leo tumetaarifiwa kuwa na yeye yamemkuta. Tunasikitika pamoja. Pole sana Mama Ngulume, ndiyo maisha.
 
2006-10-13 08:45:49
Na Nico Mwaibale , PST Mbarali


Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, mkoani Mbeya, Bi. Hawa Ngulume, amemzaba kibao usoni, Mwenyekiti wa Wakulima wa Kijiji cha Kapunga baada ya wakulima hao kuuzuia msafara wa Kamati ya Bunge ya Kilimo na Ardhi.

Baadhi ya wabunge wa Kamati hiyo waliofuatana na Bi.Ngulume ni Bw. Fred Mpendazoe Tungu(Kishapu- CCM), Mwadini Jecha(Wete- CUF), Bw. Castor Ligalama (Kilombero- CCM) na Shally Raymond( Viti Maalum- CCM).

Wananchi hao waliuzuia msafara wa kamati hiyo, wakitaka wapewe ufumbuzi wa manyanyaso, waliyodai kuyapata kutoka kwa mwekezaji kampuni ya Export Trading Limited na kuwaondoa kwenye makazi yao.

Kitendo hicho kilisababisha mvutano mkubwa kati ya wakulima hao na Mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Bi. Hawa Ngulume.?

Mvutano huo ulidumu kwa takriban dakika 10, ndipo Bi. Ngulume alipopandwa na jazba na kumzaba kibao cha usoni Mwenyekiti wa Wakulima hao, Bw. Ofred Mkemwa.

Mbali na kumnasa kibao Mwenyekiti huyo pia Bi. Ngulume, aliwaniga kabali baadhi ya wananchi waliokuwa kimbelembele katika kufunga barabara hiyo, wakitaka kuzungumza na Wabunge wa Kamati hiyo.

Kwa mujibu wa wananchi hao, kampuni hiyo ya Export Trading Ltd, imewazuia kutumia mfereji wa maji, waliokuwa wakiutumia kwa matumizi mbalimbali ya nyumbani na kumwagilia mashamba.

Walisema kitendo cha mwekezaji huyo ni kinyume na maelezo yaliyotolewa awali na viongozi wa Serikali, ambao walisema mwekezaji huyo atawasaidia wananchi na wakulima wadogo wanaoishi karibu na shamba lake.

Waliongeza kuwa mwekezaji huyo amewafukuza walimu wa Shule ya Msingi Kapunga kwenye nyumba walizokuwa wakiishi, zilizopo ndani ya shamba lake.

Walisema mwekezaji huyo ametaka walimu hao waende wakatafute makazi mengine, nje ya eneo la shamba, licha ya kwamba shule hiyo ni ya Serikali, ambayo ilijengwa kwa ajili ya watoto wa watumishi wa shamba hilo na wananchi wa jirani.?

Juhudi za Naibu Waziri wa Kilimo, Chakula na Ushirika, Bw. Christopher Chizza za kujaribu kuwasihi wananchi hao kutulia, ziligonga mwamba kutokana na wananchi kupandisha jazba.

Hali hiyo pia ilimfanya Mkuu huyo wa Wilaya, kuwafokea na kuwasukuma wananchi hao wakati wakizuia njia ili Wabunge wateremke na kuzungumza nao.?

Katika kikao cha majumuisho kilichofanyika kwenye ukumbi wa shamba hilo, Bi. Ngulume aliwaeleza Wabunge hao kuwa, wasiwe na wasiwasi na maneno ya wananchi kwa kuwa yote ni majungu ya kupikwa na baadhi ya watu na yasiyokuwa na ukweli wowote.?

SOURCE: Nipashe


i luv u JF
 
What an ugly end of an era! Juzi nilihudhuria semina moja ambako mkufunzi alifundisha kuwa kila tukio lina chanzo na kila tendo lina tokeo. Hapa na wengine wajifunze kitu kwenye hili darsa la mama Ngulume.
 
malipo ya Mungu ni hapahapa duniani,wakati ananguvu alikuwa anatoa maneno machafu mdomoni hakujua siku moja ataijua taabu,Eeeeeeeeeeee Mungu libarikiwe jina lako.
Wewe ni Mungu wa Kisasi.AMEN

Kagemuro,

Chembe ndogo tu ya utu inahitajika. Umeenda mbali mno. Mungu si wa kisasi ni mwingi wa huruma please!
 
Kagemuro,

Chembe ndogo tu ya utu inahitajika. Umeenda mbali mno. Mungu si wa kisasi ni mwingi wa huruma please!

Huyu hastahili huruma yoyote kwani alikuwa mjivuni mno enzi zake, wacha mungu amuadhibu ili liwe fundisho kwetu na wengine pia
 
DC wa zamani hoi kitandani Send to a friend Monday, 08 November 2010 01:13 0diggsdigg

hawangulume.jpg
Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Mbalali, Mkoani Iringa Hawa Ngurume, akizungumza na waandishi wa habari wa gazeti hili, nyumbani kwake Goba Kinzidi, Dar es Salaama jana, kuhusu maradhi ya figo yanayomsumbua. Picha na Venance Nestory

Raymond Kaminyoge
ALIYEKUWA mkuu wa Wilaya ya Mbarali, Hawa Ngulume yuko katika hali mbaya nyumbani kwake, Goba Kinzudi jijini Dar es Salaam akisumbuliwa na ugonjwa wa vichomi na mapafu.

"Nimeona nitumie chombo cha habari kufikisha ujumbe (wa ugonjwa) kabla sijafa," alisema mkuu huyo wa zamani wa alipoongea na Mwananchi.

Akizungumza na Mwananchi nyumbani kwake jana, Ngulume alisema kwa miezi mitatu sasa yuko hoi na hawezi kutembea bila kusaidiwa na hivyo anaiomba serikali imsaidie aweze kwenda kutibiwa nje ya nchi.
Alisema ameamua kutumia gazeti hili kufikisha ujumbe kwa serikali na CCM kuhusu maradhi yanayomsumbua baada ya njia nyingine kushindikana.

"Nilipeleka taarifa kwnye chama changu kwamba ninaumwa nahitaji msaada, lakini sikujibiwa; pia nimefanya juhudi za kutaka kumwona Waziri Mkuu ili anisaidie, lakini juhudi hazikuzaa matunda. Nimeona nitumie chombo cha habari kufikisha ujumbe kabla sijafa," alisema.

Ngulume, ambaye ni kada maarufu wa CCM aliyetumikia nafasi ya ukuu wa wilaya kwa miaka 18, alisema maradhi hayo yalianza kumsumbua baada ya kumalizika kwa mchakato wa kura za maoni za chama hicho.

Alisema aliomba ridhaa ya chama hicho kimsimamishe kuwa mgombea ubunge katika Jimbo la Singida Mjini.
"Katika mchakato ule Mohammed Dewji alishinda, na mimi nikawa mshindi wa pili. Niliporudi Dar es Salaam nikaanza kujiandaa kwenda kumpigia debe mshindi kama ulivyo utaratibu wa chama chetu, ndipo nikaanza kuumwa ghafla," alisema.

Mkuu huyo wa zamani wa wilaya ambaye amewahi kushika wadhifa huo kwenye wilaya mbalimbali zikiwemo za Bagamoyo, Ilala na Kibaha, alisema amekuwa akitibiwa katika hospitali za Lugalo, IMTU na Ocean Road
"Kuna kipimo ambacho nilitakiwa kuwekewa kwenye kinywa katika Hospitali ya Ocean Road ili kiweze kubaini kama kwenye mapafu kuna maji au la, lakini ilishindikana kwa sababu ya kukosa pumzi, na hawana kipimo cha aina nyingine," alisema.

Alishauriwa kwamba aendde India ambako kuna vipimo vya aina nyingi ambavyo havihitaji kuwekwa katika kinywa na kwamba vipimo hivyo vingemfaa kutokana na matatizo yake ya pumzi.

Alisema katika kuhangaika alifika katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, lakini cha kushangaza alikaa kuanzia saa 8.00 mchana hadi saa 11.00 jioni bila kuhudumiwa.

"Ndipo mtu mmoja anayenifahamu aliyekuwa akipita nilipoketi, akanisalimia kwa kuniita mheshimiwa. Muuguzi mmoja jina ninalihifadhi akaja kutaka kunihudumia, nikamwambia ina maana siwezi kupata huduma hadi niwe mheshimiwa, nikaondoka kwa hasira," alisema.

Alisema baada ya kutelekezwa na kunyanyapaliwa Muhimbili, amekuwa akipata matibabu kwenye hospitali za binafsi kwa ajili ya kutuliza maumivu.

"Maumivu ninayoyapata ni makali sana, nina vichomi utadhani kuna msumemo unaokata viungo vyangu ndani ya tumbo. Ninalia usiku kuchwa kwa maumivu, wanaonisaidia ni majirani tu ambao hufika kila mara kunijulia hali," alisema.
source:mwananchi

hili limenishtua ..lakini hii ndio picha halisi

Hawa Ngulume sema ukweli unachoumwa mama.....mbbona dawa zipo tu?? Kufa kila mtu atakufa. Nakumbuka ulivyokuwa mkuu wa wilaya ya Bagamoyo ulikuwa unafunga safari hadi Chalinze ukawa unawafukuza madereva wa malori makubwa wasipaki chalinze kumbe yule bwanako dereva alikuwa amekutosa akawa kapata dogodogo chalinze uliposikia kuwa sababu ya wewe kutoswa ni huyo dogodogo ukawa unafika chalinze usiku kuwatimua madereva eti wasilale chalinze....yule dereva ni ndugu yangu yuko hoi kitandani, majipu, homa kuharisha yani ni vurugu mechi.
Alafu hawa, nina uhakika Mkwere ulikuwa unatoka nae ...
Ushauri wangu, OKOKA
 
Back
Top Bottom