DC Bukoba aamuru walimu wachapwe mboko!

Mkuu wa wilaya aamuru polisi kucharaza bakora walimu 32

"Hilo ni tukio la aina yake na lakusikitisha sana kwa sababu binadamu hawezi kuongozwa njia kwa kuswagwa kama ng'ombe... ni lazima serkali ichukue hatua kali dhidi ya wahusika".[/SIZE][/FONT]

Binadamu hawezi kuongozwa kwa kuswagwa kama ng'ombe....excellent! Wanafunzi wanalambwa viboko kila siku na hakuna anayesema kitu, ina maana wao si wanadamu na ni sawa na ng'ombe? Hii adhabu ya viboko nimekuwa nikiipinga toka zamani lakini naona waalimu hawako tayari kutumia njia nyingine mbadala za kuwadiscipline, sasa sijui ndo tuseme..mkuki kwa nguruwe.......? Sifagilii alichofanya Mkuu wa wilaya lakini labda huu ndio utakuwa mwanzo wa mwisho wa adhabu za viboko mashuleni, and am sure kwa kuwa waalimu sasa wanaujua 'utamu wa bakora' watakuwa wakifiria mara mbilimbili kabla ya kutumia adhabu hii ya kikatili katika karne hii!
 
Mkuu kama ndo hivyo kila mtu angekuwa anajivunjia sheria.
Ndo maana wewe ukisimamishwa na trafic utasimama au polisi akija kukukamata utatii amri kwa nini usikatae na yule ni boss wao.
trafic akikusimamisha anakuwa hajavunja sheria na wala hajakuvunjia wewe haki yako. lakini akikukuta na kosa akakwambia shuka ulale chini nikuchape... utakubali? huu mfano haundani na issue on the table

kwani hao walimu walishikiwa mtutu?
 
Hapa hakuna cha DC wala Washington ,kilichopo hapa ni uwoza wa CCM hakuna lingine ,cha kushughulikiwa kila nikikaa na kupima naona ni CCM tu ,watawala hawa baada ya miaka 47 ya utawala wao imetosha na hakuna haja ya kuwapigia debe au kuwakokota kila tunapotaka kwenda ,Utawala wa CCM umeshapotea wala hakuna njia ya kuwarudisha kwenye mstari dawa ambayo itawaweka matumbo joto ni kuiondoa kwenye madaraka tu, mambo kama haya yanayotokea si bora kuwasakama maDC na wengineo dawa yao ni kukisakama Chama chao kizima na wala si kumkaba koo Kikwete hapana ,dawa ni hiyohiyo moja kukisama Chama kizima kuwa kimeoza na hakifai kuwepo madarakani ,wananchi waelimishwe na wataelewa tu mbona WaZanzibari wameelewa na wanaendelea na mkakati wa kuiondoa CCM madarakani kwa nguvu ,si unaelewa kuna watu wakikaa sehemu sio ya kwao na ukiwambia waondoke wanakwambia haondoki mtu ila zikitumika nguvu itabidi aondoke maana kitini hapatakalika.

Hivyo nguvu na vifijo viwe kuikatalisha CCM kwa wananchi hakuna jingine kama si leo au kesho mwishowe wananchi watashika kasi na kupata nguvu mpya ,hii michezo inayochezwa na CCM si michezo ya kuheshimiana ni michezo ya kudharau kabisa ,na hasa wanapokuwa na ukubwa wa kuongoza watu wanakuwa na kiburi na matokeo yake ndio hayo ya kujifanyia watakavyo ,akiamini kuwa hata akiondolewa DC atapelekwa sehemu nyengine. Kwani kama kungekuwa na uhakika wa mtu yeyote kufanya vioja visivyolingana na sheria za nchi kuchukuliwa hatua za kisheria ,basi si wote wangelivuka wengine wangenasa na kuwa ni fundisho kwa wengine ,lakini tamaa iliyojengeka ndani ya utawala wa CCM ni ile kuwakingia vifua viongozi majeuri,wengi wa viongozi hawa ni wale walioteuliwa tu kushika nyadhifa mbalimbali kwenye serikali hii ya CCM ,ama kwa kulipwa kutokana na uibaji mzuri wa kura au kuonekana ni mbabe wa wengine hivyo anaweza kuamrishwa na walio juu yake kufanya lolote ,hana wasiwasi atalindwa.

CCM na utawala wake wanajificha kwa kusema watafuatilia ,watachunguza ,na kurudi kwa wananchi kuwaelezea, wakishasema hivyo ndio imetoka hiyo ,mambo yashasawazishwa na husikii tena mpaka azuke mbabe mwengine na kutenda jambo na wananchi kuhamishiwa upande mwengine na nyimbo nazo hubadilika na kuwekwa usanii mwengine.

CCM kama chama tawala ambacho kipo madarakani tokea Uhuru wa Nchi mbili hizi kusema kweli kimeshavurugika na kilichobaki ni kutumia maguvu kukaa madarakani lakini kwa sifa za kuongoza Nchi hakina tena ,maana mkishafika kuwa hamuwezi tena kuchukuliana hatua inamaana serikali iliyokuwepo haina nguvu juu ya wahusika wake kila mmoja anamwogopa mwenzake, hali hiyo inapofikia ni hatari sana na ili kuiwahi isiendelee ni lazima utawala ubadilishwe ili kupisha Chama kingine aidha vyama vingine ambavyo nina uhakika vitaweza kuunda serikali shirikishi na kushirikisha vyama vyote ,ili kuondoa mvutano ,lakini kuendelea na CCM kuwepo madarakani ni kupoteza muda wa Mtanzania kupiga hatua.
 
nafikiri sasa kikwete anagundua kuwa alichagua wajinga kuwa viongozi. u cant imagine a DC ambaye anajua rule of law and discplinary machinery anaamuru watu kufanya kitendo kama hicho. na utashangaa watu wengine watasema hiyo ndio dawa. Polisi wetu wana nidhamu ya woga na hao Ma DC huku kwingine wamebadilika na kuwa marais wadogo so they can do whatever they want in their area. it is a shame that such a nasty thing may happen in a country boosting that it adhere to rule of law and respect of human dignity. while other a raising voice against canning a part of punishment others support it with all his power. he must be vindicated by his own action.
 
..hao waalimu nao wajinga. kwanini walikubali kuchapwa viboko? ningekuwa kati ya hao waalimu huyo DC angenitambua.
 
Kwa mujibu wa BBC Dira ya dunia leo waalimu huko Bukoba wamepanga kuandamana....naweza kuona sababu ya mgomo mwingine?

LHRC wanasema DC kavunka misingi ya utawala wa sheria.

Mwalimu mmojawapo aliyechapwa amehojiwa na kujieleza jinsi walivochapwa....aliitwa akiwa darasani na mwalimu mkuu wake, na DC alipowauliza kwa nini wanachelewa, walimwambia wanakaa mbali na ni kwa sababu hakuna nyumba za kuishi za serikali. Kuna mwanamke amechapwa viboko vinne matakoni. Mwendo ulikuwa: "Koplo fanya kazi yangu"! Kumbe walifungiwa ndani masikini!
 
Kwa ufupi sana nadhani uwezo wa wateule wengi ni mdogo kupindukia,hawana kazi za kufanya,hawajui majukumu yao kwa ufasaha kila kitu ni siasa mtindo mmoja.
wengi wa wateule hasa RC na DC hawana kazi za kufanya zaidi ya kumpokea rais kama ilivyoainishwa kwenye katiba ya Tanzania.Kazi zao pia zinaonekana hasa katika kipindi cha uchaguzi.RC & DC ni vyeo vilivyowekwa na wakoloni ili waweze kututawala na kutugandamiza kwa faida ya mkoloni.Mikoani na wilaya tayari kuna mlolongo mkubwa wa wataalamu wanaojitosheleza.Tanzania imezalisha vyeo kibao kwa manufaa ya siasa zaidi kwa mfano katika wilaya kuna DC,District Administrative Secretary,Distrct Director {Local Government},MP na Mayor.Ukiangalia wingi wa hawa wateule unashindwa kuelewa wanafanya nini au wana umuhimu gani katika maendeleo ya taifa letu letu masikini!.MaDC wengi ni wanajeshi wasiokuwa na ujuzi na uzoefu wa uongozi,wanachokifanya ni kukusanya data kutoka kwa wataalamu wa sector mbali mbali kama elimu,kilimo,afya na nk na kuzitoa kwa wakuu wao wakati wa ziara zao huko mikoani na wilayani,sijui kama Tanzania bado tunahitaji kusikiliza risala za kisiasa zisizokuwa na uhusiano na maisha hallisi ya watanzania wengi wasiokuwa na uhakika wa milo mitatu kwa siku.
 
Kwa ufupi sana nadhani uwezo wa wateule wengi ni mdogo kupindukia,hawana kazi za kufanya,hawajui majukumu yao kwa ufasaha kila kitu ni siasa mtindo mmoja.
wengi wa wateule hasa RC na DC hawana kazi za kufanya zaidi ya kumpokea rais kama ilivyoainishwa kwenye katiba ya Tanzania.Kazi zao pia zinaonekana hasa katika kipindi cha uchaguzi.RC & DC ni vyeo vilivyowekwa na wakoloni ili waweze kututawala na kutugandamiza kwa faida ya mkoloni.Mikoani na wilaya tayari kuna mlolongo mkubwa wa wataalamu wanaojitosheleza.Tanzania imezalisha vyeo kibao kwa manufaa ya siasa zaidi kwa mfano katika wilaya kuna DC,District Administrative Secretary,Distrct Director {Local Government},MP na Mayor.Ukiangalia wingi wa hawa wateule unashindwa kuelewa wanafanya nini au wana umuhimu gani katika maendeleo ya taifa letu letu masikini!.MaDC wengi ni wanajeshi wasiokuwa na ujuzi na uzoefu wa uongozi,wanachokifanya ni kukusanya data kutoka kwa wataalamu wa sector mbali mbali kama elimu,kilimo,afya na nk na kuzitoa kwa wakuu wao wakati wa ziara zao huko mikoani na wilayani,sijui kama Tanzania bado tunahitaji kusikiliza risala za kisiasa zisizokuwa na uhusiano na maisha hallisi ya watanzania wengi wasiokuwa na uhakika wa milo mitatu kwa siku.


Mimi nakumbusha jamani ukoloni upo na uhuru uliopatikana ulikuwa ni kwa wachache na hao wala hawajawa huru...kwa sababu kawaida wakoloni wa mwanzo walivukuwa ni kuwa wameathiri uwezo wetu wa kawaida wa kufikiri na kutupandikizia akili ambayo inatufanya tufikiri kuwa uhuru ni KUWA KAMA WALIVOKUWA WAO. Na wao walivokuwa ni hiyo hali ya KUTAWALA. Hatujabadilisha hali, tumebadili watu!

Ndo maana ni muhimu kwa mapambano ya kutubadili kwanza namna tunavofikiria tuache kufikiria kama wao na kuwa kama wao..tufikirie na kutenda kama Binadamu!
 
Mimi nakumbusha jamani ukoloni upo na uhuru uliopatikana ulikuwa ni kwa wachache na hao wala hawajawa huru...kwa sababu kawaida wakoloni wa mwanzo walivukuwa ni kuwa wameathiri uwezo wetu wa kawaida wa kufikiri na kutupandikizia akili ambayo inatufanya tufikiri kuwa uhuru ni KUWA KAMA WALIVOKUWA WAO. Na wao walivokuwa ni hiyo hali ya KUTAWALA. Hatujabadilisha hali, tumebadili watu!

Ndo maana ni muhimu kwa mapambano ya kutubadili kwanza namna tunavofikiria tuache kufikiria kama wao na kuwa kama wao..tufikirie na kutenda kama Binadamu!

Duuhh; yaani walimu wa kike, baadhi, walichapwa makalioni?
CWT taifa inabidi wafikilie jinsi gani ya kukomesha hili swala, lisije jitokeza tena. Je CWT wameshatoa tamko, kama walivyo dai? Na wataandamana lini hao wa Bukoba?
 
Duuhh; yaani walimu wa kike, baadhi, walichapwa makalioni?
CWT taifa inabidi wafikilie jinsi gani ya kukomesha hili swala, lisije jitokeza tena. Je CWT wameshatoa tamko, kama walivyo dai? Na wataandamana lini hao wa Bukoba?

Ndo maana yake,, mara ya kwanza tangu nchi 'kupata uhuru', hawajasema ni lini hasa wataandamana ila wana mpango huo.
 
..hao waalimu nao wajinga. kwanini walikubali kuchapwa viboko? ningekuwa kati ya hao waalimu huyo DC angenitambua.

JK kwa kweli hao waalimu na wenyewe ni tatizo tosha.....mtu mzima utege makalio na mwingine achape mboko!! hata kama ni nani lazima itakuwa ngumu....that ridiculous kwa waalimu kutii amri ya DC!! nina wasi wasi hao waalimu hata wangeambiwa na mkuu wa wilaya wavue nguo wange tii
 
Tatizo la msingi Hapa Sio Mwingine zaidi Ya hawa waalimu wenyewe
...How dare ...wamekubali kufanywa walichokifanaya!

Ni umbumbu usio na kisi...Kama wangekuwa wakamilifu kama watu....Wangekataa mwanzo mpka mwisho..That is all!!!
 
..hao waalimu nao wajinga. kwanini walikubali kuchapwa viboko? ningekuwa kati ya hao waalimu huyo DC angenitambua.

Walimu sio wajinga lakini umasikini walionao ndio uliowafikisha hapo walipo ,wamewekwa bila ya mishahara kwa muda mrefu na bado hadi wanapigwa hawajapokea mshahara wala malimbikizo.

Wamewaweka na njaa mpaka akili zimewatoka na hawajui mwisho wa kukaa bila ya mishahara itaendelea mpaka lini ,ila kwa kuwasaidia mishahara itakuwa ikifuata wakati utakapowadia msimu wa uchaguzi mkuu wajue kila kitu watalipwa na malimbikizo watalipwa na nyongeza wataongezewa ili wasifu kuwa CCM ndio baba au CCM ndio chama,haya yote wanayofanyiwa wao pamoja na wanafunzi hata wale wa mlimani na kwengineko ,watayasahau yote haya wanayofanyiwa na kuiunga mkono CCM kwa hali ya juu kabisa.

Si ajabu hata wanafunzi waliofukuzwa nao wakarudishwa na kulipwa siku zao zote na kama hazijatosha wakaongezwa watafanyiwa mambo ambayo yatawasahaulisha matatizo kiasi ya kupita uchaguzi CCM wanacharuka na kuanza kuwahenya na kuwaletea polisi kuwapiga marungu na bakora.
Hawa walimu ndio mstari wa mbele kuwahimiza wanafunzi kwenda kumpokea Kikwete akiongozana na DC,Dc ambae amewapiga bakora Kikwete ambae hakumuwajibisha DC mara aliposikia (Si kweli kwamba Mheshimiwa raisi hajasikia jambo hili,si kweli kwamba Waziri Mkuu hajasikia jambo hili si kweli kwamba waziri wa Elimu hajasikia jambo hili). Walimu na wanafunzi sijui kama watayakumbuka haya na kuwanyima kura viongozi wa Chama kilichoko madarakani na badala yake kama kawaida yao nao hutumika kuisimika CCM madarakani kama wanavyotumika polisi na wenginetele.

Walimu na wanafunzi pamoja na mapolisi si watu wanaofaa kuilalamikia serikali iliyopo madarakani serikali ya CCM kuwa haiwatendei haki,kwani wao ndio wasimamizi wakuu kwa kila kitu,iweje leo walalamike kwa mambo waliyoau wanayotendewa na mtawala waliemsimika na kila kukicha au uchaguzi ,hawakumbuki shida na matatizo yanayosababishwa na kile chama wanachokiweka.

CCM haina hati miliki ya nchi hii ni Chama cha siasa kama vilivyo vyama vingine ,hivyo kinapovuruga na kupoteza dira katika kuliongoza Taifa na kufanya mambo ya ajabu ajabu ni vyema wananchi kwa pamoja wakashirikiana kukiondoa madarakani iwe kwa kura na kama hawataki kuondoka kwa kura waondolewe kwa nguvu za wananchi njia ambayo hadi sasa haijaiwacha serikali jeuri madarakani ,ni serikali nyingi tu zilizokuwa zikitegemea vyombo vya dola zimeondolewa madarakani kwa nguvu za wananchi ,watu waliomo serikalini ni wachache sana na ni rahisi kuwaondoa madarakani kwa kutumia nguvu za wananchi ,msisikie ikiwa wananchi wataamua na kuwambia CCM kuwa imetosha kukaa madarakani kwa kipindi cha miaka 47 sasa muondoke au tutawaondoa kwa nguvu ,basi wataondoka tu kwa Ukubwa wa Tanzania hii,itabidi wasalimu amri maana hata wao wenyewe wanajua kuwa wameshapoteza dira ya uongozi hili sio geni kwao ,CCM wanafahamu fika kuwa kuiongoza Tanzania kwa sasa kunahitaji meno makali ambayo hayana uswahiba ,kama alivyosema Mheshimiwa Kikwete mara tu alipoapishwa kuwa Uraisi wake hauna ubia ,maana yake ni hiyo kuwa atakuwa hana uswahiba lakini uongozi wa namna hiyo umemshinda kwa kuwa Chama kizima kimeoza hakuna wa kumtegemea hata mmoja kila mmoja anamshinda mwenziwe kwa ubabe,kila mmoja anajifanyia anavyotaka kila mmoja ana amri kuliko mwenziwe utafikiri tupo kwenye kambi ya mafunzo ya jeshi maana jeshini unatakiwa ufuate amri ya mwisho kuipokea na ndipo ulipo utawala wa Serikali ya CCM ,haufuati sheria za nchi haufuati maadilio ya uongozi ni varange varange tu ,sasa kama Chama hiki hakikung'olewa kwenye madaraka kifanywe nini ?

Wakiambiwa ibadilishwe KATIBA hawataki ,wakiambiwa TUME ibadilishwe hawataki kama si udikiteta ni kitu gani ,wakiambiwa mafisadi muwafunge hawataki,wakiambiwa wawafukuze kwenye Chama hawataki bado wanawakumbatia ,wakiulizwa fedha iliyorudishwa na mafisadi ipo wapi hawana jibu zaidi ya ubabaishaji sijui imepekwa kwenye mbolea ili kusaidia wakulima wakati juzi tu waliwahadaa wananchi wa mbea kununua kura zao kwa mfuko wa mbolea?
 
JK kwa kweli hao waalimu na wenyewe ni tatizo tosha.....mtu mzima utege makalio na mwingine achape mboko!! hata kama ni nani lazima itakuwa ngumu....that ridiculous kwa waalimu kutii amri ya DC!! nina wasi wasi hao waalimu hata wangeambiwa na mkuu wa wilaya wavue nguo wange tii

Mkuu Masanilo,

Kumbuka aliyewachapa ni Koplo na kwa mujibwa wa maelezo ni kuwa mwalimu wa kiume aliyejaribu kujitetea alichapwa fimbo zisizo na idadi,

Pili hawangeweza kujiorganise wagome kwa vile hii ilikuwa kama suprise kwao, na pia hali zao kisaikolojia zimefanywa nyonge kiasi kwamba sio rahisi wapinge amri ya mtu kama mkuu wa wilaya na kiukweli ndivyo watanzaniawengi tulivo

ndo maana tunahitaji mabadiliko ya namna tunavofikiri ili kuweza kufikia hapo tunapopenda kufika!
 
Kabla ya uhuru maDC wa kijerumani na kiingereza walifatana na watu waliojulikana kama walugaluga, waliwachapa mboko watu aliozembea kazi au kutolipa kodi ya kichwa. tumerithi sheria nyingi kutoka kwa wakoloni labda kunasheria ya coporo panishimenti inayomruhusu DC kumlamba mtu mboko.
 
All said and done,

Huyu DC sasa hivi yuko wapi?

Duh! Ama kweli viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe!

Hivi kweli, JK huyu appointee wake atamfanya nini?

Lets wait and see!
 
Mboko (coporo panishment) zilianzishwa na wajerumani inawezekana watz bila mboko hakiendi kitu tena wakati ule hata usipoenda kanisani padri anakuja na mboko.
 
All said and done,

Huyu DC sasa hivi yuko wapi?

Duh! Ama kweli viongozi wetu ni reflection yetu wenyewe!

Hivi kweli, JK huyu appointee wake atamfanya nini?

Lets wait and see!


Masanja

Sintoshangaa JK akimpa u RC kwa kazi nzuri alo ifanya ...
 
This is even worse than the proverbial "Unigambire styupidi ini fronti of mai waif?"

Huyu mkuu wa Wilaya anaonekana kuamini force zaidi kuliko reason, si ajabu watoto wanafeli.

Kama shule hazina vifaa, mpango mzima wa kiuchumi hautoi mazingira mazuri kwa elimu, na sababu nyingine lukuki ndizo mzizi wa tatizo hili utawachapa walimu viboko visivyo idadi na matokeo yatazidi kuwa mabaya zaidi tu.

Lakini tatizo rais mwenyewe Kikwete, mkuu wa wilaya unamtegemea aweje?
 
Huo ni uvunjaji wa haki za binadamu na pia amejichukulia sheria mkononi. Hana tofauti na wananchi ambao wanaojichukulia sheria mikononi kwa kuwachoma vibaka/majambazi. Huyo DC inabidi kwanza akapimwe akili zake kama ziko timamu then ashitakiwe na achukuliwe hatua kali za kisheria.

Nitashangaa kusikia DC huyo akiwa bado kwenye nafasi hiyo ifikapo kesho jioni. Inabidi asimamishwe kazi haraka iwezekanavyo!!!! Ebo!!!!!!!.
 
Back
Top Bottom